< Salmos 64 >

1 Oye, o! Dios, mi voz en mi oración: guarda mi vida del miedo del enemigo:
Sikia sauti yangu, Mungu, usikilize malalamiko yangu; unilinde dhidi ya hofu ya adui zangu.
2 Escóndeme del secreto consejo de los malignos: de la conspiración de los que obran iniquidad.
Unifiche dhidi ya mipango ya siri ya wafanyao maovu, unifiche dhidi ya watendao vurugu ya udhalimu.
3 Que afilaron su lengua, como espada: armaron por su saeta palabra amarga:
Wao wamenoa ndimi zao kama panga; wamelenga mishale yao, maneno machungu,
4 Para asaetar a escondidas al perfecto: de presto le asaetean, y no temen.
ili kwamba waweze kupiga kutoka mahali pa siri kwenda kwa mtu asiye na hatia; wampige yeye kwa ghafla nao wasihofu lolote.
5 Afírmanse asimismos sobre palabra mala: tratan de esconder los lazos: dicen: ¿Quién los ha de ver?
Wao wanahamasishana wenyewe katika kupanga uovu; wanashauriana pamoja wao binafsi ili kuweka mitego; nao husema, “Ni nani atakayetuona?”
6 Inquieren iniquidades; perficionan la inquisición del inquiridor, y lo que inventó lo íntimo de cada uno, y el corazón inventivo.
Wanabuni mipango ya dhambi; “Tumemaliza,” wanasema, “ni mpango makini.” Mawazo ya ndani na mioyo ya watu ni ya kina.
7 Mas Dios los asaeteará con saeta, de repente serán sus plagas.
Lakini Mungu atawapiga wao; ghafla watajeruhiwa kwa mishale yake.
8 Y harán caer sobre sí sus mismas lenguas: espantarse han todos los que los vieren.
Watafanywa kuwa mashakani, kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko kinyume nao; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao.
9 Y temerán todos los hombres, y anunciarán la obra de Dios, y entenderán su obra.
Watu wote wataogopa na kutangaza matendo ya Mungu. Kwa hekima watafikiria kuhusu kile yeye ametenda.
10 El justo se alegrará en Jehová, y asegurarse ha en él: y alabarse han todos los rectos de corazón.
Wenye haki watakuwa na furaha kuhusu Yahwe nao watakimbilia kwake; wote wenye haki moyoni watajivuna katika yeye.

< Salmos 64 >