< Salmos 57 >

1 Ten misericordia de mí, o! Dios, ten misericordia de mí; porque en ti ha confiado mi alma, y en la sombra de tus alas me ampararé, hasta que pasen los quebrantamientos.
Unihurumie, Mungu, unihurumie mimi, kwa maana ninakukimbilia wewe mpaka matatizo haya yaishe. Ninakaa chini ya mbawa za zako kwa ajili ya ulinzi mpaka huu uharibifu utakapoisha.
2 Clamaré al Dios Altísimo, al Dios que me galardona.
Nitakulilia Mungu uliye hai, kwa Mungu, afanyaye mambo yote kwa ajili yangu.
3 El enviará desde los cielos, y me salvará de la afrenta de él que me traga. (Selah) Dios enviará su misericordia y su verdad.
Yeye atatuma msaada kutoka mbinguni na kuniokoa, ana hasira na wale wanaonishambulia. (Selah) Mungu atanitumia upendo wake mwema na uaminifu wake.
4 Mi vida está entre leones: estoy echado entre hijos de hombres que echan llamas: sus dientes son lanza y saetas, y su lengua espada aguda.
Uhai wangu uko katikati ya simba; niko katikati ya wale walio tayari kunila. Niko katikati ya watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, na ambao ndimi zao ni kali kama upanga.
5 Ensálzate sobre los cielos, o! Dios: sobre toda la tierra se ensalce tu gloria.
Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu, utukufu wako uwe juu ya nchi yote.
6 Red han compuesto a mis pasos, mi alma se ha abatido: hoyo han cavado delante de mí, caigan en medio de él. (Selah)
Wao walisambaza nje wavu kwa ajili ya miguu yangu; nilikuwa na shida sana. Walichimba shimo mbele yangu. Wao wenyewe wameangukia katikati ya shimo! (Selah)
7 Aparejado está mi corazón, o! Dios, aparejado está mi corazón: cantaré, y diré salmos.
Moyo wangu umeponywa, Mungu, moyo wangu umeponywa, nitaimba, ndiyo, nitaimba sifa.
8 Despierta, o! gloria mía, despierta salterio y arpa; levantarme he de mañana.
Inuka, moyo wa thamani; inuka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
9 Alabarte he en los pueblos, o! Señor, cantaré de ti en las naciones:
Nitakushukuru wewe, Bwana, kati ya watu; Kati ya mataifa nitakuimbia sifa.
10 Porque grande es hasta los cielos tu misericordia, y hasta las nubes tu verdad.
Maana upendo wako usiokwisha, huzifikia mbingu; na uaminifu wako mawinguni.
11 Ensálzate sobre los cielos, o! Dios; sobre toda la tierra se ensalce tu gloria.
Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu; na utukufu wako uinuliwe juu ya nchi yote.

< Salmos 57 >