< Salmos 38 >

1 Jehová, no me reprendas con tu furor, ni me castigues con tu ira.
Yahwe, usinikemee katika hasira yako; usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 Porque tus saetas descendieron en mí; y sobre mí ha descendido tu mano.
Kwa kuwa mishale yako hunichoma, na mkono wako huniangusha chini.
3 No hay sanidad en mi carne a causa de tu ira: no hay paz en mis huesos a causa de mi pecado.
Mwili wangu wote unaumwa kwa sababu ya hasira yako; kwa sababu ya dhambi zangu mifupa yangu haina afya.
4 Porque mis iniquidades han pasado sobre mi cabeza: como carga pesada, se han agravado sobre mí.
Kwa maana maovu yangu yamenielemea; yamekuwa mzigo mzito kwangu.
5 Pudriéronse, y corrompiéronse mis llagas a causa de mi locura.
Vidonda vyangu vimeoza na vinanuka kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
6 Estoy encorvado, estoy humillado en gran manera: todo el día ando enlutado.
Nimepindika na kuwa mnyonge kila siku; ninaenenda katika maombolezo siku zote.
7 Porque mis caderas están llenas de ardor: y no hay sanidad en mi carne.
Kwa maana ndani yangu, ninaungua; hakuna afya katika mwili wangu.
8 Estoy debilitado y molido en gran manera: rugiendo estoy a causa del alboroto de mi corazón.
Nimedhohofika na kulemewa sana; ninaugua kwa sababu ya dhiki yangu.
9 Señor, delante de ti están todos mis deseos: y mi suspiro no te es oculto.
Bwana, wewe unaielewa shauku ya ndani kabisa ya moyo wangu, na kuugua kwangu hakujifichika kwako.
10 Mi corazón está rodeado, me ha dejado mi vigor; y la luz de mis ojos, aun ellos no están conmigo.
Moyo wangu unapwita pwita, nguvu zangu zinaniisha, macho yangu yanafifia.
11 Mis amigos, y mis compañeros, se quitaron de delante de mi plaga: y mis cercanos se pusieron lejos.
Marafiki na ndugu zangu wamenitenga kwa sababu ya hali; majirani zangu hukaa mbali nami.
12 Y los que buscaban a mi alma armaron lazos: y los que buscaban mi mal, hablaban iniquidades: y todo el día meditaban fraudes.
Wale wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego kwa ajili yangu. Wao ambao hutafuta kunidhuru huongea maneno ya uharibifu na husema maneno ya uongo siku nzima.
13 Y yo, como sordo, no oía: y como un mudo, que no abre su boca.
Lakini, niko kama mtu kiziwi na sisikii lolote; niko kama mtu bubu ambaye hasemi lolote.
14 Y fui como un hombre que no oye: y que no hay en su boca reprensiones.
Niko kama mtu asiye sikia na mbaye hawezi kujibu.
15 Porque a ti Jehová esperaba: tú responderás Jehová Dios mío.
Hakika ninakungoja wewe, Yahwe; wewe utanijibu, Bwana Mungu wangu.
16 Porque decía: Que no se alegren de mí: cuando mi pie resbalaba se engrandecían sobre mí.
Ninasema hivi ili kwamba maadui zangu wasije wakafurahia juu yangu. Ikiwa mguu wangu utateleza, watanifanyia mambo mabaya.
17 Porque yo aparejado estoy a cojear: y mi dolor está delante de mí continuamente.
Kwa kuwa niko karibu mashakani, na niko katika maumivu ya mara kwa mara.
18 Por tanto denunciaré mi maldad: congojarme he por mi pecado.
Ninatubu makosa yangu; ninahuzunika kwa dhambi zangu.
19 Porque mis enemigos son vivos y fuertes: y hánse aumentado los que me aborrecen sin causa:
Lakini maadui zangu ni wengi; wale wanichukiao ni wengi.
20 Y pagando mal por bien me son contrarios, por seguir yo lo bueno.
Wao wananilipa mabaya kwa mema; wanavurumiza shutuma kwangu ingawa nimefuata lililo jema.
21 No me desampares, o! Jehová; Dios mío, no te alejes de mí.
Usinitelekeze, Yahwe, Mungu wangu, usikae mbali nami.
22 Apresúrate a ayudarme, Señor, que eres mi salud.
Njoo haraka unisaidie, Bwana, wokovu wangu.

< Salmos 38 >