< Salmos 34 >

1 Bendeciré a Jehová en todo tiempo; siempre será su alabanza en mi boca.
Nitamsifu Yahwe wakati wote, siku zote sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu.
2 En Jehová se alabará mi alma; oirán los mansos, y alegrarse han.
Nitamsifu Yahwe! walio onewa wasikie na kufurahi.
3 Engrandecéd a Jehová, conmigo; y ensalcemos su nombre a una.
Msifuni Yahwe pamoja nami, kwa pamoja tuliinue jina lake.
4 Busqué a Jehová, y él me oyó; y de todos mis miedos me libró.
Nilimuomba Yahwe msaada naye akanijibu, akanipa ushindi juu ya hofu yangu yote.
5 Miraron a él, y fueron alumbrados; y sus rostros no se avergonzaron.
Wale wanao mtazama yeye wana furaha, na nyuso zao hazina aibu.
6 Este pobre llamó, y Jehová le oyó, y de todas sus angustias le escapó.
Huyu mtu aliye onewa alilia na Yahwe akamsikia na kumuokoa kwenye matatizo yake yote.
7 El ángel de Jehová asienta campo en derredor de los que le temen, y los defiende.
Malaika wa Yahwe huweka kambi wakiwazunguka wale wanao muogopa yeye na kuwaokoa.
8 Gustád, y ved que es bueno Jehová; dichoso el varón que confiará en él.
Onjeni muone Yahwe ni mzuri. Amebarikiwa mtu yule ambaye Yahwe ni kimbilio lake.
9 Teméd a Jehová sus santos; porque no hay falta para los que le temen.
Muogopeni Yahwe, ninyi watu watakatifu wake. Hakuna kupungukikwa kwa wale wanao mhofu yeye.
10 Los leoncillos empobrecieron, y tuvieron hambre; y los que buscan a Jehová, no tendrán falta de ningún bien.
Simba wadogo wakati mwingine hukosa chakula na kuteseka kwa njaa, bali wale wamtafutao Yahwe hawatapungukiwa chochote kilicho kizuri.
11 Veníd, hijos, oídme; temor de Jehová os enseñaré.
Njoni, wana, mnisikilize mimi. nitawafundisha ninyi hofu ya Yahwe.
12 ¿Quién es el varón que desea vida, qué codicia días para ver bien?
Mtu nani aliyepo ambaye anatamani maisha na anapenda kuwa na siku nyingi, ili kwamba aweze kuona vizuri?
13 Guarda tu lengua de mal, y tus labios de hablar engaño.
Hivyo uepushe ulimi wako na uovu na uilinde midomo yako kuongea uongo.
14 Apártate del mal, y haz el bien; inquiere la paz, y síguela.
Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani.
15 Los ojos de Jehová están sobre los justos; y sus oídos al clamor de ellos.
Macho ya Yahwe yako kwenye haki na masikio yake huelekea kulia kwao.
16 La ira de Jehová contra los que mal hacen, para cortar de la tierra la memoria de ellos.
Uso wa Yahwe uko kinyume na wale watendao uovu, kuikatilia mbali kumbukumbu yao duniani.
17 Clamaron, y Jehová los oyó: y de todas sus angustias los escapó.
Wenye haki hulia na Yahwe husikia na kuwaokoa kwenye matatizo yao yote.
18 Cercano está Jehová a los quebrantados de corazón: y a los molidos de espíritu salvará.
Yahwe yu karibu nao waliovunjika moyo, naye huwaokoa waliogandamizwa rohoni.
19 Muchos son los males del justo: y de todos ellos le escapará Jehová.
Mateso ya wenye haki ni mengi, bali Yahwe huwaokoa nayo yote.
20 Guardando todos sus huesos; uno de ellos no será quebrantado.
Yeye huitunza mifupa yake yote, hakuna hata mmoja wao utavunjika.
21 Matará al malo la maldad; y los que aborrecen al justo serán asolados.
Uovu utawauwa waovu. Wale wachukiao haki watahukumiwa.
22 Redime Jehová la vida de sus siervos; y no serán asolados todos los que en él confían.
Yahwe huokoa maisha ya watumishi wake. Hakuna atakaye hukumiwa hata mmoja atafutaye usalama katika yeye.

< Salmos 34 >