< Salmos 30 >

1 Ensalzarte he, o! Jehová, porque me has ensalzado: y no hiciste alegrar a mis enemigos de mí.
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2 Jehová, Dios mío, clamé a ti, y me sanaste.
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3 Jehová, hiciste subir del sepulcro mi alma: dísteme vida de mi descendimiento a la sepultura. (Sheol h7585)
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol h7585)
4 Cantád a Jehová sus misericordiosos: y celebrad la memoria de su santidad.
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
5 Porque un momento hay en su furor, mas vida en su voluntad: a la tarde reposará el lloro, y a la mañana vendrá la alegría.
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
6 Y yo dije en mi quietud: No resbalaré jamás.
Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7 Porque tú, Jehová, por tu benevolencia asentaste mi monte con fortaleza: mas escondiste tu rostro, y yo fui conturbado.
Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
8 A ti, o! Jehová, llamaré: y al Señor suplicaré.
Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
9 ¿Qué provecho hay en mi muerte, cuando yo descendiere al hoyo? ¿Loarte ha el polvo? ¿anunciará tu verdad?
“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
10 Oye, o! Jehová, y ten misericordia de mí: Jehová, sé mi ayudador.
Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
11 Tú tornaste mi endecha en baile: desataste mi saco, y ceñísteme de alegría.
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
12 Por tanto a ti canté gloria, y no callé: Jehová Dios mío, para siempre te alabaré.
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.

< Salmos 30 >