< Salmos 135 >

1 Alabád el nombre de Jehová, alabád siervos de Jehová.
Msifuni Bwana. Lisifuni jina la Bwana, msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 Los que estáis en la casa de Jehová, en los patios de la casa de nuestros Dios.
ninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 Alabád a Jehová, porque es bueno Jehová: cantád salmos a su nombre, porque es suave.
Msifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema, liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 Porque Jehová ha escogido a Jacob para sí, a Israel por su posesión.
Kwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe, Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 Porque yo sé que Jehová es grande, y el Señor nuestro mayor que todos los dioses.
Ninajua ya kuwa Bwana ni mkuu, kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 Todo lo que quiso Jehová, hizo en los cielos y en la tierra, en las mares, y en todos los abismos.
Bwana hufanya lolote apendalo, mbinguni na duniani, katika bahari na vilindi vyake vyote.
7 El que hace subir las nubes del cabo de la tierra: hizo los relámpagos para la lluvia; el que saca los vientos de sus tesoros.
Hufanya mawingu kupanda kutoka miisho ya dunia; hupeleka umeme wa radi pamoja na mvua na huleta upepo kutoka ghala zake.
8 El que hirió a los primogénitos de Egipto desde el hombre hasta la bestia.
Alimuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, mzaliwa wa kwanza wa wanadamu na wanyama.
9 Envió señales y prodigios en medio de ti, o! Egipto: en Faraón, y en todos sus siervos.
Alipeleka ishara zake na maajabu katikati yako, ee Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 El que hirió a muchas naciones; y mató a reyes poderosos:
Aliyapiga mataifa mengi, na akaua wafalme wenye nguvu:
11 A Sejón rey Amorreo, y a Og rey de Basán, y a todos los reinos de Canaán.
Mfalme Sihoni na Waamori, Ogu mfalme wa Bashani na wafalme wote wa Kanaani:
12 Y dio la tierra de ellos en heredad: en heredad a Israel su pueblo.
akatoa nchi yao kuwa urithi, urithi kwa watu wake Israeli.
13 Jehová, tu nombre es eterno: Jehová, tu memoria para generación y generación.
Ee Bwana, jina lako ladumu milele, kumbukumbu za fahari zako, Ee Bwana, kwa vizazi vyote.
14 Porque Jehová juzgará a su pueblo; y sobre sus siervos se arrepentirá.
Maana Bwana atawathibitisha watu wake, na kuwahurumia watumishi wake.
15 Los ídolos de los Gentiles son plata y oro: obra de manos de hombre.
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, zilizotengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
16 Tienen boca, y no hablan: tienen ojos y no ven.
Zina vinywa, lakini haziwezi kusema, zina macho, lakini haziwezi kuona;
17 Tienen orejas y no escuchan; tampoco hay espíritu en sus bocas.
zina masikio, lakini haziwezi kusikia, wala hakuna pumzi katika vinywa vyao.
18 Como ellos sean los que los hacen; y todos los que en ellos confían.
Wale wanaozitengeneza watafanana nazo, vivyo hivyo wale wote wanaozitumainia.
19 Casa de Israel bendecíd a Jehová: Casa de Aarón bendecíd a Jehová:
Ee nyumba ya Israeli, msifuni Bwana; ee nyumba ya Aroni, msifuni Bwana;
20 Casa de Leví bendecíd a Jehová: los que teméis a Jehová, bendecíd a Jehová.
ee nyumba ya Lawi, msifuni Bwana; ninyi mnaomcha, msifuni Bwana.
21 Bendito Jehová de Sión, el que mora en Jerusalem. Alelu- Jah.
Msifuni Bwana kutoka Sayuni, msifuni yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Bwana.

< Salmos 135 >