< Salmos 132 >

1 Acuérdate, o! Jehová, de David, de toda su aflicción:
Wimbo wa kwenda juu. Ee Bwana, mkumbuke Daudi na taabu zote alizozistahimili.
2 Que juró a Jehová, prometió al fuerte de Jacob:
Aliapa kiapo kwa Bwana na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo:
3 No entraré en la morada de mi casa: no subiré sobre el lecho de mi estrado:
“Sitaingia nyumbani mwangu au kwenda kitandani mwangu:
4 No daré sueño a mis ojos, ni a mis párpados adormecimiento,
sitaruhusu usingizi katika macho yangu, wala kope zangu kusinzia,
5 Hasta que halle lugar para Jehová, moradas para el fuerte de Jacob.
mpaka nitakapompatia Bwana mahali, makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.”
6 He aquí, en Efrata oímos de ella: hallámosla en los campos del bosque.
Tulisikia habari hii huko Efrathi, tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara:
7 Entraremos en sus tiendas: encorvarnos hemos al estrado de sus pies.
“Twendeni kwenye makao yake, na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake;
8 Levántate, o! Jehová, a tu reposo, tú, y el arca de tu fortaleza.
inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, wewe na Sanduku la nguvu zako.
9 Tus sacerdotes vistan justicia; y tus piadosos se regocijen.
Makuhani wako na wavikwe haki, watakatifu wako na waimbe kwa furaha.”
10 Por amor de David tu siervo no vuelvas de tu ungido el rostro.
Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, usimkatae mpakwa mafuta wako.
11 Juró Jehová verdad a David, no se apartará de ella: de fruto de tu vientre pondré sobre tu trono.
Bwana alimwapia Daudi kiapo, kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe katika kiti chako cha enzi,
12 Si tus hijos guardaren mi alianza, y mi testimonio que yo les enseñaré: sus hijos también se asentarán sobre tu trono para siempre.
kama wanao watashika Agano langu na sheria ninazowafundisha, ndipo wana wao watarithi kiti chako cha enzi milele na milele.”
13 Porque Jehová ha elegido a Sión: la codició por habitación para sí.
Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, amepaonea shauku pawe maskani yake:
14 Este será mi reposo para siempre: aquí habitaré, porque la he codiciado.
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku:
15 A su mantenimiento daré bendición: sus pobres hartaré de pan.
Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: nitashibisha maskini wake kwa chakula.
16 Y a sus sacerdotes vestiré de salud; y sus piadosos exultarán de gozo.
Nitawavika makuhani wake wokovu, nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha.
17 Allí haré reverdecer el cuerno de David: yo he aparejado lámpara a mi ungido.
“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, na kuweka taa kwa ajili ya masiya wangu.
18 A sus enemigos vestiré de confusión; y sobre él florecerá su corona.
Adui zake nitawavika aibu, bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”

< Salmos 132 >