< Salmos 129 >

1 Mucho me han angustiado desde mi juventud, díga lo ahora Israel;
“Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia,” Israeli na iseme.
2 Mucho me han angustiado desde mi juventud: mas no prevalecieron contra mí.
“Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia, lakini hawajanishinda.
3 Sobre mis espaldas araron gañanes: hicieron luengos surcos:
Wakulima wamekuwa wakilima mgonngoni kwangu; wametengeneza matuta yao marefu.
4 Mas Jehová justo, cortó las coyundas de los impíos.
Yahwe ni mwenye haki; amezikata kamba za waovu.”
5 Serán avergonzados, y vueltos atrás, todos los que aborrecen a Sión.
Wote waaibishwe na kurudishwa nyuma, wale wachukiao Sayuni.
6 Serán como la yerba de los tejados: que antes que salga, se seca;
Na wawe kama nyasi juu ya paa ambayo hunyauka kabla hayajakua,
7 De la cual no hinchió su mano segador; ni su brazo el que hace gavillas.
ambayo hayawezi kujaza mkono wa mvunaji wala kifua cha mfunga miganda.
8 Ni dijeron los que pasaron: Bendición de Jehová sea sobre vosotros: os bendecimos en nombre de Jehová.
Wale wapitao karibu wasiseme, “Baraka za Mungu na ziwe juu yako; Tunakubariki katika jina la Yahwe.”

< Salmos 129 >