< Salmos 120 >

1 A Jehová llamé estando en angustia; y él me respondió.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 Jehová, escapa mi alma del labio mentiroso: de la lengua engañosa.
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 ¿Qué te dará a ti, o qué te añadirá la lengua engañosa?
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 Es como saetas de valiente agudas con brasas de enebros.
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 ¡Ay de mí que peregrino en Mesec: habito con las tiendas de Cedar!
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 Mucho se detiene mi alma con los que aborrecen la paz.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 Yo soy pacífico; y cuando hablo, ellos guerrean.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.

< Salmos 120 >