< Salmos 116 >

1 Amé a Jehová, porque ha oído mi voz: mis ruegos.
Nampenda Yahwe kwa kuwa anasikia sauti yangu na kuomba kwangu kwa ajili ya huruma.
2 Porque ha inclinado su oído a mí; y en mis días le llamaré,
Kwa sababu alinisikiliza, nitamuita yeye ningali ninaishi.
3 Rodeáronme los dolores de la muerte, las angustias del sepulcro me hallaron: angustia y dolor había hallado: (Sheol h7585)
Kamba za mauti zilinizunguka, na mitego ya kuzimu ilinikabili; niliona dhiki na huzuni. (Sheol h7585)
4 Y llamé el nombre de Jehová: Escapa ahora mi alma, o! Jehová.
Kisha niliita kwa jina la Yahwe: “Tafadhali Yahwe, uiokoe nafsi yangu.”
5 Clemente es Jehová y justo, y misericordioso nuestro Dios.
Yahwe ni mwenye neema na haki; Mungu wetu ni mwenye huruma.
6 Guarda a los sencillos Jehová: yo estaba debilitado y salvóme.
Yahwe huwalinda wasio na hila; nilishushwa chini akaniokoa.
7 Vuelve, o! alma mía, a tu reposo; porque Jehová te ha hecho bien.
Nafsi yangu inaweza kurudi mahali pake pa kupumzika, kwa kuwa Yahwe amekuwa mwema kwangu.
8 Porque has librado mi alma de la muerte, mis ojos de las lágrimas, mis pies del rempujón.
Kwa maana uliokoa uhai wangu dhidi ya kifo, mcho yangu dhidi ya machozi, na miguu yangu dhidi ya kujikwaa.
9 Andaré delante de Jehová en las tierras de los vivos.
Nitamtumikia Yahwe katika nchi ya walio hai.
10 Creí, por tanto hablé: y fui afligido en gran manera.
Nilimwamini yeye, hata niliposema, “nimeteswa sana.”
11 Y dije en mi apresuramiento: Todo hombre es mentiroso.
Kwa haraka nilisema, “Watu wote ni waongo.”
12 ¿Qué pagaré a Jehová por todos sus beneficios sobre mí?
Nimlipeje Yahwe kwa wema wake wote kwangu?
13 El vaso de saludes tomaré; e invocaré el nombre de Jehová.
Nitakiinua kikombe cha wokovu, na kuliitia jina la Yahwe.
14 Ahora pagaré mis votos a Jehová delante de todo su pueblo.
Nitatimiza viapo vyangu kwa Yahwe katika uwepo wa watu wake wote.
15 Estimada es en los ojos de Jehová la muerte de sus piadosos.
Mauti ya wacha Mungu ina thamani machoni pa Mungu.
16 Así es, o! Jehová; porque yo soy tu siervo, yo soy tu siervo, hijo de tu sierva, tú rompiste mis prisiones.
Ee Yahwe, hakika, mimi ni mtumishi wako; mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umefungua vifungo vyangu.
17 A ti sacrificaré sacrificio de alabanza; y el nombre de Jehová invocaré.
Nitakutolea dhabihu ya shukrani na nitaliitia jina la Yahwe.
18 Ahora pagaré mis votos a Jehová delante de todo su pueblo;
Nitatimiza viapo vyangu kwa Yahwe katika uwepo wa watu wake wote,
19 En los patios de la casa de Jehová; en medio de ti, o! Jerusalem. Alelu- Jah.
katika nyua za nyumba ya Yahwe, katikati yako, Yerusalemu. Msifuni Yahwe.

< Salmos 116 >