< Salmos 109 >

1 ¡O Dios de mi alabanza! no calles:
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, ambaye ninakusifu, usiwe kimya,
2 Porque boca de impío, y boca de engañador se han abierto sobre mí: han hablado de mí con lengua mentirosa.
kwa maana watu waovu na wadanganyifu wamefungua vinywa vyao dhidi yangu; wasema dhidi yangu kwa ndimi za udanganyifu.
3 Y con palabras de odio me rodearon; y pelearon contra mí sin causa.
Wamenizunguka kwa maneno ya chuki, wananishambulia bila sababu.
4 En pago de mi amor me han sido adversarios; y yo, hacía oración.
Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki, lakini mimi ninawaombea.
5 Y pusieron contra mí mal por bien; y odio por mi amor.
Wananilipiza mabaya kwa mema, chuki badala ya urafiki wangu.
6 Pon sobre él al impío, y Satanás esté a su diestra.
Agiza mtu mwovu ampinge, mshtaki asimame mkono wake wa kuume.
7 Cuando fuere juzgado, salga por impío, y su oración sea para pecado.
Anapohukumiwa, apatikane na hatia, nayo maombi yake yamhukumu.
8 Sean sus días pocos: tome otro su oficio.
Siku zake za kuishi na ziwe chache, nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine.
9 Sean sus hijos huérfanos; y su mujer viuda.
Watoto wake na waachwe yatima, mke wake na awe mjane.
10 Y anden sus hijos vagabundos, y mendiguen; y procuren de sus desiertos.
Watoto wake na watangetange wakiomba, na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.
11 Enrede el acreedor todo lo que tiene; y extraños saqueen su trabajo.
Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo, matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.
12 No tenga quien le haga misericordia; ni haya quien tenga compasión de sus huérfanos.
Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema wala wa kuwahurumia yatima wake.
13 Su posteridad sea talada: en segunda generación sea raído su nombre.
Uzao wake na ukatiliwe mbali, majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.
14 Venga en memoria cerca de Jehová la maldad de sus padres; y el pecado de su madre no sea raído.
Maovu ya baba zake na yakumbukwe mbele za Bwana, dhambi ya mama yake isifutwe kamwe.
15 Estén delante de Jehová siempre; y él corte de la tierra su memoria.
Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana, ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.
16 Por cuanto no se acordó de hacer misericordia; y persiguió al varón afligido, y menesteroso, y quebrantado de corazón, para matarle.
Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema, bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.
17 Y amó la maldición, y vínole; y no quiso la bendición, y ella se alejó de él.
Alipenda kulaani, nayo laana ikampata; hakupenda kubariki, kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.
18 Y vistióse de maldición como de su vestido; y entró como agua en sus entrañas, y como aceite en sus huesos.
Alivaa kulaani kama vazi lake, nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji, kwenye mifupa yake kama mafuta.
19 Séale como vestido con que se cubra; y en lugar de cinto con que siempre se ciña.
Na iwe kama joho alilozungushiwa, kama mshipi aliofungiwa daima.
20 Este sea el salario, de parte de Jehová, de los que me calumnían; y los que hablan mal contra mi alma.
Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu, kwa wale wanaoninenea mabaya.
21 Y tú, Jehová Señor, haz conmigo por causa de tu nombre: escápame, porque tu misericordia es buena.
Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi, unitendee wema kwa ajili ya jina lako, uniokoe kwa wema wa pendo lako.
22 Porque yo soy afligido y necesitado; y mi corazón está herido dentro de mí.
Maana mimi ni maskini na mhitaji, moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23 Como la sombra cuando declina me voy; soy sacudido como langosta.
Ninafifia kama kivuli cha jioni, nimerushwa-rushwa kama nzige.
24 Mis rodillas están enflaquecidas a causa del ayuno; y mi carne está falta de gordura.
Magoti yangu yamelegea kwa kufunga, mwili wangu umedhoofika na kukonda.
25 Yo he sido a ellos oprobio: mirábanme, y meneaban su cabeza.
Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu, wanionapo, hutikisa vichwa vyao.
26 Ayúdame, Jehová Dios mío: sálvame conforme a tu misericordia;
Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie, niokoe sawasawa na upendo wako.
27 Y entiendan que esta es tu mano; que tú, Jehová, has hecho esto.
Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako, kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili.
28 Maldigan ellos, y bendigas tú; levántense, mas sean avergonzados: y tu siervo sea alegrado.
Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki, watakaposhambulia wataaibishwa, lakini mtumishi wako atashangilia.
29 Sean vestidos de vergüenza los que me calumnían; y sean cubiertos como de manto de su confusión.
Washtaki wangu watavikwa fedheha, na kufunikwa na aibu kama joho.
30 Yo alabaré a Jehová en gran manera con mi boca; y en medio de muchos le loaré:
Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana, katika umati mkubwa nitamsifu.
31 Porque él se pondrá a la diestra del pobre; para librar su alma de los que juzgan.
Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji, kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.

< Salmos 109 >