< Salmos 105 >

1 Alabád a Jehová, invocád su nombre: hacéd notorias sus obras en los pueblos.
Mshukuruni Yahwe, liitieni jina lake; myafanye matendo yake yajulikane kati ya mataifa.
2 Cantád a él, decíd salmos a él: hablád de todas sus maravillas.
Mwimbieni yeye, mwimbieni sifa yeye; semeni matendo yake yote ya ajau.
3 Gloriáos en su nombre santo: alégrese el corazón de los que buscan a Jehová.
Mjivune katika utakatifu wa jina lake; moyo wao wamtafutao Yahwe ufurahi.
4 Buscád a Jehová, y a su fortaleza: buscád su rostro siempre.
Mtafuteni Yahwe na nguvu zake; utafuteni uwepo wake siku zote.
5 Acordáos de sus maravillas, que hizo: de sus prodigios, y de los juicios de su boca,
Kumbukeni mambo ya ajabu aliyoyatenda,
6 Simiente de Abraham su siervo: hijos de Jacob sus escogidos.
miujiza yake na amri zitokazo kinywani mwake, enyi kizazi cha Ibrahimu mtumishi wake, enyi watu wa Yakobo, wachaguliwa wake.
7 El es Jehová nuestro Dios: en toda la tierra están sus juicios.
Yeye ni Yahwe, Mungu wetu. Amri zake ziko juu ya nchi yote.
8 Acordóse para siempre de su alianza: de la palabra que mandó para mil generaciones:
Naye hulikumbuka agano lake milele, neno alilo amuru kwa ajili ya vizazi elfu.
9 La cual concertó con Abraham, y de su juramento a Isaac.
Hulikumbuka agano alilolifanya na Ibrahimu na kiapo alicho mwapia Isaka.
10 Y establecióla a Jacob por decreto, a Israel por concierto eterno,
Hiki ndicho alicho mthibitishia Yakobo kama agano na kama agano la milele kwa Israeli.
11 Diciendo: A ti daré la tierra de Canaán, por cordel de vuestra heredad.
Alisema, “Nitakupa wewe ardhi ya Kanaani kama sehemu yako ya urithi.”
12 Siendo ellos pocos hombres en número, y extranjeros en ella.
Alisema hili wakati tu walipokuwa wachache katika hesabu, yaani wachahe sana, nao walikuwa wageni katika nchi.
13 Y anduvieron de gente en gente: de un reino a otro pueblo.
Walienda taifa hadi taifa na kutoka ufalme moja kwenda mwingine.
14 No consintió que hombre los agraviase: y por causa de ellos castigó a los reyes.
Hakuruhusu yeyote kuwaonea; aliwakemea wafalme kwa ajili yao.
15 No toquéis en mis ungidos: ni hagáis mal a mis profetas.
Alisema, “Msiwaguze wapakwa mafuta wangu, na msiwadhuru manabii wangu.”
16 Y llamó a la hambre sobre la tierra: y toda fuerza de pan quebrantó.
Aliita njaa katika nchi; akaondoa upatikanaji wa mkate wote.
17 Envió un varón delante de ellos: por siervo fue vendido José.
Akatuma mtu mbele yao; Yusufu aliuzwa kama mtumishi.
18 Afligieron sus pies con grillos: en hierro entró su persona,
Miguu yake ilifungwa kwa pingu; alivishwa mnyororo wa chuma shingoni mwake,
19 Hasta la hora que llegó su palabra: el dicho de Jehová le purificó.
mpaka wakati wa maneno yake ulipotimia, nalo neno la Yahwe lilimjaribu.
20 Envió el rey, y soltóle: el señor de los pueblos, y le desató.
Mfalme alituma watumishi kumfungua; mtawala wa watu alimuweka huru.
21 Púsole por señor de su casa: y por enseñoreador en toda su posesión.
Alimuweka kuwa msimamizi wa nyumba yake kama mtawala wa mali zake zote
22 Para echar presos sus príncipes, como él quisiese; y enseñó sabiduría a sus viejos.
kuwaelekeza wakuu kama alivyopenda na kuwafundisha viongozi wake hekima.
23 Y entró Israel en Egipto: y Jacob fue extranjero en la tierra de Cam.
Kisha Israeli iliingia Misri, na Yakobo aliishi kwa muda katika nchi ya Hamu.
24 E hizo crecer su pueblo en gran manera: e hízole fuerte más que sus enemigos.
Yahwe aliwajalia watu wake wazae sana, na aliwafanya wenye nguvu kuliko adui zao.
25 Volvió el corazón de ellos, para que aborreciesen a su pueblo: para que pensasen mal contra sus siervos.
Alisababisha adui zao wawachukie watu wake, na kuwatendea visivyo watumishi wake.
26 Envió a su siervo Moisés: a Aarón, al cual escogió.
Alimtuma Musa, mtumishi wake, na Haruni, ambaye alikwisha mchagua.
27 Pusieron en ellos las palabras de sus señales, y sus prodigios en la tierra de Cam.
Walifanya ishara zake kati ya Wamisri na maajabu yake katika ya nchi ya Hamu.
28 Echó tinieblas, e hizo oscuridad, y no fueron rebeldes a su palabra.
Alituma giza na likaifanya nchi hiyo kuwa giza, lakini watu wake hawakutii amri zake.
29 Volvió sus aguas en sangre, y mató sus pescados.
Aligeuza maji kuwa damu na aliua samaki wao.
30 Engendró ranas su tierra en las camas de sus reyes.
Nchi yao ilijaa vyura, hata katika vyumba vya watawala wao.
31 Dijo, y vino una mezcla de diversas moscas, piojos en todo su término.
Alisema, na makundi ya inzi na chawa wakaja mjini mwote.
32 Volvió sus lluvias en granizo: en fuego de llamas en su tierra.
Aliigeuza mvua yao kuwa mvua ya mawe, pamoja na miali ya moto juu ya ardhi yao.
33 E hirió sus viñas, y sus higueras; y quebró los árboles de su término.
Aliiharibu mizabibu yao na mitini yao; akaivunja miti ya mji wao.
34 Dijo, y vino langosta, y pulgón sin número;
Alisema, na nzige wakaja, nzige wengi sana.
35 Y comió toda la yerba de su tierra, y comió el fruto de su tierra.
Nzige walikula mboga zao zote za majani katika nchi yao. Walikula mazao yote ardhini.
36 E hirió a todos los primogénitos en su tierra, el principio de toda su fuerza.
Aliua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao, malimbuko ya nguvu zao.
37 Y sacólos con plata y oro; y no hubo en sus tribus enfermo.
Aliwatoa nje Waisraeli wakiwa na fedha na dhahabu; hakuna mmoja wa kabila lake aliyejikwaa njiani.
38 Egipto se alegró en su salida; porque había caído sobre ellos el terror de ellos.
Misri ilifurahi walipoondoka, maana Wamisri waliwaogopa.
39 Extendió una nube por cubierta, y fuego para alumbrar la noche.
Alitandaza wingu liwafunike na alifanya moto uwaangazie wakati wa usiku.
40 Pidieron, e hizo venir codornices; y de pan del cielo les hartó.
Waisraeli waliomba chakula, naye aliwaletea kware na aliwatosheleza kwa mkate kutoka mbiguni.
41 Abrió la peña, y corrieron aguas; fueron por las securas como un río.
Aliugawa mwamba, maji yalimwagika kutoka humo; yalitiririka katika jangwa kama mto.
42 Porque se acordó de su santa palabra con Abraham su siervo.
Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu aliyoifanya kwa Ibrahimu mtumishi wake.
43 Y sacó a su pueblo con gozo; con júbilo a sus escogidos.
Aliwaongoza watu wake kwa furaha, wateule wake kwa kelele za ushindi.
44 Y dióles las tierras de los Gentiles: y los trabajos de las naciones heredaron:
Aliwapa nchi za mataifa; walichukua milki ya mali za watu
45 Para que guardasen sus estatutos; y conservasen sus leyes. Alelu- Jah.
ili waweze kushika amri zake na kutii sheria zake. Msifuni Yahwe.

< Salmos 105 >