< Salmos 104 >

1 Bendice, alma mía, a Jehová; Jehová Dios mío, mucho te has engrandecido, de gloria y de hermosura te has vestido.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 Que se cubre de luz como de vestidura, que extiende los cielos como una cortina;
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 Que entabla con las aguas sus doblados, el que pone a las nubes por su carro, el que anda sobre las alas del viento.
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 El que hace a sus ángeles espíritus, sus ministros al fuego flameante.
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 El fundó la tierra sobre sus basas, no se moverá por ningún siglo.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 Con el abismo, como con vestido, la cubriste: sobre los montes estaban las aguas.
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 De tu reprensión huyeron; por el sonido de tu trueno se apresuraron.
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 Subieron los montes, descendieron los valles a este lugar, que tú les fundaste.
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 Pusíste les término, el cual no traspasarán, ni volverán a cubrir la tierra.
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 El que envía las fuentes en los arroyos; entre los montes van.
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 Abrévanse todas las bestias del campo; los asnos salvajes quebrantan su sed.
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 Junto a ellos habitan las aves de los cielos; entre las hojas dan voces.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 El que riega los montes desde sus doblados; del fruto de tus obras se harta la tierra.
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 El que hace producir el heno para las bestias; y la yerba para servicio del hombre, sacando el pan de la tierra,
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 Y el vino que alegra el corazón del hombre; haciendo relumbrar la faz con el aceite; y el pan sustenta el corazón del hombre.
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 Hártanse los árboles de Jehová; los cedros del Líbano que él plantó:
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 Para que aniden allí las aves; la cigüeña tenga su casa en las hayas.
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 Los montes altos para las cabras monteses, las peñas madrigueras para los conejos.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 Hizo la luna para sazones: el sol conoció su occidente.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 Pones las tinieblas, y la noche es; en ella corren todas las bestias del monte.
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 Los leoncillos braman a la presa, y para buscar de Dios su comida.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 Sale el sol, recógense, y échanse en sus cuevas.
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 Sale el hombre a su hacienda, y a su labranza hasta la tarde.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 ¡Cuán muchas son tus obras, o! Jehová! todas ellas hiciste con sabiduría: la tierra está llena de tu posesión.
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 Esta gran mar y ancha de términos; allí hay pescados sin número, bestias pequeñas y grandes.
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 Allí andan navíos, este leviatán que hiciste para que jugase en ella.
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 Todas ellas esperan a ti, para que les des su comida a su tiempo.
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 Dásles, recogen: abres tu mano, hártanse de bien.
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 Escondes tu rostro, túrbanse: les quitas el espíritu, dejan de ser, y tórnanse en su polvo.
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 Envías tu espíritu, críanse: y renuevas la haz de la tierra.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 Sea la gloria a Jehová para siempre: alégrese Jehová en sus obras.
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 El que mira a la tierra, y tiembla: toca en los montes, y humean.
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 A Jehová cantaré en mi vida: a mi Dios diré salmos mientras viviere.
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 Serme ha suave hablar de él: yo me alegraré en Jehová.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 Sean consumidos de la tierra los pecadores: y los impíos dejen de ser. Bendice alma mía a Jehová. Alelu- Jah.
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.

< Salmos 104 >