< Proverbios 7 >

1 Hijo mío, guarda mis razones, y encierra contigo mis mandamientos.
Mwanangu, yatunze maneno yangu na ndani yako udhihifadhi amri zangu.
2 Guarda mis mandamientos, y vivirás; y mi ley como las niñas de tus ojos.
Uzilinde amri zangu ili uishi na uyatunzetu mafundisho yangu kama mboni ya jicho.
3 Lígalos a tus dedos: escríbelos en la tabla de tu corazón.
Uyafunge katika vidole vyako; uyaandike katika kibao cha moyo wako.
4 Di a la sabiduría: Tú eres mi hermana; y a la inteligencia llama parienta:
Mwambie hekima, “wewe ni dada yangu,” na ufahamu mwite jamaa yako,
5 Para que te guarden de la mujer ajena, y de la extraña, que ablanda sus palabras.
ili ujitunze mwenyewe dhidi ya mwanake haramu, dhidi ya mwanamke mgeni mwenye maneno laini.
6 Porque mirando yo por la ventana de mi casa, por mi ventana,
Nilikuwa naangalia kwenye wavu wa dirisha la nyumba yangu.
7 Miré entre los simples, consideré entre los mancebos un mancebo falto de entendimiento,
Nikawatazama watu mwenye ukosefu wa uzoefu, na miongoni mwa watu vijana nikamwona kijana asiye na akili.
8 El cual pasaba por la calle, junto a su esquina; e iba camino de su casa,
Kijana huyo alishuka mtaani kwenye kona karibu na yule mwanamke, akaenda kwenye nyumba yake.
9 A la tarde del día, ya que oscurecía, en la oscuridad y tiniebla de la noche:
Ilikuwa katika utusiutusi wa siku muda wa jioni, wakati wa usiku na giza.
10 Y veis aquí una mujer, que le sale al encuentro con atavío de ramera, astuta de corazón,
Akakutana na yule mwanake, amevaa kama kahaba, katika moyo wa udanyanyifu.
11 Alborotadora y rencillosa: sus pies no pueden estar en casa:
Alikuwa na kelele na upotovu; miguu yake haikutulia kwenye masikani.
12 Ahora de fuera, ahora por las plazas: asechando por todas las encrucijadas.
Alielekea mitaani, kisha sehemu ya sokoni, na katika kila upande alisubiri kwa kuviza.
13 Y traba de él, y bésale; desvergonzó su rostro; y díjole:
Basi akamshika na kumbusu, kwa uso wa nguvu akamwambia,
14 Sacrificios de paz he prometido, hoy he pagado mis votos:
leo nimetoa sadaka yangu ya amani, nimelipa nadhili yangu,
15 Por tanto he salido a encontrarte, buscando diligentemente tu faz; y héte hallado.
hivyo nilikuja kukutana nawe, kuutafuta uso wako kwa hamu, na sasa nimekupata.
16 Con paramentos he emparamentado mi cama, alzados con cuerdas de Egipto.
Nimeweka matandiko juu ya kitanda changu, kitani za rangi kutoka Misri.
17 He sahumado mi cámara con mirra, áloes, y canela.
Kitanda changu nimenyunyizia manemane, udi na mdalasini.
18 Ven, embriaguémosnos de amores hasta la mañana: alegrémosnos en amores.
Njoo, tunywe tujishibishe kwa upendo wetu hata asubuhi; tupate furaha kuu kwa matendo ya mahaba.
19 Porque el marido no está en su casa, ha ido a un viaje muy largo:
Maana mume wangu hayupo nyumbani kwake; amekwenda safari ya mbali.
20 El saco del dinero llevó en su mano, el día de la fiesta volverá a su casa.
Alichukua mkoba wa fedha; atarudi siku ya mwezi mpevu.
21 Derribóle con la multitud de la suavidad de sus palabras: con la blandura de sus labios le compelió.
katika maneno yake mengi akamshinda; na kwa midomo yake laini anampotosha.
22 Váse en pos de ella luego, como va el buey al degolladero, y como el insensato a las prisiones para ser castigado:
Ghafula alimfuata kama maksai anayekwenda kwa mchinjaji, kama ayala aliyekamatwa kwa nguvu,
23 De tal manera que la saeta traspasó su hígado: como el ave que se apresura al lazo, y no sabe que es contra su vida.
mpaka mshale upasue ini lake. Alikuwa kama ndege anayekimbili kwenye mtego. Hakujua kuwa itamgharimu maisha yake.
24 Ahora pues hijos, oídme, y estád atentos a las razones de mi boca.
Na sasa, wanangu, nisikilizeni; zingatieni maneno ya kinywa changu.
25 No se aparte a sus caminos tu corazón; y no yerres en sus veredas.
Moyo wako usiyageukie mapito yake; usipotoshwe katika mapito yake.
26 Porque a muchos ha hecho caer muertos; y todos los fuertes han sido muertos por ella.
Amesababisha watu wengi kuanguka kwa kuwajeruhi; ameua watu wengi.
27 Caminos del sepulcro son su casa, que descienden a las cámaras de la muerte. (Sheol h7585)
Nyumba yake ipo juu ya barabara ya kwenda kuzimu; huelekea chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)

< Proverbios 7 >