< Proverbios 27 >

1 No te alabes del día de mañana; porque no sabes que parirá el día.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, maana hujui siku italeta nini.
2 Alábete el extraño, y no tu boca: el ajeno, y no tus labios.
Mtu mwingine akusifu na wala si kinywa chako mwenyewe, mgeni na wala si midomo yako mwenyewe.
3 Pesada es la piedra, y la arena pesa: mas la ira del insensato es más pesada que ambas cosas.
Fikiria uzito wa jiwe na uzito wa mchanga- uchokozi wa mpumbavu ni mzito zaidi kuliko hivyo vyote.
4 Cruel es la ira; e impetuoso el furor: ¿mas quién parará delante de la envidia?
Kuna ukatili wenye ghadhabu kali na mafuriko ya hasira, lakini ni nani anayeweza kusimama mbele ya wivu?
5 Mejor es la reprensión manifiesta, que el amor oculto.
Ni bora karipio la wazi kuliko upendo uliofichwa.
6 Fieles son las heridas del que ama; e importunos los besos del que aborrece.
Mwaminifu ni jeraha zilizosababishwa na rafiki, lakini adui anaweza kukubusu kwa kuomba radhi mno.
7 El alma harta huella el panal de miel: mas al alma hambrienta todo lo amargo es dulce.
Mtu aliyekula na kushiba hulikataa hata sega la asali, bali kwa mtu mwenye njaa, kila kitu kichungu ni kitamu.
8 Cual es el ave que se va de su nido, tal es el hombre que se va de su lugar.
Ndege anayezurura kutoka kwenye kiota chake ni kama mtu anayepotea sehemu ambayo anaishi.
9 El ungüento y el sahumerio alegran el corazón; y el amigo al hombre con el consejo dado de ánimo.
Pafumu na manukato huufanya moyo ufurahi, lakini utamu wa rafiki ni bora kuliko ushauri wake.
10 No dejes a tu amigo, ni al amigo de tu padre: ni entres en casa de tu hermano el día de tu aflicción: mejor es el vecino cercano, que el hermano lejano.
Usimwache rafiki yako na rafiki wa baba yako, na usiende kwenye nyumba ya ndugu yako katika siku ya msiba wako. Ni bora rafiki ambaye yupo karibu kuliko ndugu ambaye yupo mbali.
11 Sé sabio, o! hijo mío, y alegra mi corazón; y tendré que responder al que me deshonrare.
Mwanangu, uwe na busara, moyo wangu ufurahi; kisha nitamjibu yule anayenidhihaki.
12 El avisado ve el mal, y escóndese: mas los simples pasan, y llevan el daño.
Mtu mwenye busara huiona taabu na kujificha mwenyewe, lakini mjinga huendelea mbele na kuteseka kwa ajili ya taabu.
13 Quítale su ropa, porque fió al extraño; y por la extraña, préndale.
vazi kama mwenyewe anaweka pesa kama dhamana kwa deni la mgeni; lichukue kama anaweka dhamana kwa malaya.
14 El que bendice a su amigo a alta voz madrugando de mañana, por maldición se le contará.
Anayempa jirani yake baraka kwa sauti ya juu mapema asubuhi, baraka hiyo itafikiriwa kuwa laana!
15 Gotera continua en tiempo de lluvia, y la mujer rencillosa son semejantes.
Mke mgomvi ni kama siku ya manyunyu ya mvua ya daima;
16 El que la escondió, escondió el viento; porque el aceite en su mano derecha clama.
kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kushika mafuta kwa mkono wako wa kulia.
17 Hierro con hierro se aguza; y el hombre aguza el rostro de su amigo.
Chuma hunoa chuma; kwa njia ile ile; mtu humnoa rafiki yake.
18 El que guarda la higuera, come su fruto: y el que guarda a su señor, será honrado.
Yule anayeutunza mtini atakula matunda yake, na yule mwenye kumlinda bwana wake ataheshimiwa.
19 Como un agua se parece a otra, así el corazón del hombre al otro.
Kama maji yanavyoakisi taswira ya sura ya mtu, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwaksi mtu.
20 El sepulcro y la perdición nunca se hartan: así los ojos de los hombres nunca se hartan. (Sheol h7585)
Kama kuzimu na Uharibifu havitosheki, ndivyo yalivyo macho ya mtu hayawezi kutosheka. (Sheol h7585)
21 El crisol prueba la plata, y la fragua el oro; y al hombre la boca del que le alaba.
Kalibu ni kwa fedha na tanuru ni kwa dhahabu; na mtu hujaribiwa anaposifiwa.
22 Aunque majes al insensato en un mortero entre granos de trigo majados a pisón, no se quitará de él su fatuidad.
Hata kama utamponda mpumbavu kwa mchI- pamoja na nafaka- bado upumbavu wake hautatoka.
23 Considera atentamente el rostro de tus ovejas: pon tu corazón al ganado.
Hakikisha unajua hali ya makundi yako na ujishughulishe juu ya makundi yako,
24 Porque las riquezas no son para siempre; ¿y la corona será para perpetuas generaciones?
maana utajiri haudumu daima. Je taji hudumu kwa vizazi vyote?
25 Saldrá la grama, aparecerá la yerba, y segarse han las yerbas de los montes.
Majani huondoka na ukuaji mpya huonekana na milima ya chakula cha mifugo hukusanywa ndani.
26 Los corderos para tus vestidos, y los cabritos para el precio del campo.
Wanakondoo watakupatia mavazi yako na mbuzi watakupatia gharama ya shamba.
27 Y abundancia de leche de las cabras para tu mantenimiento, y para mantenimiento de tu casa, y para sustento de tus criadas.
Kutakuwa na maziwa ya mbuzi kwa chakula chako- chakula kwa kaya yako- na chakula kwa watumishi wako wasichana.

< Proverbios 27 >