< Proverbios 27 >

1 No te alabes del día de mañana; porque no sabes que parirá el día.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
2 Alábete el extraño, y no tu boca: el ajeno, y no tus labios.
Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
3 Pesada es la piedra, y la arena pesa: mas la ira del insensato es más pesada que ambas cosas.
Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
4 Cruel es la ira; e impetuoso el furor: ¿mas quién parará delante de la envidia?
Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
5 Mejor es la reprensión manifiesta, que el amor oculto.
Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
6 Fieles son las heridas del que ama; e importunos los besos del que aborrece.
Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
7 El alma harta huella el panal de miel: mas al alma hambrienta todo lo amargo es dulce.
Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
8 Cual es el ave que se va de su nido, tal es el hombre que se va de su lugar.
Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
9 El ungüento y el sahumerio alegran el corazón; y el amigo al hombre con el consejo dado de ánimo.
Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
10 No dejes a tu amigo, ni al amigo de tu padre: ni entres en casa de tu hermano el día de tu aflicción: mejor es el vecino cercano, que el hermano lejano.
Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
11 Sé sabio, o! hijo mío, y alegra mi corazón; y tendré que responder al que me deshonrare.
Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
12 El avisado ve el mal, y escóndese: mas los simples pasan, y llevan el daño.
Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
13 Quítale su ropa, porque fió al extraño; y por la extraña, préndale.
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
14 El que bendice a su amigo a alta voz madrugando de mañana, por maldición se le contará.
Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
15 Gotera continua en tiempo de lluvia, y la mujer rencillosa son semejantes.
Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
16 El que la escondió, escondió el viento; porque el aceite en su mano derecha clama.
Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
17 Hierro con hierro se aguza; y el hombre aguza el rostro de su amigo.
Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
18 El que guarda la higuera, come su fruto: y el que guarda a su señor, será honrado.
Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
19 Como un agua se parece a otra, así el corazón del hombre al otro.
Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
20 El sepulcro y la perdición nunca se hartan: así los ojos de los hombres nunca se hartan. (Sheol h7585)
Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol h7585)
21 El crisol prueba la plata, y la fragua el oro; y al hombre la boca del que le alaba.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
22 Aunque majes al insensato en un mortero entre granos de trigo majados a pisón, no se quitará de él su fatuidad.
Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
23 Considera atentamente el rostro de tus ovejas: pon tu corazón al ganado.
Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
24 Porque las riquezas no son para siempre; ¿y la corona será para perpetuas generaciones?
Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
25 Saldrá la grama, aparecerá la yerba, y segarse han las yerbas de los montes.
Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
26 Los corderos para tus vestidos, y los cabritos para el precio del campo.
wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
27 Y abundancia de leche de las cabras para tu mantenimiento, y para mantenimiento de tu casa, y para sustento de tus criadas.
Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.

< Proverbios 27 >