< Proverbios 21 >

1 Como los repartimientos de las aguas así está el corazón del rey en la mano de Jehová: a todo lo que quiere, le inclina.
Moyo wa mfalme uko katika mkono wa Bwana; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo.
2 Todo camino del hombre es recto en su opinión: mas Jehová pesa los corazones.
Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali Bwana huupima moyo.
3 Hacer justicia y juicio es a Jehová más agradable que sacrificio.
Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa Bwana kuliko dhabihu.
4 Altivez de ojos, y grandeza de corazón, y pensamiento de los impíos es pecado.
Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
5 Los pensamientos del solícito ciertamente van a abundancia: mas todo presuroso ciertamente a pobreza.
Mipango ya mwenye bidii huelekeza kwenye faida, kama vile kwa hakika pupa huelekeza kwenye umaskini.
6 Allegar tesoros con lengua de mentira, es vanidad, que será echada con los que buscan la muerte.
Mali iliyopatikana kwa ulimi wa uongo ni mvuke upitao upesi na mtego wa kufisha.
7 La rapiña de los impíos los destruirá: porque no quisieron hacer juicio.
Jeuri ya waovu itawaburuta mbali, kwa kuwa wanakataa kufanya yaliyo sawa.
8 El camino del hombre es torcido y extraño: mas la obra del limpio es recta.
Njia ya mwenye hatia ni ya upotovu, bali tabia ya mtu asiye na hatia ni nyofu.
9 Mejor es vivir en un rincón de casa, que con la mujer rencillosa en casa espaciosa.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
10 El alma del impío desea mal: su prójimo no le parece bien.
Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
11 Cuando el burlador es castigado, el simple se hace sabio; y enseñando al sabio, toma sabiduría.
Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
12 Considera el justo la casa del impío: que los impíos son trastornados por el mal.
Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
13 El que cierra su oído al clamor del pobre, también él clamará y no será oído.
Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
14 El presente en secreto amansa el furor, y el don en el seno la fuerte ira.
Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
15 Alegría es al justo hacer juicio: mas quebrantamiento a los que hacen iniquidad.
Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
16 El hombre que yerra del camino de la sabiduría, en la compañía de los muertos reposará.
Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
17 Hombre necesitado será el que ama la alegría; y el que ama el vino y el ungüento no enriquecerá.
Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
18 El rescate del justo será el impío; y por los rectos será castigado el prevaricador.
Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
19 Mejor es morar en tierra del desierto, que con la mujer rencillosa, e iracunda.
Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
20 Tesoro de codicia, y aceite está en la casa del sabio: mas el hombre insensato lo disipará.
Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
21 El que sigue la justicia y la misericordia, hallará la vida, la justicia, y la honra.
Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
22 La ciudad de los fuertes tomó el sabio; y derribó la fuerza de su confianza.
Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
23 El que guarda su boca, y su lengua, su alma guarda de angustias.
Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
24 Soberbio, arrogante, burlador, es el nombre del que hace con saña de soberbia.
Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
25 El deseo del perezoso le mata; porque sus manos no quieren hacer.
Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
26 Todo el tiempo desea: mas el justo da; y no perdona.
Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
27 El sacrificio de los impíos es abominación, ¿cuánto más ofreciéndole con maldad?
Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
28 El testigo mentiroso perecerá: mas el hombre que oye, permanecerá en su dicho.
Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
29 El hombre impío asegura su rostro: mas el recto ordena sus caminos.
Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
30 No hay sabiduría, ni inteligencia, ni consejo contra Jehová.
Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
31 El caballo se apareja para el día de la batalla: mas de Jehová es el salvar.
Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.

< Proverbios 21 >