< Proverbios 20 >

1 El vino hace burlador: la cerveza, alborotador; y cualquiera que en él errare, no será sabio.
Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
2 Bramido, como de cachorro de león, es el miedo del rey: el que le hace enojar, peca contra su alma.
Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
3 Honra es del hombre dejarse de pleito: mas todo insensato se envolverá en él.
Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
4 El perezoso no ara a causa del invierno: mas él pedirá en la segada, y no hallará.
Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
5 Aguas profundas es el consejo en el corazón del hombre: mas el hombre entendido le alcanzará.
Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
6 Muchos hombres pregonan cada cual el bien que han hecho: mas hombre de verdad ¿quién le hallará?
Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
7 El justo que camina en su integridad, bienaventurados serán sus hijos después de él.
Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
8 El rey que está en el trono de juicio, con su mirar disipa todo mal.
Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
9 ¿Quién podrá decir: Yo he limpiado mi corazón, limpio estoy de mi pecado?
Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
10 Doblada pesa, y doblada medida, abominación son a Jehová ambas cosas.
Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
11 El muchacho aun es conocido por sus obras, si su obra es limpia y recta.
Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
12 El oído oye, y el ojo ve: Jehová hizo aun ambas cosas.
Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
13 No ames el sueño, porque no te empobrezcas: abre tus ojos, hartarte has de pan.
Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
14 El que compra, dice: Malo es, malo es: mas en apartándose, él se alaba.
“Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
15 Hay oro, y multitud de piedras preciosas: mas los labios sabios son vaso precioso.
Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
16 Quítale su ropa, porque fió al extraño; y préndale por la extraña.
Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
17 Sabroso es al hombre el pan de mentira: mas después, su boca será llena de cascajo.
Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
18 Los pensamientos con el consejo se ordenan; y con industria se hace la guerra.
Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
19 El que descubre el secreto, anda en chismes; y con el que lisonjea de sus labios, no te entremetas.
Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
20 El que maldice a su padre, o a su madre, su candela será apagada en oscuridad tenebrosa.
Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
21 La herencia adquirida de priesa en el principio, su postrimería aun no será bendita.
Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
22 No digas: Yo me vengaré: espera a Jehová, y él te salvará.
Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
23 Abominación son a Jehová las pesas dobladas; y el peso falso, no es bueno.
Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
24 De Jehová son los pasos del hombre: el hombre pues, ¿cómo entenderá su camino?
Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
25 Lazo es al hombre tragar santidad; y después de los votos andar preguntando.
Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
26 El rey sabio esparce los impíos; y sobre ellos hace tornar la rueda.
Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
27 Candela de Jehová es el alma del hombre, que escudriña lo secreto del vientre.
Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
28 Misericordia y verdad guardan al rey; y con clemencia sustenta su trono.
Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
29 La honra de los mancebos es su fortaleza; y la hermosura de los viejos, su vejez.
Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
30 Las señales de las heridas son medicina en el malo; y las plagas en lo secreto del vientre.
Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.

< Proverbios 20 >