< Proverbios 20 >

1 El vino hace burlador: la cerveza, alborotador; y cualquiera que en él errare, no será sabio.
Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi; yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.
2 Bramido, como de cachorro de león, es el miedo del rey: el que le hace enojar, peca contra su alma.
Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.
3 Honra es del hombre dejarse de pleito: mas todo insensato se envolverá en él.
Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.
4 El perezoso no ara a causa del invierno: mas él pedirá en la segada, y no hallará.
Mvivu halimi kwa majira; kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama lakini hapati chochote.
5 Aguas profundas es el consejo en el corazón del hombre: mas el hombre entendido le alcanzará.
Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina, lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.
6 Muchos hombres pregonan cada cual el bien que han hecho: mas hombre de verdad ¿quién le hallará?
Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma, bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?
7 El justo que camina en su integridad, bienaventurados serán sus hijos después de él.
Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama, wamebarikiwa watoto wake baada yake.
8 El rey que está en el trono de juicio, con su mirar disipa todo mal.
Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu, hupepeta ubaya wote kwa macho yake.
9 ¿Quién podrá decir: Yo he limpiado mi corazón, limpio estoy de mi pecado?
Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi; mimi ni safi na sina dhambi?”
10 Doblada pesa, y doblada medida, abominación son a Jehová ambas cosas.
Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti, Bwana huchukia vyote viwili.
11 El muchacho aun es conocido por sus obras, si su obra es limpia y recta.
Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na adili.
12 El oído oye, y el ojo ve: Jehová hizo aun ambas cosas.
Masikio yasikiayo na macho yaonayo, Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.
13 No ames el sueño, porque no te empobrezcas: abre tus ojos, hartarte has de pan.
Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.
14 El que compra, dice: Malo es, malo es: mas en apartándose, él se alaba.
“Haifai, haifai!” asema mnunuzi, kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.
15 Hay oro, y multitud de piedras preciosas: mas los labios sabios son vaso precioso.
Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi, lakini midomo inenayo maarifa ni kito cha thamani kilicho adimu.
16 Quítale su ropa, porque fió al extraño; y préndale por la extraña.
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
17 Sabroso es al hombre el pan de mentira: mas después, su boca será llena de cascajo.
Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu, bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.
18 Los pensamientos con el consejo se ordenan; y con industria se hace la guerra.
Fanya mipango kwa kutafuta mashauri, ukipigana vita, tafuta maelekezo.
19 El que descubre el secreto, anda en chismes; y con el que lisonjea de sus labios, no te entremetas.
Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika, kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.
20 El que maldice a su padre, o a su madre, su candela será apagada en oscuridad tenebrosa.
Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itazimwa katika giza nene.
21 La herencia adquirida de priesa en el principio, su postrimería aun no será bendita.
Urithi upatikanao haraka mwanzoni, hautabarikiwa mwishoni.
22 No digas: Yo me vengaré: espera a Jehová, y él te salvará.
Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!” Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
23 Abominación son a Jehová las pesas dobladas; y el peso falso, no es bueno.
Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu, nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
24 De Jehová son los pasos del hombre: el hombre pues, ¿cómo entenderá su camino?
Hatua za mtu huongozwa na Bwana. Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?
25 Lazo es al hombre tragar santidad; y después de los votos andar preguntando.
Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.
26 El rey sabio esparce los impíos; y sobre ellos hace tornar la rueda.
Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu, hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.
27 Candela de Jehová es el alma del hombre, que escudriña lo secreto del vientre.
Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu, huchunguza utu wake wa ndani.
28 Misericordia y verdad guardan al rey; y con clemencia sustenta su trono.
Upendo na uaminifu humweka mfalme salama, kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.
29 La honra de los mancebos es su fortaleza; y la hermosura de los viejos, su vejez.
Utukufu wa vijana ni nguvu zao, mvi ni fahari ya uzee.
30 Las señales de las heridas son medicina en el malo; y las plagas en lo secreto del vientre.
Mapigo na majeraha huusafisha ubaya, nayo michapo hutakasa utu wa ndani.

< Proverbios 20 >