< Proverbios 17 >

1 Mejor es un bocado de pan seco, y en paz, que la casa de cuestión llena de víctimas.
Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
2 El siervo prudente se enseñoreará del hijo deshonrador; y entre los hermanos partirá la herencia.
Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
3 Afinador a la plata, y fragua al oro: mas Jehová prueba los corazones.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
4 El malo está atento al labio inicuo; y el mentiroso escucha a la lengua maldiciente.
Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
5 El que escarnece al pobre, afrenta a su hacedor; y el que se alegra en la calamidad ajena no será sin castigo.
Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
6 Corona de los viejos son los hijos de los hijos; y la honra de los hijos, sus padres.
Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
7 No conviene al insensato el labio excelente: ¿cuánto menos al príncipe el labio mentiroso?
Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
8 Piedra preciosa es el presente en ojos de sus dueños: a donde quiera que se vuelve, da prosperidad.
Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
9 El que cubre la prevaricación, busca amistad: mas el que reitera la palabra, aparta al príncipe.
Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
10 Aprovecha la reprensión en el entendido, más que cien azotes en el insensato.
Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
11 El rebelde no busca sino mal; y mensajero cruel será enviado contra él.
Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
12 Encuentre con el hombre un oso, que le hayan quitado sus cachorros, y no un insensato en su locura.
Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
13 El que da mal por bien, no se apartará mal de su casa.
Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
14 Soltar las aguas es el principio de la contienda: pues antes que se revuelva el pleito, déjalo.
Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
15 El que justifica al impío, y el que condena al justo, ambos a dos son abominación a Jehová.
Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
16 ¿De qué sirve el precio en la mano del insensato para comprar sabiduría, no teniendo entendimiento?
Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
17 En todo tiempo ama el amigo: mas el hermano para la angustia es nacido.
Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
18 El hombre falto de entendimiento toca la mano, fiando a otro delante de su amigo.
Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
19 La prevaricación ama, el que ama pleito; y el que alza su portada, busca quebrantamiento.
Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
20 El perverso de corazón nunca hallará bien; y el que revuelve con su lengua, caerá en mal.
Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
21 El que engendra al insensato, para su tristeza le engendra; y el padre del insensato no se alegrará.
Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
22 El corazón alegre hará buena disposición: mas el espíritu triste seca los huesos.
Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
23 El impío toma presentes del seno, para pervertir las veredas del derecho.
Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
24 En el rostro del entendido se parece la sabiduría: mas los ojos del insensato, hasta el cabo de la tierra.
Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
25 El hijo insensato es enojo a su padre; y amargura a la que le engendró.
Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
26 Ciertamente condenar al justo, no es bueno: ni herir a los príncipes sobre el derecho.
Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
27 Detiene sus dichos el que sabe sabiduría; y de preciado espíritu es el hombre entendido.
Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
28 Aun el insensato cuando calla, es contado por sabio: el que cierra sus labios es entendido.
Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.

< Proverbios 17 >