< Proverbios 1 >

1 Los proverbios de Salomón, hijo de David, rey de Israel:
Mithali za Sulemani mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.
2 Para entender sabiduría y castigo: para entender las razones prudentes:
Mithali hizi zinafundisha hekima na maarifa, kufundisha maneno ya busara,
3 Para recibir el castigo de prudencia, justicia, y juicio, y equidad:
ili mpate maarifa kwa ajili ya kuishi kwa kutenda wema, haki na adili.
4 Para dar a los simples astucia, y a los mozos inteligencia y consejo.
Mithali hizi zinatoa hekima kwa wale ambao hawakufunzwa, na kuwapa vijana maarifa na hadhari.
5 Oirá el sabio y aumentará la doctrina; y el entendido adquirirá consejo.
Watu wenye busara wasikie na kuongeza elimu yao na watu wenye ufahamu wapate mwongozo,
6 Para entender parábola y declaración, palabras de sabios, y sus dichos oscuros.
kwa kuelewa mithali, misemo, vitendawili na maneno ya wenye busara.
7 El principio de la sabiduría es el temor de Jehová: los insensatos despreciaron la sabiduría y la instrucción.
Hofu ya Yehova ni chanzo cha maarifa- wapumbavu hudharau hekima na nidhamu.
8 Oye, hijo mío, el castigo de tu padre, y no deseches la ley de tu madre:
Mwanangu, sikia fundisho la baba yako na wala usiziache kanuni za mama yako;
9 Porque aumento de gracia serán a tu cabeza, y collares a tu cuello.
zitakuwa kilemba cha neema katika kichwa chako na jebu zinazoning'inia kwenye shingo yako.
10 Hijo mío, si los pecadores te quisieren engañar, no consientas.
Mwanangu wenye dhambi wakikushawishi katika dhambi zao, kataa kuwafuata.
11 Si dijeren: Ven con nosotros, espiemos a la sangre: asechemos al inocente sin razón:
Kama watasema, “haya tufuatae, tuvizie ili kufanya mauaji, tujifiche ili tuwashambulie watu wasio na hatia, pasipo sababu.
12 Tragarlos hemos como el sepulcro, vivos; y enteros, como los que caen en sima: (Sheol h7585)
Haya tuwameza wakiwa hai, kama kuzimu inavyowachukua wenye afya, na kuwa kama wale waangukao kwenye shimoni. (Sheol h7585)
13 Hallaremos riquezas de todas suertes: henchiremos nuestras casas de despojos:
Tutapata vitu vyote vya thamani; tutazijaza nyumba zetu vile tunavyoiba kwa wengine.
14 Echa tu suerte entre nosotros: tengamos todos una bolsa:
Weka vitu vyako kwetu; tutakuwa na mfuko moja kwa pamoja.”
15 Hijo mío, no andes en camino con ellos: aparta tu pie de sus veredas:
Mwanangu, usitembee katika njia moja pamoja nao; usiruhusu mguu wako kugusa katika mapito yao;
16 Porque sus pies correrán al mal; e irán presurosos a derramar sangre.
miguu ya hukimbilia mabaya na huharakisha kumwaga damu.
17 Porque en vano se tenderá la red delante de los ojos de toda ave.
Kwa kuwa haina maana kumtegea ndege mtego wakati ndege anaona.
18 Mas ellos a su sangre espían, y a sus almas asechan.
Watu hawa huvizia kujiua wenyewe—wanatega mtego kwa ajili yao wenyewe.
19 Tales son las sendas de todo codicioso de codicia, la cual prenderá el alma de sus poseedores.
Ndivyo zilivyo njia za kila ambaye hupata utajiri kwa udhalimu; mapato ya udhalimu huondoa uhai wa wenye utajiri.
20 La sabiduría clama de fuera: en las plazas da su voz:
Hekima inalia kwa sauti mtaani, inapaza sauti katika viwanja;
21 En las encrucijadas de los murmullos de gente clama: en las entradas de las puertas de la ciudad dice sus razones:
katika mitaa inalia kwa sauti kuu, kwenye maingilio ya milango ya mji inasema “
22 ¿Hasta cuándo, o! simples, amaréis la simpleza, y los burladores desearán el burlar, y los insensatos aborrecerán la ciencia?
Mpaka lini enyi wajinga mtapenda kuwa wajinga? Mpaka lini enyi wenye dhihaka mtapenda dhihaka, na hadi lini enyi wapumbavu, mtachukia maarifa?
23 Volvéos a mi reprensión: he aquí que yo os derramaré mi espíritu, y os haré saber mis palabras.
Zingatia karipio langu; nitatoa mawazo yangu kwa ajili yenu; nitawafahamisha maneno yangu.
24 Por cuanto llamé, y no quisisteis: extendí mi mano, y no hubo quien escuchase:
Nimeita, nanyi mkakataa kusikiliza; nimeunyosha mkono wangu, wala hakuna aliyezingatia.
25 Y desechasteis todo consejo mío, y no quisisteis mi reprensión:
Lakini mumedharau mafundisho yangu yote na wala hamkuzingatia maelekezo yangu.
26 También yo me reiré en vuestra calamidad; y me burlaré cuando os viniere lo que teméis.
Nitacheka katika taabu yenu, nitawadhihaki wakati wa kupatwa taabu-
27 Cuando viniere, como una destrucción, lo que teméis; y vuestra calamidad viniere como un torbellino: cuando viniere sobre vosotros tribulación y angustia:
hofu ya kutisha itawapata kama tufani na maafa yatawakumba kama upepo wa kisulisuli, taabu na uchungu vitawapata.
28 Entonces me llamarán, y no responderé: buscarme han de mañana, y no me hallarán:
Halafu wataniita, nami sitawajibu; wataniita katika hali ya kukata tamaa lakini hawataniona.
29 Por cuanto aborrecieron la sabiduría; y no escogieron el temor de Jehová:
Kwa sababu wamechukia maarifa na hawakuchagua kuwa na hofu ya Yehova,
30 Ni quisieron mi consejo; y menospreciaron toda reprensión mía.
hawakufuata mafundisho yangu na wakayadharau masahihisho yangu yote.
31 Comerán pues del fruto de su camino; y de sus consejos se hartarán.
Watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa kwa matunda ya hila zao wenyewe.
32 Porque el reposo de los ignorantes los matará; y la prosperidad de los insensatos los echará a perder.
kwa maana wajinga hufa wanaporudi nyuma, na kutojali kwa wapumbavu kutawaangamiza.
33 Mas el que me oyere, habitará confiadamente; y vivirá reposado de temor de mal.
Bali kila anisikilizaye ataishi kwa usalama na atapumzika salama pasipo hofu ya maafa.

< Proverbios 1 >