< Números 33 >

1 Estas son las partidas de los hijos de Israel, que salieron de la tierra de Egipto por sus escuadrones, por mano de Moisés y Aarón,
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 Que Moisés escribió sus salidas por sus partidas por dicho de Jehová: y estas son sus partidas por sus salidas.
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 De Ramesses partieron el mes primero a los quince días del mes primero: el segundo día de la pascua salieron los hijos de Israel con mano alta a ojos de todos los Egipcios.
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 Enterrando los Egipcios los que Jehová había muerto de ellos, a todo primogénito; y habiendo Jehová hecho juicios en sus dioses.
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 Partieron pues los hijos de Israel de Ramesses, y asentaron campo en Socot.
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 Y partiendo de Socot asentaron en Etam, que es al cabo del desierto.
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 Y partiendo de Etam volvieron sobre Pihahirot, que es delante de Baal-sefón, y asentaron delante de Magdalo.
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 Y partiendo de Pihahirot pasaron por medio de la mar al desierto, y anduvieron camino de tres días por el desierto de Etam, y asentaron en Mara.
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 Y partiendo de Mara vinieron a Elim, donde había doce fuentes de aguas y setenta palmas; y asentaron allí.
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 Y partidos de Elim asentaron junto al mar Bermejo.
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 Y partidos del mar Bermejo asentaron en el desierto de Sin.
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 Y partidos del desierto de Sin asentaron en Dafca.
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 Y partidos de Dafca asentaron en Alús.
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 Y partidos de Alús asentaron en Rafidim, donde el pueblo no tuvo aguas para beber.
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 Y partidos de Rafidim asentaron en el desierto de Sinaí.
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 Y partidos del desierto de Sinaí asentaron en Kibrot-hattaava.
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 Y partidos de Kibrot-hattaava asentaron en Jaserot.
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 Y partidos de Jaserot asentaron en Retma.
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 Y partidos de Retma asentaron en Remmon-fares.
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 Y partidos de Remmon-fares asentaron en Lebna.
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 Y partidos de Lebna asentaron en Ressa.
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 Y partidos de Ressa asentaron en Cealata.
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 Y partidos de Cealata asentaron en el monte de Sefer.
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 Y partidos del monte de Sefer asentaron en Harada.
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 Y partidos de Harada asentaron en Macelot.
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 Y partidos de Macelot asentaron en Tahat.
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 Y partidos de Tahat asentaron en Tare.
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 Y partidos de Tare asentaron en Metca.
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 Y partidos de Metca asentaron en Hesmona.
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 Y partidos de Hesmona asentaron en Moserot.
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 Y partidos de Moserot asentaron en Bene-jaacán.
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 Y partidos de Bene-jaacán asentaron en el monte de Guidgad.
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 Y partidos del monte de Guidgad asentaron en Jetebata.
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 Y partidos de Jetebata asentaron en Hebrona.
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 Y partidos de Hebrona asentaron en Asión-gaber.
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 Y partidos de Asión-gaber asentaron en el desierto de Zin, que es Cádes.
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 Y partidos de Cádes asentaron en el monte de Hor en el fin de la tierra de Edom.
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 Y subió Aarón el sacerdote en el monte de Hor, conforme al dicho de Jehová, y allí murió a los cuarenta años de la salida de los hijos de Israel de la tierra de Egipto, en el mes quinto, en el primero del mes.
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 Y era Aarón de edad de ciento y veinte y tres años cuando murió en el monte de Hor.
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 Y oyó el Cananeo rey de Arad, que habitaba al mediodía en la tierra de Canaán, como habían entrado los hijos de Israel.
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 Y partidos del monte de Hor asentaron en Salmona.
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 Y partidos de Salmona asentaron en Funón.
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 Y partidos de Funón asentaron en Obot.
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 Y partidos de Obot asentaron en Je-abarim en el término de Moab.
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 Y partidos de Je-abarim asentaron en Dibon-gad.
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 Y partidos de Dibon-gad asentaron en Helmon-deblataim.
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 Y partidos de Helmon-deblataim asentaron en los montes de Abarim delante de Nebo.
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 Y partidos de los montes de Abarim asentaron en los campos de Moab junto al Jordán de Jericó.
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 Finalmente asentaron junto al Jordán desde Bet-jesimot hasta Abel-satim en los campos de Moab.
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 Y habló Jehová a Moisés en los campos de Moab junto al Jordán de Jericó, diciendo:
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 Habla a los hijos de Israel, y díles: Cuando hubiereis pasado el Jordán a la tierra de Canaán,
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 Echaréis a todos los moradores de la tierra de delante de vosotros, y destruiréis todas sus pinturas, y todas sus imágenes de fundición, destruiréis asimismo todos sus altos:
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 Y echaréis los moradores de la tierra, y habitaréis en ella: porque yo os la he dado para que la heredéis.
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 Y heredaréis la tierra por suertes por vuestras familias; al mucho daréis mucho por su heredad, y al poco daréis poco por su heredad: donde le saliere la suerte, allí la tendrá: por las tribus de vuestros padres heredaréis.
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 Y si no echareis los moradores de la tierra de delante de vosotros, será, que los que dejareis de ellos serán por aguijones en vuestros ojos, y por espinas en vuestros costados, y afligiros han sobre la tierra en que vosotros habitareis.
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 Y será, que como yo pensé hacerles a ellos, haré a vosotros.
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”

< Números 33 >