< Job 5 >

1 Ahora pues da voces, si habrá quien te responda; y si habrá alguno de los santos a quien mires.
“Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
2 Es cierto que al insensato la ira le mata; y al codicioso consume la envidia.
Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
3 Yo he visto al necio que echaba raíces, y en la misma hora maldije su habitación.
Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
4 Sus hijos serán lejos de la salud, y en la puerta serán quebrantados, y no habrá quien los libre.
Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
5 Hambrientos comerán su segada, y la sacarán de entre las espinas; y sedientos beberán su hacienda.
Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
6 Porque la pena no sale del polvo, ni la molestia reverdece de la tierra.
Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
7 Antes como las centellas se levantan para volar por el aire, así el hombre nace para la aflicción.
Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
8 Ciertamente yo buscaría a Dios, y depositaría en él mis negocios;
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
9 El cual hace grandes cosas, que no hay quien las comprenda; y maravillas que no tienen cuento:
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10 Que da la lluvia sobre la haz de la tierra, y envía las aguas sobre las haces de las plazas:
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11 Que pone los humildes en altura, y los enlutados son levantados a salud:
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
12 Que frustra los pensamientos de los astutos, para que sus manos no hagan nada:
Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
13 Que prende a los sabios en su astucia, y el consejo de los perversos es entontecido.
Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
14 De día se topan con tinieblas, y en mitad del día andan a tiento, como en noche.
Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
15 Y libra de la espada al pobre, de la boca de los impíos, y de la mano violenta.
Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
16 Que es esperanza al menesteroso, y la iniquidad cerró su boca.
Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
17 He aquí, que bienaventurado es el hombre a quien Dios castiga: por tanto no menosprecies la corrección del Todopoderoso.
“Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
18 Porque él es el que hace la llaga, y él que la ligará: el hiere, y sus manos curan.
Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
19 En seis tribulaciones te librará, y en la séptima no te tocará el mal.
Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
20 En la hambre te redimirá de la muerte, y en la guerra, de las manos de la espada.
Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
21 Del azote de la lengua serás encubierto: ni temerás de la destrucción, cuando viniere.
Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
22 De la destrucción y de la hambre te reirás, y no temerás de las bestias del campo.
Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
23 Y aun con las piedras del campo tendrás tu concierto, y las bestias del campo te serán pacíficas.
Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
24 Y sabrás que hay paz en tu tienda; y visitarás tu morada, y no pecarás.
Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
25 Y entenderás que tu simiente es mucha; y tus pimpollos, como la yerba de la tierra.
Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
26 Y vendrás en la vejez a la sepultura, como el montón de trigo que se coge a su tiempo.
Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
27 He aquí lo que hemos inquirido, lo cual es así: óyelo, y tú sabe para ti.
“Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”

< Job 5 >