< Job 38 >

1 Y respondió Jehová a Job desde la oscuridad, y dijo:
Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
2 ¿Quién es este que oscurece el consejo con palabras sin sabiduría?
“Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
3 Ahora ciñe como varón tus lomos: preguntarte he, y me harás saber.
Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
4 ¿Dónde estabas tú, cuando yo fundaba la tierra? házme lo saber, si tienes inteligencia.
Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
5 ¿Quién ordenó sus medidas, si lo sabes? ¿o quién extendió sobre ella cordel?
Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
6 ¿Sobre qué están fundadas sus basas? ¿o quién puso su piedra esquinada,
Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
7 Cuando todas las estrellas del alba alababan, y jubilaban todos los hijos de Dios?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
8 ¿Quién encerró con puertas la mar, cuando rebentó del vientre saliendo?
Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
9 ¿Cuándo puse nubes por su vestidura, y por su faja oscuridad?
wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
10 Y determiné sobre ella mi decreto, y le puse puertas y cerrojo,
Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
11 Y dije: Hasta aquí vendrás, y no pasarás adelante; y allí parará la hinchazón de tus ondas.
na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
12 ¿Has tú mandado a la mañana en tus días? ¿has mostrado al alba su lugar,
Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
13 Para que asga los fines de la tierra, y que sean sacudidos de ella los impíos?
ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
14 Trasmudándose como lodo de sello; y parándose como vestidura:
Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
15 Mas la luz de los impíos es quitada de ellos; y el brazo enaltecido es quebrantado.
'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
16 ¿Has tú entrado hasta los profundos de la mar, y has andado escudriñando el abismo?
Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
17 ¿Te han sido descubiertas las puertas de la muerte? ¿y has visto las puertas de la sombra de muerte?
Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
18 ¿Has tú considerado hasta las anchuras de la tierra? Declara, si sabes todo esto.
Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
19 ¿Por dónde va el camino a la habitación de la luz? ¿y el lugar de las tinieblas, donde es?
Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
20 ¿Si la tomarás tú en sus términos? ¿y si entenderás las sendas de su casa?
Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
21 ¿Si sabías tú cuándo habías de nacer? ¿y si el número de tus días había de ser grande?
Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
22 ¿Has tú entrado en los tesoros de la nieve? ¿y has visto los tesoros del granizo,
Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
23 Lo cual yo he guardado para el tiempo de la angustia, para el día de la guerra, y de la batalla?
vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
24 ¿Cuál sea el camino por donde se reparte la luz; por donde se esparce el viento solano sobre la tierra?
Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
25 ¿Quién repartió conducto al turbión; y camino a los relámpagos y truenos;
Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
26 Haciendo llover sobre la tierra deshabitada; sobre el desierto, donde no hay hombre;
na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
27 Para hartar la tierra desierta; e inculta; y para hacer producir verdura de renuevos?
kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
28 ¿Tiene la lluvia padre? ¿o quién engendró las gotas del rocío?
Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
29 ¿De vientre de quién salió el hielo? ¿y la helada del cielo, quién la engendró?
Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
30 Las aguas se tornan a manera de piedra, y la haz del abismo se aprieta.
Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
31 ¿Detendrás tú los deleites de las Pléyades? ¿o desatarás las ataduras del Orión?
Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
32 ¿Sacarás tú a su tiempo los signos de los cielos? ¿o guiarás el Arcturo con sus hijos?
Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
33 ¿Supiste tú las ordenanzas de los cielos? ¿Dispondrás tú de su potestad en la tierra?
Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
34 ¿Alzarás tú a las nubes tu voz, para que te cubra multitud de aguas?
Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
35 ¿Enviarás tú los relámpagos, para que ellos vayan? ¿y diránte ellos a ti: Hénos aquí?
Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
36 ¿Quién puso la sabiduría en los riñones? ¿o quién dio al entendimiento la inteligencia?
Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
37 ¿Quién puso por cuenta los cielos con sabiduría? ¿y los odres de los cielos, quién los hizo parar,
Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
38 Cuando el polvo se ha endurecido con dureza, y los terrones se pegaron unos a otros?
wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
39 ¿Cazarás tú la presa para el león? ¿y henchirás la hambre de los leoncillos,
Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
40 Cuando están echados en las cuevas, y se están en sus cabañas para asechar?
wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
41 ¿Quién preparó al cuervo su caza, cuando sus pollos dan voces a Dios, perdidos sin comida?
Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?

< Job 38 >