< Job 38 >

1 Y respondió Jehová a Job desde la oscuridad, y dijo:
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 ¿Quién es este que oscurece el consejo con palabras sin sabiduría?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Ahora ciñe como varón tus lomos: preguntarte he, y me harás saber.
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 ¿Dónde estabas tú, cuando yo fundaba la tierra? házme lo saber, si tienes inteligencia.
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 ¿Quién ordenó sus medidas, si lo sabes? ¿o quién extendió sobre ella cordel?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 ¿Sobre qué están fundadas sus basas? ¿o quién puso su piedra esquinada,
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 Cuando todas las estrellas del alba alababan, y jubilaban todos los hijos de Dios?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 ¿Quién encerró con puertas la mar, cuando rebentó del vientre saliendo?
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 ¿Cuándo puse nubes por su vestidura, y por su faja oscuridad?
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 Y determiné sobre ella mi decreto, y le puse puertas y cerrojo,
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 Y dije: Hasta aquí vendrás, y no pasarás adelante; y allí parará la hinchazón de tus ondas.
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 ¿Has tú mandado a la mañana en tus días? ¿has mostrado al alba su lugar,
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 Para que asga los fines de la tierra, y que sean sacudidos de ella los impíos?
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 Trasmudándose como lodo de sello; y parándose como vestidura:
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 Mas la luz de los impíos es quitada de ellos; y el brazo enaltecido es quebrantado.
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 ¿Has tú entrado hasta los profundos de la mar, y has andado escudriñando el abismo?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 ¿Te han sido descubiertas las puertas de la muerte? ¿y has visto las puertas de la sombra de muerte?
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 ¿Has tú considerado hasta las anchuras de la tierra? Declara, si sabes todo esto.
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 ¿Por dónde va el camino a la habitación de la luz? ¿y el lugar de las tinieblas, donde es?
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 ¿Si la tomarás tú en sus términos? ¿y si entenderás las sendas de su casa?
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 ¿Si sabías tú cuándo habías de nacer? ¿y si el número de tus días había de ser grande?
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 ¿Has tú entrado en los tesoros de la nieve? ¿y has visto los tesoros del granizo,
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 Lo cual yo he guardado para el tiempo de la angustia, para el día de la guerra, y de la batalla?
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 ¿Cuál sea el camino por donde se reparte la luz; por donde se esparce el viento solano sobre la tierra?
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 ¿Quién repartió conducto al turbión; y camino a los relámpagos y truenos;
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 Haciendo llover sobre la tierra deshabitada; sobre el desierto, donde no hay hombre;
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 Para hartar la tierra desierta; e inculta; y para hacer producir verdura de renuevos?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 ¿Tiene la lluvia padre? ¿o quién engendró las gotas del rocío?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 ¿De vientre de quién salió el hielo? ¿y la helada del cielo, quién la engendró?
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 Las aguas se tornan a manera de piedra, y la haz del abismo se aprieta.
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 ¿Detendrás tú los deleites de las Pléyades? ¿o desatarás las ataduras del Orión?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 ¿Sacarás tú a su tiempo los signos de los cielos? ¿o guiarás el Arcturo con sus hijos?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 ¿Supiste tú las ordenanzas de los cielos? ¿Dispondrás tú de su potestad en la tierra?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 ¿Alzarás tú a las nubes tu voz, para que te cubra multitud de aguas?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 ¿Enviarás tú los relámpagos, para que ellos vayan? ¿y diránte ellos a ti: Hénos aquí?
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 ¿Quién puso la sabiduría en los riñones? ¿o quién dio al entendimiento la inteligencia?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 ¿Quién puso por cuenta los cielos con sabiduría? ¿y los odres de los cielos, quién los hizo parar,
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 Cuando el polvo se ha endurecido con dureza, y los terrones se pegaron unos a otros?
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 ¿Cazarás tú la presa para el león? ¿y henchirás la hambre de los leoncillos,
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 Cuando están echados en las cuevas, y se están en sus cabañas para asechar?
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 ¿Quién preparó al cuervo su caza, cuando sus pollos dan voces a Dios, perdidos sin comida?
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

< Job 38 >