< Job 30 >

1 Mas ahora los más mozos de días que yo, se rien de mí, cuyos padres yo desdeñara de ponerlos con los perros de mi ganado,
“Lakini sasa watu wadogo kwa umri kuniliko wananidhihaki, watu ambao baba zao ningekataa kwa dharau kuwaweka pamoja na mbwa wangu wa kulinda kondoo.
2 Porque ¿para qué había yo menester la fuerza de sus manos, en los cuales pereció el tiempo?
Nguvu za mikono yao zingekuwa na faida gani kwangu, kwa kuwa nguvu zao zilikuwa zimewaishia?
3 Por causa de la pobreza y de la hambre solos: que huían a la soledad, al lugar tenebroso, asolado y desierto.
Wakiwa wamekonda kutokana na kupungukiwa na kwa njaa, walizurura usiku katika nchi kame iliyo ukiwa.
4 Que cogían malvas entre los árboles, y raíces de enebros para calentarse.
Katika vichaka walikusanya mimea ya chumvi, nacho chakula chao kilikuwa mizizi ya mti wa mfagio.
5 Eran echados de entre las gentes, y todos les daban grita como a ladrón.
Walifukuzwa mbali na watu wao, wakipigiwa kelele kama wevi.
6 Que habitaban en las barrancas de los arroyos, en las cavernas de la tierra, y en las piedras.
Walilazimika kuishi katika mikondo ya vijito vilivyokauka, kwenye majabali na mahandaki.
7 Que bramaban entre las matas, y se congregaban debajo de las espinas.
Kwenye vichaka walilia kama punda, na walijisongasonga pamoja kwenye vichaka.
8 Hijos de viles, y hombres sin nombre: mas bajos que la misma tierra.
Wao ni watoto wa wapumbavu wenye asili ya ubaya, waliofukuzwa watoke katika nchi.
9 Y ahora yo soy su canción, y soy hecho a ellos refrán.
“Nao sasa wana wao wananidhihaki katika nyimbo; nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.
10 Abomínanme, aléjanse de mí; y aun de mi rostro no detuvieron su saliva.
Wananichukia sana na kujitenga nami, wala hawasiti kunitemea mate usoni.
11 Porque Dios desató mi cuerda, y me afligió; y quitaron el freno delante de mi rostro.
Sasa kwa kuwa Mungu ameilegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa, wamekuwa huru kunitendea waonavyo.
12 A la mano derecha se levantaron los muchachos; rempujaron mis pies, y pisaron sobre mí las sendas de su contrición.
Kuume kwangu kundi linashambulia; wao huitegea miguu yangu tanzi, na kunizingira.
13 Mi senda derribaron: aprovecháronse de mi quebrantamiento; contra los cuales no hubo ayudador.
Huizuia njia yangu, nao hufanikiwa katika kuniletea maafa, nami sina yeyote wa kunisaidia.
14 Vinieron como por portillo ancho: revolviéronse por mi calamidad.
Wananijia kama watu wapitao katika ufa mpana; katikati ya magofu huja na kunishambulia.
15 Turbaciones se convirtieron sobre mí: combatieron como un viento mi voluntad, y mi salud como nube que pasa.
Vitisho vimenifunika; heshima yangu imetoweshwa kama kwa upepo, salama yangu imetoweka kama wingu.
16 Y ahora mi alma está derramada en mí: días de aflicción me han comprendido.
“Sasa maisha yangu yamefikia mwisho; siku za mateso zimenikamata.
17 De noche taladra sobre mí mis huesos, y mis pulsos no reposan.
Usiku mifupa yangu inachoma; maumivu yanayonitafuna hayatulii kamwe.
18 Con la grandeza de la fuerza del dolor mi vestidura es mudada; cíñeme como el collar de mi ropa.
Kwa uwezo wake mkuu Mungu huwa kwangu kama nguo; hushikamana nami kama ukosi wa vazi langu.
19 Derribóme en el lodo, y soy semejante al polvo, y a la ceniza.
Yeye amenitupa kwenye matope, nami nimekuwa kama mavumbi na majivu.
20 Clamo a ti, y no me oyes: me presento, y no me echas de ver.
“Ee Bwana, ninakulilia wewe lakini hunijibu; ninasimama, nawe unanitazama tu.
21 Háste tornado cruel para mí: con la fortaleza de tu mano me amenazas.
Wewe unanigeukia bila huruma; unanishambulia kwa nguvu za mkono wako.
22 Levantásteme, e hicísteme cabalgar sobre el viento, y derretiste en mí el ser.
Unaninyakua na kunipeperusha kwa upepo; umenirusha huku na huko kwenye dhoruba kali.
23 Porque yo conozco que me tornas a la muerte, y a la casa determinada a todo viviente.
Ninajua utanileta mpaka kifoni, mahali ambapo wenye uhai wote wamewekewa.
24 Mas él no extenderá la mano contra el sepulcro; ¿clamarán los sepultados cuando él los quebrantare?
“Hakika hakuna yeyote amshambuliaye mhitaji, anapoomba msaada katika shida yake.
25 ¿No lloré yo al afligido, y mi alma no se entristeció sobre el menesteroso?
Je, sikulia kwa ajili ya wale waliokuwa katika taabu? Je, nafsi yangu haikusononeka kwa ajili ya maskini?
26 Cuando esperaba el bien, entonces me vino el mal; y cuando esperaba la luz, vino la oscuridad.
Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinijia; nilipotafuta nuru, ndipo giza lilipokuja.
27 Mis entrañas hierven, y no reposan: previniéronme días de aflicción.
Kusukwasukwa ndani yangu kamwe hakutulii; siku za mateso zinanikabili.
28 Denegrido anduve, y no por el sol: levantéme en la congregación, y clamé.
Ninazunguka nikiwa nimeungua, lakini si kwa jua; ninasimama katika kusanyiko nikiomba msaada.
29 Hermano fui de los dragones, y compañero de las hijas del avestruz.
Nimekuwa ndugu wa mbweha, rafiki wa mabundi.
30 Mi cuero está denegrido sobre mí, y mis huesos se secaron con sequedad.
Ngozi yangu imekuwa nyeusi nayo inachunika; mifupa yangu inaungua kwa homa.
31 Y mi arpa se tornó en luto, y mi órgano en voz de lamentantes.
Kinubi changu kimegeuka kuwa maombolezo, nayo filimbi yangu imekuwa sauti ya kilio.

< Job 30 >