< Job 21 >

1 Y respondió Job, y dijo:
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
2 Oíd atentamente mi palabra, y sea esto por vuestros consuelos.
“Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
3 Soportádme, y yo hablaré; y después que hubiere hablado, escarnecéd.
Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
4 ¿Hablo yo a algún hombre? y si es así, ¿por qué no se angustiará mi espíritu?
Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
5 Mirádme, y espantáos, y ponéd la mano sobre la boca.
Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
6 Que cuando yo me acuerdo, me asombro; y toma temblor mi carne.
Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
7 ¿Por qué viven los impíos, y se envejecen, y aun crecen en riquezas?
Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
8 Su simiente con ellos, compuesta delante de ellos; y sus renuevos delante de sus ojos.
Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
9 Sus casas seguras de temor, ni hay sobre ellos azote de Dios.
Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
10 Sus toros engendran y no yerran: paren sus vacas y no amueven.
Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
11 Echan sus chiquitos como manada de ovejas, y sus hijos andan saltando.
Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
12 A son de tamboril y de vihuela saltan; y se huelgan al son del órgano.
Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
13 Gastan sus días en bien, y en un momento descienden a la sepultura. (Sheol h7585)
Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol h7585)
14 Y dicen a Dios: Apártate de nosotros, que no queremos el conocimiento de tus caminos.
Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
15 ¿Quién es el Todopoderoso para que le sirvamos? ¿y de qué nos aprovechará que oremos a él?
Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
16 He aquí, que su bien no está en su mano: el consejo de los impíos lejos esté de mí.
Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
17 ¡Oh cuántas veces la antorcha de los impíos es apagada; y viene sobre ellos su contrición; y con su ira Dios les reparte dolores!
Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
18 Serán como la paja delante del viento, y como el tamo que arrebata el torbellino.
Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
19 Dios guardará para sus hijos su violencia; y le dará su pago, para que conozca.
Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
20 Verán sus ojos su quebranto; y beberá de la ira del Todopoderoso.
Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
21 Porque ¿qué deleite tendrá él de su casa después de sí, siendo cortado el número de sus meses?
Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
22 ¿Enseñará él a Dios sabiduría, juzgando él las alturas?
Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
23 Este morirá en la fortaleza de su hermosura todo quieto y pacífico.
Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
24 Sus pechos están llenos de leche, y sus huesos serán regados de tuétano.
Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
25 Y estotro morirá con amargo ánimo, y no comerá con bien.
Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
26 Juntamente yacerán sobre la tierra, y gusanos los cubrirán.
Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
27 He aquí, que yo conozco vuestros pensamientos, y las imaginaciones que contra mí forjáis.
Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
28 Porque decís: ¿Qué es de la casa del príncipe? ¿y qué es de la tienda de las moradas de los impíos?
Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
29 ¿No habéis preguntado a los que pasan por los caminos, cuyas señas no negaréis?
Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
30 Que el malo es guardado del día de la contrición, del día de las iras son llevados.
kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
31 ¿Quién le denunciará en su cara su camino? ¿y de lo que él hizo, quién le dará el pago?
Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
32 Porque él ya será llevado a los sepulcros, y en el montón permanecerá.
Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
33 Los terrones del arroyo le serán ya dulces; y tras de él será llevado todo hombre, y antes de él no hay número.
Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
34 ¿Cómo pues me consoláis en vano, pues vuestras respuestas quedan por mentira?
Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”

< Job 21 >