< Éxodo 40 >

1 Y Jehová habló a Moisés, diciendo:
Kisha Bwana akamwambia Mose:
2 En el día del mes primero, el primero del mes harás levantar el tabernáculo, el tabernáculo del testimonio.
“Simika Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
3 Y pondrás en él el arca del testimonio, y cubrirla has con el velo.
Weka Sanduku la Ushuhuda ndani yake na ulifunike kwa pazia. Ingiza meza na kupanga vitu vyake juu yake.
4 Y meterás la mesa, y ponerla has en orden: y meterás el candelero, y encenderás sus lámparas.
Kisha ingiza kinara cha taa na uweke taa zake juu yake.
5 Y pondrás el altar de oro para el perfume delante del arca del testimonio: y pondrás el pabellón de la puerta del tabernáculo.
Weka madhabahu ya dhahabu ya kufukizia uvumba mbele ya Sanduku la Ushuhuda kisha uweke pazia kwenye lango la Maskani ya Mungu.
6 Después pondrás el altar del holocausto delante de la puerta del tabernáculo, del tabernáculo del testimonio.
“Weka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa mbele ya lango la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania;
7 Luego pondrás la fuente entre el tabernáculo del testimonio y el altar: y pondrás agua en ella.
weka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, na uweke maji ndani yake.
8 Finalmente pondrás el patio al rededor, y el pabellón de la puerta del patio.
Fanyiza ua kuzunguka maskani na uweke pazia penye ingilio la ua.
9 Y tomarás el aceite de la unción, y ungirás el tabernáculo, y todo lo que estará en él, y santificarlo has con todos sus vasos, y será santo.
“Chukua mafuta ya upako, ipake Maskani ya Mungu pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake; iweke wakfu pamoja na vitu vyote vilivyomo ndani mwake, nayo itakuwa takatifu.
10 Y ungirás también el altar del holocausto, y todos sus vasos: y santificarás el altar, y será el altar santidad de santidades.
Kisha yapake mafuta hayo madhabahu ya kuteketezea sadaka pamoja na vifaa vyake vyote; weka wakfu madhabahu nayo yatakuwa takatifu sana.
11 Asimismo ungirás la fuente y su basa, y santificarla has.
Paka sinia mafuta pamoja na kishikilio chake na uviweke wakfu.
12 Y harás llegar a Aarón y a sus hijos a la puerta del tabernáculo del testimonio, y lavarlos has con agua.
“Mlete Aroni na wanawe kwenye ingilio la Hema la Kukutania na uwaoshe kwa maji.
13 Y harás vestir a Aarón las santas vestiduras, y ungirle has, y consagrarle has, para que sea mi sacerdote.
Kisha mvike Aroni yale mavazi matakatifu, umtie mafuta na kumweka wakfu ili apate kunitumikia katikati ya ukuhani.
14 Después harás llegar sus hijos, y vestirles has las túnicas.
Walete wanawe na uwavike makoti.
15 Y ungirles has como ungiste a su padre, y serán mis sacerdotes: y será, que su unción les será por sacerdocio perpetuo por sus generaciones.
Kisha watie mafuta kama ulivyomtia baba yao, ili nao pia wanitumikie katika kazi ya ukuhani. Kutiwa mafuta kwao kutakuwa kwa ajili ya ukuhani utakaoendelea kwa vizazi vyote vijavyo.”
16 E hizo Moisés conforme a todo lo que Jehová le mandó: así lo hizo.
Mose akafanya kila kitu sawa kama vile Bwana alivyomwagiza.
17 Así en el mes primero, en el segundo año al primero del mes, el tabernáculo fue levantado.
Kwa hiyo Maskani ya Mungu ilisimikwa katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, katika mwaka wa pili.
18 E hizo Moisés levantar el tabernáculo, y puso sus basas, y puso sus tablas, y puso sus barras, e hizo alzar sus columnas.
Mose alipoweka wakfu Maskani ya Mungu, aliweka vitako mahali pake, akasimamisha mihimili, akatia mataruma na kusimamisha nguzo.
19 Y tendió la tienda sobre el tabernáculo, y puso el cobertor sobre el tabernáculo encima, como Jehová había mandado a Moisés.
Kisha akalitandaza hema juu ya Maskani ya Mungu na kuifunika hema, kama Bwana alivyomwagiza.
20 Y tomó, y puso el testimonio en el arca; y puso las barras sobre el arca: y la cubierta sobre el arca encima.
Akachukua ule Ushuhuda na kuuweka ndani ya Sanduku la Agano, akaweka ile mipiko ya kubebea hilo Sanduku na kuweka kiti cha rehema juu yake.
21 Y metió el arca en el tabernáculo: y puso el velo de la tienda, y cubrió el arca del testimonio, como Jehová había mandado a Moisés.
Kisha Mose akalileta Sanduku ndani ya Maskani ya Mungu, akatundika pazia ili kulifunika Sanduku la Ushuhuda, kama Bwana alivyomwagiza.
22 Y puso la mesa en el tabernáculo del testimonio al lado del aquilón del pabellón fuera del velo.
Mose akaweka meza ndani ya Hema la Kukutania, upande wa kaskazini ya Maskani ya Mungu nje ya pazia
23 Y sobre ella puso por orden los panes delante de Jehová, como Jehová había mandado a Moisés.
na kupanga mikate juu yake mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
24 Y puso el candelero en el tabernáculo del testimonio en frente de la mesa, al lado del mediodía del pabellón.
Akaweka kinara cha taa ndani ya Hema la Kukutania mkabala na meza upande wa kusini mwa Maskani ya Mungu
25 Y encendió las lámparas delante de Jehová, como Jehová había mandado a Moisés.
na kuziweka taa mbele za Bwana, kama Bwana alivyomwagiza.
26 Puso también el altar de oro en el tabernáculo del testimonio, delante del velo.
Mose akaweka madhabahu ya dhahabu ndani ya Hema la Kukutania mbele ya pazia
27 Y encendió sobre él el perfume aromático, como Jehová había mandado a Moisés.
na kufukiza uvumba wenye harufu nzuri, kama Bwana alivyomwagiza.
28 Puso asimismo el pabellón de la puerta del tabernáculo.
Kisha akaweka pazia kwenye ingilio la Maskani ya Mungu.
29 Y puso el altar del holocausto a la puerta del tabernáculo, del tabernáculo del testimonio: y ofreció sobre el holocausto y presente, como Jehová había mandado a Moisés.
Mose akaweka madhabahu ya sadaka za kuteketezwa karibu na ingilio la Maskani ya Mungu, yaani Hema la Kukutania, na kutoa juu yake sadaka za kuteketezwa na sadaka za nafaka kama Bwana alivyomwagiza.
30 Y puso la fuente entre el tabernáculo del testimonio y el altar: y puso en ella agua para lavar.
Akaweka sinia kati ya Hema la Kukutania na madhabahu, akaweka maji ndani yake kwa ajili ya kunawia,
31 Y lavaban en ella Moisés, y Aarón, y sus hijos sus manos y sus pies.
Naye Mose, Aroni na wanawe wakayatumia kwa kunawia mikono na miguu yao.
32 Cuando entraban en el tabernáculo del testimonio, y cuando se llegaban al altar se lavaban, como Jehová había mandado a Moisés.
Wakanawa kila walipoingia katika Hema la Kukutania au walipoikaribia madhabahu kama Bwana alivyomwagiza Mose.
33 Finalmente levantó el patio en derredor del tabernáculo y del altar, y puso el pabellón de la puerta del patio: y así acabó Moisés la obra.
Kisha Mose akafanya ua kuizunguka Maskani ya Mungu na madhabahu, pia akaweka pazia kwenye ingilio la huo ua. Hivyo Mose akaikamilisha kazi.
34 Entonces una nube cubrió el tabernáculo del testimonio, y la gloria de Jehová hinchió el tabernáculo.
Ndipo wingu likafunika Hema la Kukutania, na utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
35 Y no podía Moisés entrar en el tabernáculo del testimonio, porque la nube estaba sobre él, y la gloria de Jehová lo tenía lleno.
Mose hakuweza kuingia ndani ya Hema la Kukutania kwa sababu wingu lilikuwa limetua juu ya Hema, nao utukufu wa Bwana ukaijaza Maskani ya Mungu.
36 Y cuando la nube se alzaba del tabernáculo, los hijos de Israel se movían en todas sus partidas.
Katika safari yote ya Waisraeli, kila wakati wingu lilipoinuka kutoka juu ya Maskani ya Mungu, wangeondoka;
37 Y si la nube no se alzaba, no se partían, hasta el día que ella se alzaba.
lakini kama wingu halikuinuka, hawakuondoka, mpaka siku lilipoinuka.
38 Porque la nube de Jehová estaba de día sobre el tabernáculo, y el fuego estaba de noche en él, en ojos de toda la casa de Israel en todas sus partidas.
Kwa hiyo wingu la Bwana lilikuwa juu ya maskani mchana, na moto ulikuwa katika hilo wingu wakati wa usiku, machoni pa nyumba yote ya Israeli siku zote za safari zao.

< Éxodo 40 >