< Eclesiastés 10 >

1 Las moscas muertas hacen heder y dar mal olor el perfume del perfumador; y al estimado por sabiduría y honra una pequeña insensatez.
Kama nzi walio kufa husababisha manukato kutoa harufu ya uozo, hivyo hivyo upumbavu kidogo hushinda hekima na heshima.
2 El corazón del sabio está a su mano derecha: mas el corazón del insensato, a su mano izquierda.
Moyo wa mtu mwenye hekima huelekea kulia, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
3 Y aun cuando el insensato va por el camino, su cordura falta; y dice a todos: insensato es.
Wakati mpumbavu anapotembea barabarani, fikira zake zina upungufu, ikithibitisha kwa kila mtu kwamba ni mpumbavu.
4 Si espíritu de señor te acometiere, no dejes tu lugar; porque la flojedad hará reposar grandes pecados.
Kama jaziba za mtawala zikiinuka kinyume na wewe, usiache kazi yako. Utulivu unaweza kutuliza ukatili mkubwa.
5 Hay otro mal que ví debajo del sol, como salido de delante del señor por yerro:
Kuna uovu niliouona chini ya jua, aina ya kosa ambalo huja kutoka kwa mtawala:
6 La insensatez está asentada en grandes alturas; y los ricos están sentados en bajeza.
Wapumbavu wanapewa nafasi za uongozi, wakati watu walio faulu wanapewa nafasi za chini.
7 Ví siervos encima de caballos, y príncipes que andaban, como siervos, a tierra.
Nimewaona watumwa wakipanda farasi, na watu walio faulu wakitembea kama watumwa juu ya ardhi.
8 El que hiciere el hoyo, caerá en él; y el que aportillare el vallado, morderle ha la serpiente.
Yeyote anayechimba shimo anaweza kutumbukia yake, na popote mtu anayevunja ukuja, nyoka anaweza kumuuma.
9 El que mudare las piedras, tendrá trabajo en ellas: el que cortare la leña, peligrará en ella.
Yeyote achongaye mwawe, anaweza kuumizwa nayo. Na mtu achongaye mbao, anaweza kujihatarisha kwa hiyo.
10 Si se embotare el hierro, y su filo no fuere aguzado, añadir más fuerza: mas la bondad de la sabiduría excede.
Kama chuma bapa kisicho na makali, na mtu hainoi, kisha ni lazima atumie nguvu nyingi, lakini hekima hutoa faida kwa ufaulu.
11 Si la serpiente mordiere no encantada, no es más el lenguaz.
Kama nyoka akiuma kabla hajafurahi, hivyo hakuna faida kwa mfurahishaji.
12 Las palabras de la boca del sabio son gracia: mas los labios del insensato lo echan a perder.
Maneno ya kinywa cha mtu mwenye hekima yana huruma. Lakini midomo ya mpumbavu humumeza mwenyewe.
13 El principio de las palabras de su boca es insensatez; y el fin de su habla, desvarío malo.
Kama maneno yanavyo anza kutiririka mdomoni mwa mpumbavu, ujinga hutoka, na mwisho mdomo wake hutiririka wazimu mbaya.
14 El insensato multiplica palabras, y dice: No sabe hombre lo que ha de ser: ¿y quién le hará saber, lo que será después de él?
Mpumbavu huongeza maneno, lakini hakuna ajuaye kinachokuja. Ni nani ajuaye baada yake?
15 El trabajo de los insensatos los fatiga; porque no saben por donde van a la ciudad.
Jasho la wapumbavu huwavaa wao, hivyo hawajui hata barabara ya kwenda mjini.
16 ¡Ay de ti tierra, cuando tu rey fuere mozo, y tus príncipes comen de mañana!
Ole wako ardhi kama mfalme wako ni kijana mdogo, na kama viongozi wako huanza karamu ahsubuhi!
17 ¡Bienaventurada tierra tú, cuando tu rey fuere hijo de nobles, y tus príncipes comen a su hora por la fuerza, y no por el beber!
Lakini umebarikiwa ardhi kama mfalme wako ni mwana wa waungwana, na kama vingozi wako hula wakati muafaka, kwa nguvu, na sio kwa ulevi.
18 Por la pereza se cae la techumbre; y por la flojedad de manos se llueve la casa.
Kwa sababu ya uvivu paa huanguka. Na kwa sababu isiyo fanya kazi nyumba hupata ufa.
19 Por el placer se hace el convite, y el vino alegra los vivos; y el dinero responde a todo.
Watu huandaa chakula kwa kicheko, divai huleta furaha maishani, na fedha hutimiza hitaji kwa kila kitu.
20 Ni aun en tu pensamiento digas mal del rey; ni en los secretos de tu cámara digas mal del rico; porque las aves del cielo llevarán la voz; y las que tienen alas, harán saber la palabra.
Usimlaani mfalme, hata katika akili, na usiwalaani wenye mali katika chumba chako cha kulala. Kwa kuwa ndege wa angani inaweza kuchukua maneno yako. Chochote kilicho na mabawa kinaweza kusambaza jambo.

< Eclesiastés 10 >