< 1 Timoteo 2 >

1 Amonesto, pues, ante todas cosas, que se hagan rogativas, oraciones, peticiones y acciones de gracias, por todos los hombres:
Kwanza kabisa, basi naomba dua, sala, maombi na sala za shukrani zitolewe kwa Mungu kwa ajili ya watu wote,
2 Por los reyes, y por todos los que están en autoridad; que vivamos quieta y reposadamente en toda piedad y honestidad.
kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, ili tupate kuishi maisha ya utulivu na amani pamoja na uchaji wa Mungu na mwenendo mwema.
3 Porque esto es bueno y agradable delante de Dios Salvador nuestro:
Jambo hili ni jema na lampendeza Mungu Mwokozi wetu,
4 El cual quiere que todos los hombres sean salvos, y que vengan al conocimiento de la verdad.
ambaye anataka watu wote waokolewe na wapate kuujua ukweli.
5 Porque hay un Dios, y asimismo un solo mediador entre Dios y los hombres, el hombre Cristo Jesús;
Maana yuko Mungu mmoja, na pia yuko mmoja anayewapatanisha watu na Mungu, binadamu Kristo Yesu,
6 El cual se dio a sí mismo en precio del rescate por todos, para testimonio en su propio tiempo.
ambaye alijitoa mwenyewe kuwakomboa watu wote. Huo ulikuwa uthibitisho, wakati ufaao ulipowadia.
7 Para lo que yo soy puesto por predicador y apóstol, (digo verdad en Cristo, no miento, ) instruidor de las naciones en fe y verdad.
Kwa sababu hiyo mimi nilitumwa niwe mtume na mwalimu wa watu wa mataifa, niutangaze ujumbe wa imani na ukweli. Nasema ukweli; sisemi uongo!
8 Quiero, pues, que los varones oren en todo lugar, levantando manos limpias, sin ira ni contienda.
Basi, popote mnapokutana kufanya ibada nataka wanaume wasali, watu waliojitolea kweli na ambao wanaweza kuinua mikono yao wakisali bila hasira wala ubishi.
9 Asimismo también oren las mujeres en hábito honesto, ataviándose de vergüenza y modestia; no con cabellos encrespados, o oro, o perlas, o vestidos costosos;
Hali kadhalika, nawataka wanawake wawe wanyofu na wenye busara kuhusu mavazi yao; wavae sawasawa na si kwa urembo wa mitindo ya kusuka nywele, kujipamba kwa dhahabu, lulu au mavazi ya gharama kubwa,
10 Mas de buenas obras, como conviene a mujeres que profesan la piedad.
bali kwa matendo mema kama iwapasavyo wanawake wamchao Mungu.
11 La mujer aprenda en silencio con toda sujeción.
Wanawake wanapaswa kukaa kimya na kuwa wanyenyekevu wakati wa kujifunza.
12 Porque no permito a la mujer enseñar, ni tomarse autoridad sobre el varón, sino estar en silencio.
Mimi simruhusu mwanamke amfundishe au amtawale mwanamume; anapaswa kukaa kimya.
13 Porque Adam fue formado el primero: luego Eva.
Maana Adamu aliumbwa kwanza, halafu Hawa.
14 Y Adam no fue engañado; mas la mujer siendo engañada incurrió en la prevaricación.
Na wala si Adamu aliyedanganywa; bali mwanamke ndiye aliyedanganywa, akaivunja sheria ya Mungu.
15 Empero será salva engendrando hijos, si permaneciere en la fe y caridad, y en santificación y modestia.
Hata hivyo, mwanamke ataokolewa kwa kupata watoto, kama akidumu katika imani, upendo, utakatifu na unyofu.

< 1 Timoteo 2 >