< 1 Crónicas 3 >

1 Estos son los hijos de David, que le nacieron en Hebrón: Ammón el primogénito, de Acinoam de Jezrael. El segundo, Daniel, de Abigail del Carmelo.
Hawa ndio waliokuwa wana wa Daudi waliozaliwa huko Hebroni: Mzaliwa wa kwanza alikuwa Amnoni ambaye mama yake aliitwa Ahinoamu wa Yezreeli; wa pili, Danieli ambaye mama yake alikuwa Abigaili wa Karmeli;
2 El tercero, Absalom, hijo de Maaca hija de Tolmai rey de Gessur: el cuatro, Adonías, hijo de Aggit:
wa tatu alikuwa Absalomu, ambaye mama yake alikuwa Maaka, binti Talmai mfalme wa Geshuri; wa nne, Adoniya, ambaye mama yake alikuwa Hagithi;
3 El quinto, Safatias, de Abital: el sexto, Jetraham, de Egla su mujer.
wa tano alikuwa Shefatia ambaye mama yake alikuwa Abitali; wa sita alikuwa Ithreamu, aliyezaliwa na mke wake Egla.
4 Estos seis le nacieron en Hebrón, donde reinó siete años y seis meses: y en Jerusalem reinó treinta y tres años.
Hawa sita walizaliwa huko Hebroni ambako Daudi alitawala kwa miaka saba na miezi sita. Daudi alitawala Yerusalemu kwa miaka thelathini na mitatu,
5 Estos cuatro le nacieron en Jerusalem: Simmaa, Sobab, Natán, y Salomón de Bet-sua, hija de Ammiel.
nao hawa ndio watoto wa Daudi waliozaliwa huko Yerusalemu: mkewe Bathsheba, binti Amieli, alimzalia Shamua, Shobabu, Nathani na Solomoni.
6 Y otros nueve; Jebaar, Elisama,
Pia kulikuwa na wana wengine: Ibihari, Elishua, Elifeleti,
7 Elifalet, Nogé, Nefeg, Jafía,
Noga, Nefegi, Yafia,
8 Elisama, Eliada, y Elifalet.
Elishama, Eliada na Elifeleti; wote walikuwa tisa.
9 Todos estos fueron los hijos de David, sin los hijos de las concubinas. Y Tamar fue hermana de ellos.
Hawa wote walikuwa wana wa Daudi, mbali na wale wana waliozaliwa na masuria. Naye Tamari alikuwa dada yao.
10 Hijo de Salomón fue Roboam, cuyo hijo fue Abiá, cuyo hijo fue Asa, cuyo hijo fue Josafat,
Mwana wa Solomoni alikuwa Rehoboamu, mwanawe huyo alikuwa Abiya, mwanawe huyo alikuwa Yehoshafati, mwanawe huyo alikuwa Asa,
11 Cuyo hijo fue Joram, cuyo hijo fue Ocozías, cuyo hijo fue Joas,
mwanawe huyo alikuwa Yehoramu, mwanawe huyo alikuwa Ahazia, mwanawe huyo alikuwa Yoashi,
12 Cuyo hijo fue Amasías, cuyo hijo fue Azarías, cuyo hijo fue Joatam,
mwanawe huyo alikuwa Amazia, mwanawe huyo alikuwa Azaria, mwanawe huyo alikuwa Yothamu,
13 Cuyo hijo fue Acaz, cuyo hijo fue Ezequías, cuyo hijo fue Manasés,
mwanawe huyo alikuwa Ahazi, mwanawe huyo alikuwa Hezekia, mwanawe huyo alikuwa Manase,
14 Cuyo hijo fue Amón, cuyo hijo fue Josías.
mwanawe huyo alikuwa Amoni na mwanawe huyo alikuwa Yosia.
15 Y los hijos de Josías fueron Johanán su primogénito, el segundo Joacim, el tercero Sedecías, el cuarto Sellum.
Wana wa Yosia walikuwa: Yohanani mzaliwa wake wa kwanza, Yehoyakimu mwanawe wa pili, wa tatu Sedekia, wa nne Shalumu.
16 Los hijos de Joacim fueron Jeconías su hijo, cuyo hijo fue Sedecías.
Walioingia mahali pa Yehoyakimu kama wafalme ni: Yekonia mwanawe, na Sedekia.
17 Y los hijos de Jeconías fueron Asir, cuyo hijo fue Salatiel,
Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yekonia aliyekuwa mateka: Shealtieli mwanawe,
18 Melquiram, Padaia, Senneser, y Jecemia, Hosama, y Nadabia.
Malkiramu, Pedaya, Shenasari, Yekamia, Hoshama na Nedabia.
19 Y los hijos de Padaia fueron Zorobabel, y Semeí. Y los hijos de Zorobabel fueron Mosollam, Jananías, y Salomit su hermana;
Wana wa Pedaya walikuwa: Zerubabeli na Shimei. Wana wa Zerubabeli walikuwa: Meshulamu na Hanania. Shelomithi alikuwa dada yao.
20 Y Hasaba, Ohol, Baraquías, Hasadias, y Josabhesed, todos cinco.
Pia walikuwepo wengine watano: Hashuba, Oheli, Berekia, Hasadia na Yushab-Hesedi.
21 Los hijos de Jananías fueron Paltias, y Jesaías, hijo de Rafaias, hijo de Arnán, hijo de Abdías, hijo de Sequenías.
Wazao wa Hanania walikuwa: Pelatia na Yeshaya, na wana wa Refaya, na wana wa Arnani, na wana wa Obadia, na wana wa Shekania.
22 Hijo de Sequenías fue Semeías. Y los hijos de Semeías fueron Harus, Jegaal, Barias, Naarias, Safat, seis.
Wazao wa Shekania: Shemaya na wanawe: Hatushi, Igali, Baria, Nearia na Shafati; jumla yao walikuwa sita.
23 Los hijos de Naarias fueron estos tres, Elioenai, Ezequías, y Ezricam.
Wana wa Nearia walikuwa: Elioenai, Hizkia na Azrikamu; jumla yao watatu.
24 Los hijos de Elioenai fueron estos siete, Oduias, Eliasub, Pelaías, Accub, Johanán, Dalaias, Anani.
Wana wa Elioenai walikuwa: Hodavia, Eliashibu, Pelaya, Akubu, Yohanani, Delaya na Anani; jumla yao wote saba.

< 1 Crónicas 3 >