< 1 Crónicas 24 >

1 También los hijos de Aarón tuvieron sus repartimientos. Los hijos de Aarón fueron; Nadab, Abiú, Eleazar, Itamar,
Makundi vya kazi kulingana na uzao wa Aroni yalikuwa haya: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
2 Mas Nadab y Abiú murieron antes de su padre, y no tuvieron hijos: Eleazar e Itamar tuvieron el sacerdocio.
Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao kufa. Walikuwa hawana watoto, kwahiyo Eleazari na Ithamari walitumika kama makuhani.
3 Y David los repartió: Sadoc era de los hijos de Eleazar, y Aquimelec de los hijos de Itamar, en su cuenta, en su ministerio.
Daudi pamoja na Zadoki, uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, uzao wa Ithamari, waliwagawanya katika makundi yao ya kazi kama makuhani.
4 Y los hijos de Eleazar fueron hallados muchos más, en cuanto a sus principales varones, que los hijos de Itamar; y repartiéronlos así: De los hijos de Eleazar diez y seis cabezas por las familias de sus padres: y de los hijos de Itamar por las familias de sus padres, ocho.
Kulikuwa na wanaume viongozi zaidi kati ya uzao wa Eleazari kuliko kati ya uzao wa Ithamari, kwahiyo waligawanya uzao wa Eleazari katika makundi kumi na sita. Walifanya hivyo na viongozi wa ukoo na uzao wa Ithamari. Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi, sambamba na koo zao.
5 Y repartiéronlos por suerte los unos con los otros: porque de los hijos de Eleazar, y de los hijos de Itamar, hubo príncipes del santuario, y príncipes de Dios.
Waliwagawanya bila upendeleo kwa kura, kwa kuwa walikuwa waamuzi watakatifu na waamuzi wa Mungu, kutoka pande zote uzao wa Eleazari na uzao wa Ithamari.
6 Y Semeías, hijo de Natanael, escriba de los Levitas, los escribió delante del rey, y de los príncipes, y delante de Sadoc el sacerdote, y de Aquimelec, hijo de Abiatar, y de los príncipes de las familias de los sacerdotes y Levitas: y a Eleazar atribuyeron una familia, y a Itamar fue atribuida otra.
Shemaia mwana wa Nethaneli mwandishi, Mlawi, aliandika majina yao mbele ya mfalme, muamuzi, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa makuhani na familia za Walawi. Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari.
7 Y la primera suerte salió por Joiarib, la segunda por Jedei,
Kura ya kwanza ilienda kwa Yehoiaribu, ya pili kwa Yedaia,
8 La tercera por Harim, la cuarta por Seorim,
ya tatu kwa Harimu, ya nne kwa Seorimu,
9 La quinta por Melquías, la sexta por Maimán,
ya tano kwa Malikija, ya sita kwa Mijamini,
10 La séptima por Accos, la octava por Abías,
ya saba kwa Hakozi, ya nane kwa Abija,
11 La nona por Jesúa, la décima por Sequemias,
ya tisa kwa Yeshua, ya kumi kwa Shekania,
12 La undécima por Eliasib, la duodécima por Jacim,
ya kumi na moja kwa Eliashibu, ya kumi na mbili kwa Yakimu,
13 La trecena por Hopfa, la catorcena por Isbaab,
ya kumi na tatu kwa Hupa, ya kumi na nne kwa Yesheheabu,
14 La quincena por Belga, la dieziseisena por Emmer,
ya kumi na tano kwa Biliga, ya kumi na sita kwa Imma,
15 La decimaséptima por Hezir, la décimaoctava por Afses,
ya kumi na saba kwa Heziri, ya kumi na nane kwa Hapizezi,
16 La décimanona por Feceia, la vigésima por Hezeciel,
ya kumi na tisa kwa Pethaia, ya ishirini kwa Yehezikeli,
17 La veinte y una por Joaquim, la veinte y dos por Gamul,
ya ishirini na moja kwa Yakini, ya ishirini na mbili kwa Gamuli,
18 La veinte y tres por Dalaiau, la veinte y cuatro por Maaziau.
ya ishirini na tatu kwa Delaia, na ya ishirini na nne kwa Maazia.
19 Estos fueron contados en su ministerio, para que entrasen en la casa de Jehová conforme a su costumbre, debajo de la mano de Aarón su padre, de la manera que le había mandado Jehová el Dios de Israel.
Hii ilikuwa taratibu ya utumishi wao, walipo kuja kwenye nyumba ya Yahweh, wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao, kama Yahweh, Mungu wa Israeli, alivyo waagiza.
20 Y de los hijos de Leví que quedaron: De los hijos de Amram era Subael: y de los hijos de Subael, Jehedeias.
Hawa walikuwa Walawi waliobakia: Wana wa Amiramu, Shebueli; wana wa Shebaeli, Yedeia.
21 Y de los hijos de Rohobias, Jesías el principal.
Wana wa Rehabia: wana wa Rehabia, Ishia kiongozi.
22 De Isaari, Salemot: e hijo de Salemot fue Jahat.
Wa Waizari, Shelomothi; mwana wa Shelomothi, Yahathi.
23 Y su primer hijo fue Jeriau, el segundo Amarías, el tercero Jahaziel, el cuatro Jecmaam.
Wana wa Hebroni: Yeria kiongozi, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
24 Hijo de Oziel fue Mica, e hijo de Mica fue Samir.
Wana wa uzao wa Uzieli ulimjumuisha Mika. Uzao wa Mika ulimjumuisha Shamiri.
25 Hermano de Mica fue Jesía, e hijo de Jesía fue Zacarías.
Kaka wa Mika alikuwa Ishia. Wana wa Ishia akijumuishwa Zakaria.
26 Los hijos de Merari fueron Moholi, y Musi: hijo de Oziau fue Benno.
Wana na Merari: Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia, Beno.
27 Los hijos de Merari de Oziau fueron Benno y Soam, Zacur y Hebri,
Wana wa Merari: Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibrri.
28 Y Eleazar de Moholi, el cual no tuvo hijos.
Wana wa Mahili: eleazari, ambaye alikuwa hana wana.
29 Hijo de Cis fue Jerameel.
Wana wa Kishi: Yerameli
30 Los hijos de Musi fueron Moholi, Eder, y Jerimot. Estos fueron los hijos de los Levitas conforme a las casas de sus familias.
wana wa Mushi: Mahli, Eda, na yerimothi. Walikuwa walawi, walio orodheshwa na familia zao.
31 Estos también echaron suertes contra sus hermanos los hijos de Aarón delante del rey David, y de Sadoc, y de Aquimelec, y de los príncipes de las familias de los sacerdotes, y de los Levitas, el principal de los padres contra su hermano menor.
Wanaume hawa ambao walikuwa vichwa katika nyumba za baba zao na kila wadogo zao, walipiga kura katika uwepo wa Mfalme Daudi, na Zadoki na Ahimeleki, pamoja na viongozi wa familia wa makuhani na Walawi. Walirusha kura kama uzao wa Aroni walivyofanya.

< 1 Crónicas 24 >