< 1 Crónicas 2 >

1 Estos son los hijos de Israel: Rubén, Simeón, Leví, Judá, Isacar, Zabulón,
Hawa ndio wana wa Israeli: Reubeni, Simioni, Lawi, Yuda, Isakari, Zebuloni,
2 Dan, José, Ben-jamín, Neftalí, Gad, y Asser.
Dani, Yusufu, Benyamini, Naftali, Gadi, na Asheri.
3 Los hijos de Judá fueron Er, Onán, y Sela. Estos tres le nacieron de la hija de Sue Cananea. Y Er primogénito de Judá, fue malo delante de Jehová, y le mató.
Wana wa Yuda walikuwa Eri, Onani, na Shela, ambao walizaliwa na binti wa Shua, Wakanaani. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa muovu katika macho ya Yahweh, na Yahweh akamwua.
4 Y Tamar su nuera le parió a Fares, y a Zara; y así todos los hijos de Judá fueron cinco.
Tamari, mkwe wake, alimzalia Peresi na Zera. Yuda alikuwa na wana wa kiume wa tano.
5 Los hijos de Fares fueron Jesrón, y Hamul.
Wana wa Peresi walikuwa Hesroni na Hamuli.
6 Y los hijos de Zara fueron Zamrí, Etán, Hemán, Calcal, y Darda, todos cinco.
Wana wa Zera walikuwa Zimri, Ethani, Hemani, Kalikoli na Darda, wote kwa jumla ni watano.
7 Acán fue hijo de Carmi: este alborotó a Israel, porque prevaricó en el anatema.
Mwana wa Karmi alikuwa ni Akani, aliye leta taabu katika Israeli alipo iba kile kilicho hifadhiwa kwa ajili ya Mungu.
8 Azaría fue hijo de Etán.
Mwana wa Ethani alikuwa Azaria.
9 Los hijos que nacieron a Jesrón fueron Jerameel, Ram, y Calubai.
Wana wa Hezroni walikuwa ni Yerameeli, Ramu, na Kalebu.
10 Y Ram engendró a Aminadab: y Aminadab engendró a Nahasón príncipe de los hijos de Judá.
Ramu akawa baba wa Aminadabu, na Aminadabu akawa baba wa Nashoni, kiongozi miongoni uzao wa Yuda.
11 Y Nahasón engendró a Salma: y Salma engendró a Booz.
Nashoni akawa baba wa Salmoni, na Salmon akawa baba wa Boazi.
12 Y Booz engendró a Obed: y Obed engendró a Isaí.
Boazi akawa baba wa Obedi, na Obedi akawa baba wa Yese.
13 Y Isaí engendró a Eliab su primogénito, y el segundo Abinadab, el tercero Samaa,
Yese akawa baba wa mzaliwa wake wa kwanza Eliabu, wa pili Abinadabu, wa tatu Shama.
14 El cuarto Natanael, el quinto Radai,
Nethaneli wa nne, Radai wa tano.
15 El sexto Osem, el séptimo David:
Ozemu wa sita, na Daudi wa saba.
16 De los cuales Sarvia y Abigail fueron hermanas. Los hijos de Sarvia fueron tres, Abisaí, Joab, y Asael.
Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa Abishai, Yoabu, na Asaheli, jumla watatu.
17 Abigail engendró a Amasa, y su padre fue Jeter Ismaelita.
Abigali akamzaa Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri Mwishmaeli.
18 Caleb, hijo de Jesrón, engendró a Jeriot de su mujer Azuba. Y los hijos de ella fueron Jaser, Sobad, y Ardón.
Kalebu mwana wa Hesroni akawa baba wa watoto wa Azubu mkewe, na Yeriothi. Wanawe walikuwa Yesheri, Shobabu, na Ardoni.
19 Y muerta Azuba, Caleb, tomó por mujer a Efrata, la cual le parió a Jur.
Azuba akafa, na Kalebu akamuoa Efrathi, aliye mzalia Huri.
20 Y Jur engendró a Urí: y Urí engendró a Beseleel.
Huri akawa baba wa Uri, na Uri akawa baba wa Besaleli.
21 Después Jesrón entró a la hija de Maquir padre de Galaad, la cual tomó siendo él de sesenta años: y ella le parió a Segub.
Baadae Hesroni (alipo kuwa na miaka sitini) akamuoa binti wa Makiri, baba wa Gileadi. Akamzalia Segubu.
22 Y Segub engendró a Jair, este tuvo veinte y tres ciudades en la tierra de Galaad.
Segubu akawa baba wa Yairi, aliye miliki miji ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi.
23 Y Gessur y Aram tomaron las ciudades de Jair de ellos, y a Cenat, y sus aldeas, que fueron sesenta lugares. Todos estos fueron los hijos de Maquir padre de Galaad.
Geshuri na Aramu wakawapokonya miji ya Yairi na Kenathi, pamoja na miji sitini iliyo zunguka. Hawa wakazi wote walikuwa ni uzao wa Makiri, baba wa Gileadi.
24 Y muerto Jesrón en Caleb de Efrata, Abiá mujer de Jesrón le parió a Asur padre de Tecua.
Baada ya kifo cha Hesroni, Kalebu akalala na Efrata, mke wa baba yake Hesroni. Akamzalia Ashuri, baba wa Tekoa.
25 Y los hijos de Jerameel primogénito de Jesrón fueron Ram, su primogénito, Buna, Arán, Asom, y Aquía.
Wana wa Yerameeli, mzaliwa wa kwanza wa Hesroni, walikuwa ni Ramu mzaliwa wa kwanza, Buna, Oreni, Ozemu, na Ahiya.
26 Y tuvo Jerameel otra mujer llamada Atara, que fue madre de Onam.
Yerameeli alikuwa na mke mwingine, Jina lake lilikuwa Atara. Yeye alikuwa mama wa Onamu.
27 Y los hijos de Ram primogénito de Jerameel fueron Moos, Jamín, y Acar.
Wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, Yamini, na Ekeri.
28 Y los hijos de Onam fueron Semeí y Jada. Los hijos de Semeí: Nadab y Abisur.
Wana wa Onamu walikuwa ni Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa ni Nadabu na Abishuri.
29 Y el nombre de la mujer de Abisur fue Abijail, la cual le parió a Abán, y a Molid.
Jina la mke wa Abishuri lilikuwa Abihaili, na akamzalia Abani na Molidi.
30 Y los hijos de Nadab fueron Saled y Afaim: y Saled murió sin hijos.
Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa pasipo watoto.
31 Y Jesi fue hijo de Afaim: y Sesán fue hijo de Jesi: y Alai fue hijo de Sesán.
Mwana wa Apaimu alikuwa Ishi. Mwana wa Ishi alikuwa Sheshani. Mwana wa Sheshani alikuwa Alai.
32 Los hijos de Jada, hermano de Semeí, fueron Jeter, y Jonatán: y murió Jeter sin hijos.
Wana wa Yada, kaka yake Shamai, walikuwa Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa pasipo mtoto.
33 Y los hijos de Jonatán fueron Falet, y Ziza. Estos fueron los hijos de Jerameel.
Wana wa Yonathani walikuwa Pelethi na Zaza. Hawa ndio uzao wa Yerameeli.
34 Y Sesán no tuvo hijos, sino hijas.
Sasa Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, bali wa kike pekee. Sheshani alikuwa na mtumishi, wa Kimisri, ambaye jina lake lilikuwa Yariha.
35 Y tuvo Sesán un siervo Egipcio llamado Jeraa, al cual dio Sesán a su hija por mujer: y ella le parió a Etei.
Sheshani alimkabidhi binti yake kwa Yariha mtumishi wake kama mke wake. Akamzalia Atai.
36 Y Etei engendró a Natán: y Natán engendró a Zabad.
Atai akawa baba wa Nathani, na Nathani akawa baba wa Zabadi.
37 Y Zabad engendró a Oflal: y Oflal engendró a Obed.
Zabadi akawa baba wa Efalali, na Afalali akawa baba wa Obedi.
38 Y Obed engendró a Jehú: y Jehú engendró a Azarías.
Obedi akawa baba wa Yehu, na Yehu akawa baba wa Azaria.
39 Y Azarías engendró a Helles: y Helles engendró a Elasa.
Azaria akawa baba wa Helesi, na Helesi akawa baba wa Eleasa.
40 Elasa engendró a Sisamai: y Sisamai engendró a Sellum.
Eleasa akawa baba wa Sismai, na Sismai akawa baba wa Shalumu.
41 Y Sellum engendró a Icamia; e Icamia engendró a Elisama.
Shalumu akawa baba wa Yekamia, na Yekamia akawa baba wa Elishama.
42 Los hijos de Caleb hermano de Jerameel fueron, Mesa su primogénito; este es el padre de Zif; y de sus hijos Maresa, padre de Hebrón.
Wana wa Kalebu, kaka yake Yerameeli, walikuwa ni Mesha mzaliwa wake wa kwanza, aliye kuwa baba wa Zifu. Mwanae wa pili, Maresha, allikuwa baba wa Hebroni.
43 Y los hijos de Hebrón fueron Coré, y Tappua, y Recem, y Samma.
Wana wa Hebroni walikuwa Kora, Tapua, Rekemu, na Shema.
44 Y Samma engendró a Raham padre de Jercaam: y Recem engendró a Sammai.
Shema akawa baba wa Rahamu, baba wa Yorkeamu. Rekemu akawa baba wa Shamai.
45 Maón fue hijo de Sammai: y Maón padre de Bet-zur.
Mwana wa Shamai alikuwa Maoni, na Maoni alikuwa baba wa Bethsuri.
46 Y Efa concubina de Caleb le parió a Haram, y a Mosa, y a Gezez. Y Haram engendró a Gezez.
Efa, suria wa Kalebu, alimza Harani, Mosa, na Gazezi. Harani akawa baba wa Gazezi.
47 Y los hijos de Jahaddai fueron Regom, Joatam, Gesam, Falet, Efa, y Saaf.
Wana wa Yadai walikuwa Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa, na Shaafa.
48 Maaca concubina de Caleb le parió a Saber y a Tarana.
Maaka, suria wa Kalebu, alimza Sheberi na Tirhana.
49 Y también le parió a Saaf padre de Madmena, y a Sue padre de Macbena, y padre de Gabaa. Y Aca fue hija de Caleb.
Pia akamza Shaafu baba wa Madmana, Sheva baba wa Makbena na baba wa Gibea. Binti wa Kalebu alikuwa Aksa. Hawa walikuwa uzao wa Kalebu.
50 Estos fueron los hijos de Caleb, hijo de Jur, primogénito de Efrata: Sobal padre de Cariat-jarim,
Hawa walikuwa wana wa Huri, mzaliwa wake wa kwanza kwa Efratha: Shobali baba wa Kiriath-Yearimu.
51 Salma padre de Belén, Haref padre de Bet-gader.
Salma baba wa Bethlehemu, na Harefu baba wa Beth-gaderi.
52 Y los hijos de Sobal padre de Cariat-jarim, el cual veía la mitad de Hamenuot.
Shobali baba wa kiriath-Yearimu alikuwa na uzao: Haroe, nusu ya watu Wamenuthite,
53 Y las familias de Cariat-jarim fueron los Jetreos, y los Futeos, y los Samateos, y los Masereos; de los cuales salieron los Saratitas, y los Estaolitas.
na ukoo wa Kiriath-Yearimu: Waithri, Waputhi, Washumathi, na Wamishrai. Wasorathi na Waeshtaoli walitoka huku.
54 Los hijos de Salma: Belén y los Netofatitas, los cuales son las coronas de la casa de Joab, y de la mitad de los Manatitas, los Saraitas.
Ukoo wa Salma ulikuwa kama ufatao: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, na nusu ya Wamenuhothi na Wazori,
55 Y las familias de los escribas que moraban en Jabes, fueron los Tirateos, Simateos, Sucateos; los cuales son los Cineos, que vinieron de Hemat, padre de la casa de Recab.
ukoo wa waandishi walio ishi Yabesi: Watirathi, Washimeathi, na Wasukathi. Hawa walikuwa Wakeni walio toka katika uzao wa Hamathi, babu wa Warekabu.

< 1 Crónicas 2 >