< 1 Crónicas 11 >

1 Entonces todo Israel se juntó a David en Hebrón, diciendo: He aquí, nosotros somos tu hueso y tu carne:
Kisha Waisraeli wote walikuja Hebroni kwa Daudi na kusema, “Angalia, sisi ni nyama na mifupa yako.
2 Y demás de esto, ayer y anteayer, aun cuando Saul reinaba, tú sacabas y metías a Israel. También Jehová tu Dios te ha dicho: Tú apacentarás mi pueblo Israel, y tú serás príncipe sobre mi pueblo Israel.
Katika wakati uliopita, Sauli alipoo kuwa mfalme juu yetu, ni wewe uliye ongoza jeshi la Israeli. Yahweh Mungu wako alisema kwako, 'utawachunga watu wangu wa Isaraeli, na utakuwa mtawala wa watu wangu wa Israeli”'.
3 Y vinieron todos los ancianos de Israel al rey en Hebrón; y David hizo con ellos alianza en Hebrón delante de Jehová; y ellos ungieron a David por rey sobre Israel, conforme a la palabra de Jehová por mano de Samuel.
Kwaiyo wazee wote wa Israeli wakamjia mfalme huko Hebroni, na Daudi akafanya agano nao mbele ya Yahweh. Wakampaka mafuta Daudi kuwa mfalme wa Israeli. Kwa namna hii, neno la Yahweh lilo nenwa na Samweli likawa kweli.
4 Entonces David con todo Israel se fue a Jerusalem, la cual es Jebús, porque allí el Jebuseo era habitador de aquella tierra.
Daudi na Israeli yote wakaenda Yerusalemu (yani, Yebusi). Sasa Wayebusi, wakazi wa nchi, walikuwa pale.
5 Y los de Jebús dijeron a David: No entrarás acá. Mas David tomó la fortaleza de Sión, que es la ciudad de David.
Wakazi wa yebusi wakamwabia Daudi, “Hautakuja humu.” Lakini Daudi alichukuwa ngome ya Sayuni, mji wa Daudi.
6 Y David dijo: El que primero hiriere al Jebuseo, será cabeza y príncipe. Entonces subió Joab, hijo de Sarvia, el primero, y fue hecho príncipe.
Daudi alisema, “Yeyote atakaye washambulia Wayebusi wa kwanza atakuwa mkuu wa jeshi” kwaiyo Yoabu mwana wa Zeruia akashambulia wa kwanza, hivyo akafanywa mkuu wa jeshi.
7 Y David habitó en la fortaleza, y por esto la llamaron la ciudad de David.
Daudi akaanza kuishi katika hiyo ngome. Kwaiyo wakaiita mji wa Daudi.
8 Y edificó la ciudad al derredor desde Melo hasta la cerca: y Joab reparó el resto de la ciudad.
Akaimarisha mji kutoka Milo na hadi mpaka ukuta unao zunguka. Yoabu akaimairisha mji wote uliyo baki.
9 Y David se aumentaba, yendo creciendo, y Jehová de los ejércitos era con él.
Daudi akawa mkuu na mkuu kwa sababu Yahweh wa Majeshi alikuwa naye.
10 Estos son los capitanes de los valientes hombres que David tuvo, y los que le ayudaron en su reino, con todo Israel, para hacerle rey sobre Israel, conforme a la palabra de Jehová.
Hawa walikuwa viongozi Daudi aliyo kuwa nao, waliyo jionyesha imara katika ufalme wake, pamoja na Israeli, kumfanya mfalme, kutii neno la Yahweh kuhusu Israeli.
11 Y este es el número de los valientes que David tuvo: Jesbaán, hijo de Hacamoní, príncipe de los treinta, el cual blandió su lanza una vez contra trescientos, a los cuales mató.
Hii ni orodha ya wanajeshi shupavu wa Daudi. Yashobeami, mwana wa Mhakimoni, alikuwa mkuu wa kikosi cha thelathini. Aliwaua wanaume mia tatu na mkuki wake katika sehemu moja.
12 Tras este fue Eleasar, hijo de Dodo, Ahohita, el cual era entre los tres valientes.
Baada ya yeye alikuwa Eleazari mwana wa Dodo, Mahohi, aliyekuwa mmoja wa wanaume watatu hodari.
13 Este estaba con David en Fes-domim, estando allí juntos en batalla los Filisteos: y había allí una suerte de tierra llena de cebada, y huyendo el pueblo delante de los Filisteos,
Alikuwa na Daudi huko Pasidamimu, na pale Wafilisti wakakusanyika pamoja kwa mapambano, ambapo palikuwa na uwanja wa ngano na jeshi liliwakimbia Wafilisti.
14 Ellos se pusieron en medio de la haza, y la defendieron, y vencieron a los Filisteos; y salvó Jehová de gran salud.
Walisimama katikati ya uwanja. Wakautetea na kuwakata Wafilisti na Yahweh akawaokoa na ushindi mkubwa.
15 Ítem, tres de los treinta principales, descendieron a la peña a David, a la cueva de Odollam, estando el campo de los Filisteos en el valle de Rafaim.
Kisha watatu wa viongozi thelathini wakashuka chini kwenye mwamba wa Daudi, katika pango la Adulamu. Jeshi la Wafilisti walieka kambi katika bonde la Refaim.
16 Y David estaba entonces en la fortaleza, y el alojamiento de los Filisteos estaba en Belén.
Kwa wakati huo Daudi alikuwa katika ngome yake, pangoni, Wafilisti walikita kambi yao Bethilehemu.
17 Entonces David deseó, y dijo: ¡Oh quién me diese a beber de las aguas del pozo de Belén, que está a la puerta!
Daudi alikuwa na kiu ya maji na akasema, “Laiti mtu akanipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho Bethilehemu, kisima kilicho pembeni mwa lango!”
18 Entonces aquellos tres rompieron por el campo de los Filisteos, y sacaron agua del pozo de Belén, que está a la puerta: y tomaron, y trajéronla a David: mas él no la quiso beber, mas derramóla a Jehová, y dijo:
Hawa wanaume hodari watatu wakatoboa kupita jeshi la Wafilisti na kuchota maji kwenye kisima cha Bethilehemu, kisima pembeni mwa lango. Wakachukuwa maji na kumletea Daudi, lakini alikataa kunywa. Badala yake, akamwaga chini kwa Yahweh.
19 Guárdeme mi Dios de hacer esto: ¿había yo de beber la sangre de estos varones con sus vidas, que con el peligro de sus vidas la han traído? Y no la quiso beber. Esto hicieron aquellos tres valientes.
Kisha akasema, “Yahweh, iwe mbali na mimi, kwamba ni yanywe haya maji. Je ninywe damu ya wanaume walio hatarisha maisha yao?” Kwa sababu wameeka maisha ya hatarini, akakataa kunywa. Haya ni mambo wanaume hodari watatu walio fanya.
20 Ítem, Abisaí, hermano de Joab, era cabeza de los tres, el cual blandió su lanza sobre trescientos, a los cuales hirió: y en los tres fue nombrado.
Abishai kaka wa Yoabu, alikuwa kiongozi wa watatu. Alitumia mkuki wake dhidi ya watu mia tatu na kuwaua. Ametajwa pamoja na wale watatu.
21 Y fue el más ilustre de los tres, en los segundos; y fue príncipe de ellos: mas no llegó a los tres primeros.
Kati ya wale watatu, yeye alipewa heshima mara mbili na akawa kiongozi wao. Japo hakuwa mmoja wa miongoni mwao.
22 Banaías, hijo de Joiada, hijo de varón de esfuerzo, de grandes hechos, de Cabseel. Este venció los dos leones de Moab. El mismo descendió, e hirió un león en mitad de un foso en tiempo de nieve.
Benaia mwana wa Yehoiada alikuwa mwanaume mwenye nguvu aliye fanya mambo makuu. Aliua wana wawili wa Arieli wa Moabu. Pia alishuka chini ya shimo na kumuua simba wakati theluji ikianguka.
23 El mismo venció a un Egipcio, hombre de medida de cinco codos: y el Egipcio traía una lanza como un enjullo de tejedor: y él descendió a él con un bastón; y arrebató al Egipcio la lanza de la mano, y matóle con su misma lanza.
Alimua hadi Mmisri, mwanaume mwenye mita mbili na theluthi moja. Mmisri alikuwa na mkuki kama gongo la mshonaji, lakini alimfuata chini na fimbo tu. Akakamata mkuki katika mkono wa Mmisri na kumuua na mkuki wake.
24 Esto hizo Banaías, hijo de Joiada, y fue nombrado entre los tres valientes,
Benaia mwana wa Yehoiada alifanya haya matukio, na akatajwa miongoni mwa wale wanaume hodari watatu.
25 Y fue el más honrado de los treinta, mas no llegó a los tres. A este puso David en su consejo.
Alisifika zaidi ya wale wanajeshi thelathini kwa ujumla, lakini hakuwa pewa hadhi ya wale wanajeshi watatu hodari. Daudi alimueka kiongozi wa walinzi wake.
26 Y los valientes de los ejércitos fueron Asael, hermano de Joab, y Elcanán, hijo de Dodo, de Belén,
Wanaume hodari walikuwa Asaheli kaka wa Yoabu, Elhanani mwana wa Dodo wa Bethilehemu,
27 Samot Arotita, Helles Falonita,
Shamothi Mherori, Helezi Mpeloni,
28 Ira, hijo de Acces Tecuita, Abiezer Anatotita,
Ira mwana wa Ikeshi Mtekoi, Abi Eza Manathothi,
29 Sobocai Husatita, Ilai Ahohita,
Sibekai Mhushathite, Ilai Mahohite,
30 Maharai Netofatita, Heled, hijo de Baana Netofatita,
Maharai Mnetofathi, Heledi mwana wa Baana Mnetofathite,
31 Etai, hijo de Ribai, de Gabaat, de los hijos de Ben-jamín, Banaías Paratonita,
Itai mwana wa Ribai wa Gibea uzao wa Benjamini, Benaia Mpirathoni,
32 Hurai del río de Gaas, Abiel Arbatita,
Hurai wa mabonde ya Gaashi, Abieli Marbathi,
33 Azmot Bauramita, Eliaba Salabonita.
Azmavethi Mbaharumi, Eliaba Mshaalboni,
34 Los hijos de Assem Gezonita, Jonatán, hijo de Sage Ararita,
Mwana wa Hashemu Mgizoni, Yonathani mwana wa Shagee Mhararite,
35 Ahiam, hijo de Sacar Ararita, Elifal, hijo de Ur,
Ahiamu mwana wa Sacari Mhararite, Elifali mwana wa Uri,
36 Hefer Meceratita, Ahia Felonita,
Hefa Mmekarathi, Ahija Mpeloni,
37 Jesro Carmelita, Naharari, hijo de Azbai,
Hezro Mcarmeli, Maarai mwana wa Ezibai,
38 Joel hermano de Natán, Mibahar, hijo de Hagarai,
Yoeli kaka wa Nathani, Mibhari mwana wa Hagiri,
39 Selec Ammonita, Naharai Berotita, escudero de Joab, hijo de Sarvia,
Zeleki Mamoni, Naharai Mberothi ( mbeba ngao ya Yoabu mwana wa Zeruia),
40 Ira Jetreo, Gareb Jetreo,
Ira Mithire, Garebu Mithire,
41 Urías Jetteo, Zabad, hijo de Alai,
Uria Mhiti, Zabadi mwana wa Ahlai,
42 Adina, hijo de Siza Rubenita, príncipe de los Rubenitas, y con él treinta.
Adina mwana wa Shiza Mreubeni ( kiongozi wa Wareubeni) na thelathini pamoja nae,
43 Hanán, hijo de Maaca, y Josafat Matanita,
Hanani mwana wa Maaka, na Yoshafati Mmithini,
44 Ozías Astarotita, Samma, y Jehiel, hijo de Hotán Arorita,
Uzia Mashiterathi, Shama na Yeieli wana wa Hothamu Waaroeri,
45 Jedihiel, hijo de Samrí, y Joha su hermano Tosaita,
Jediaeli mwana wa Shimri, Joha ( kaka yake Mtize),
46 Eliel Mahumita, Jeribai, y Josaia, hijo de Elnaam, y Jetma Moabita,
Elieli Mmahavi, Yeribai na Yoshavia mwana wa Elnaamu, Ithima Mmoabi,
47 Eliel, y Obed, y Jasiel Mosobia.
Elieli, Obedi, na Yaasieli Wamezobai.

< 1 Crónicas 11 >