< Luka 10 >

1 Po tem pa izvoli Gospod še drugih sedemdeset, in pošlje jih po dva in dva pred obličjem svojim v vsako mesto in kraj, kamor je imel sam priti.
Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
2 In pravil jim je: Žetve je sicer mnogo, ali delalcev malo; prosite torej gospodarja žetve, naj pošlje delalcev na žetev svojo.
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
3 Pojdite; glej, jaz vas pošiljam kakor jagnjeta sredi volkov.
Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
4 Ne nosite mošnje, ne torbe, ne obutala; in nikogar na poti ne pozdravljajte.
Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
5 V kterokoli pa hišo vnidete, naprej recite: Mir tej hiši!
Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
6 In če bo tu sin mirú, ostal bo mir vaš na njem; če pa ne vrnil se bo k vam.
Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
7 A v tej hiši prebivajte, in jejte in pijte, kar imajo; kajti vreden je delalec plačila svojega. Ne prehajajte iz hiše v hišo.
Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
8 In v kterokoli mesto pridete, in vas sprejmó, jejte, kar vam postavijo,
Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
9 In uzdravljajte bolnike, kteri so v njej, in pravite jim: Približalo se je k vam kraljestvo Božje.
Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
10 A v kterokoli mesto pridete, in vas ne sprejmó, izidite na ulice njegove in recite:
Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
11 Tudi prah, ki se nas je v mestu vašem prijel, otresamo vam; ali vedite to, da se je približalo k vam kraljestvo Božje.
Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
12 Pravim vam pa, da bo Sodomljanom tisti dan laže, nego temu mestu.
Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
13 Gorjé ti, Korazin! gorjé ti, Betsajda! kajti ko bi se bili v Tiru in Sidonu zgodili čudeži, kteri so se zgodili v vama, bila bi se davno, v žaklji in pepelu sedeč, spokorila.
“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
14 Ali Tiru in Sidonu bo laže na sodbi, nego vama.
Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
15 In ti, Kapernaum, ki si se do neba povzdignil, zagnan boš do pekla. (Hadēs g86)
Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu.” (Hadēs g86)
16 Kdor posluša vas, posluša mene; in kdor se odreka vas, odreka se mene: a kdor se mene odreka, odreka se tega, kdor me je poslal.
Halafu akasema, “Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma.”
17 Vrnejo pa se sedemdeseteri z radostjo, govoreč: Gospod, tudi hudiči so nam pokorni v imenu tvojem.
Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, “Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako.”
18 Pa jim reče: Videl sem satana, da je padel z neba kakor blisk.
Yeye akawaambia, “Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
19 Glej, dajem vam oblast stopati na kače in škorpijone, in vso silo vražjo: in nič vam ne bo škodovalo.
Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
20 Ali temu se ne radujte, da so vam hudiči pokorni; radujte se pa marveč, da so imena vaša zapisana na nebesih.
Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 V ta čas se oveselí Jezus v duhu, in reče: Zahvaljujem ti, oče, Gospodar neba in zemlje! da si to prikril modrim in razumnim, in si je razodel nedoraslim; dà, oče: ker tako je bila volja tvoja.
Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, “Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.”
22 Vse mi je izročil oče moj; in nikdor ne vé, kdo je sin, razen oče, in kdo je oče, razen sin, in komurkoli če sin razodeti.
Kisha akasema, “Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo.”
23 In obrnivši se k učencem posebej, reče: Blagor očém, ktere vidijo, kar vi vidite,
Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, “Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
24 Kajti pravim vam, da je veliko prerokov in kraljev želelo videti, kar vi vidite, in niso videli; in slišati, kar vi slišite, in niso slišali.
Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie.”
25 In glej, učenik postave vstane, in izkušajoč ga, reče: Učenik, kaj naj storim, da zadobóm večno življenje? (aiōnios g166)
Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
26 On mu pa reče: V zakonu kaj je pisano? kako bereš?
Yesu akamwuliza, “Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?”
27 On pa odgovarjajoč, reče: "Ljubi Gospoda Boga svojega iz vsega srca svojega, in iz vse duše svoje, in iz vse močí svoje, in iz vse pameti svoje;" in: "a bližnjega svojega kakor samega sebe."
Akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
28 Pa mu reče: Prav si odgovoril; to delaj, in živel boš.
Yesu akawaambia, “Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi.”
29 On pa, hoteč samega sebe opravičiti, reče Jezusu: Kdo pa je bližnji moj?
Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
30 Odgovarjajoč pa Jezus, reče: En človek je šel iz Jeruzalema v Jeriho in je med razbojnike padel, kteri so, ko so ga bili slekli in ranili, odšli, pustivši ga na pol mrtvega.
Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
31 Po naključbi pa je šel neki duhoven po tej poti, in videvši ga prejde mimo.
Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
32 Enako pa tudi Levit, ko je bil na tem mestu, pride, in videvši ga, prejde mimo.
Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
33 Neki Samarijan pa, kteri je šel po poti, pride do njega; in ko ga ugleda, zasmili mu se.
Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
34 In pristopivši, obveže mu rane, in vlije olja in vina; in posadivši ga na svoje kljuse, pripelje ga v gostilnico, in poskrbi za-nj.
Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
35 Drugi dan pa, ko je odhajal, vzeme dva srebrnika iz mošnje, in dá krčmarju, in reče mu: Skrbi za-nj; in karkoli več boš potrošil, povrnil ti bom jaz, kedar se vrnem.
Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi.”
36 Kdo torej od teh tréh ti se zdí, da je bil bližnji temu, ki je padel med razbojnike?
Kisha Yesu akauliza, “Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?”
37 On pa reče: Ta, kteri se ga je usmilil. Reče mu torej: Pojdi, tudi ti delaj enako.
Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, “Ni yule aliyemwonea huruma.” Yesu akamwambia, “Nenda ukafanye vivyo hivyo.”
38 Zgodí se pa, ko so šli, pa vnide on v eno vas; a neka žena po imenu Marta sprejme ga v hišo svojo.
Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
39 In ta je imela sestro, ktera se je imenovala Marija, ktera je tudi sedeč pri nogah Jezusovih poslušala besedo njegovo.
Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
40 A Marta si je dajala veliko opraviti s postrežbo; ter pristopi, in reče: Gospod, kaj ti ni mar, da me je sestra moja samo pustila, naj strežem? Reci jej torej, naj mi pomore.
Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, “Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie.”
41 Odgovarjajoč pa, reče jej Jezus: Marta! Marta! skrbiš in trudiš se za mnogo;
Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
42 Ali le eno je potrebno. A Marija je dobri del izvolila, kteri jej se ne bo odvzel.
Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya.”

< Luka 10 >