< Luka 1 >

1 Ko so mnogi jeli opisovati rečí, ktere so popolnoma gotove med nami,
Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
2 Kakor so nam izročili, kteri so od začetka sami videli in so služabniki besede bili:
kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
3 Namenil sem tudi jaz, ki sem vse od začetka na tanko pozvedel, po vrsti pisati tebi, častiti Teofil!
Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
4 Da spoznaš gotovost rečî, kterih si se naučil.
Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
5 Bil je v dnéh Heroda kralja Judejskega neki duhoven po imenu Zaharija, od reda Abijevega; in žena njegova od hčeri Aronovih, in ime jej je bilo Elizabeta.
Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
6 Bila sta pa oba pravična pred Bogom, in živela sta po vseh zapovedih in ustavah Gospodovih brez madeža.
Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
7 In nista imela otrók, ker je bila Elizabeta nerodovitna, in oba sta se bila uže postarala.
Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
8 Zgodí se pa, ko je po vrsti reda svojega služil pred Bogom,
Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
9 Po navadi duhovstva zadene ga opravilo, naj vnide v tempelj Gospodov, da pokadí.
Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
10 In vsa množiča ljudstva je bila zunej, in molila je v čas kajenja.
Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
11 Prikaže pa mu se angelj Gospodov, stoječ na desnej strani kadilnega oltarja.
Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
12 In Zaharija se ustraši, ko ga ugleda, in groza ga obide.
Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
13 Angelj mu pa reče: Ne boj se, Zaharija! kajti uslišana je molitev tvoja, in žena tvoja Elizabeta ti bo rodila sina, in imenuj ime njegovo Janez.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
14 In bo ti na radost in na veselje, in veliko se jih bo rojstvu njegovemu radovalo.
Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
15 Kajti velik bo pred Gospodom; in vina in močne pijače ne bo pil, in napolnil se bo Duha svetega še v telesu matere svoje.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 In veliko sinov Izraelskih bo obrnil h Gospodu Bogu njih.
Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
17 In on pojde pred njim z duhom in močjó Elijevo, da obrne srca očetov k otrokom, in nevernike k razumnosti pravičnih: da pripravi Gospodu ljudstvo gotovo.
Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
18 Pa reče Zaharija angelju: Po čem bom poznal to? kajti jaz sem star, in žena moja se je postarala.
Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
19 In odgovarjajoč angelj, reče mu: Jaz sem Gabrijel, ki stojim pred Bogom, in poslan sem, naj s teboj govorim, in ti to veselje oznanim.
Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
20 In glej, mutast boš in ne boš mogel govoriti do dné, ko se bo to zgodilo; ker nisi veroval besedam mojim, ktere se bodo izpolnile o svojem času.
Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
21 In čakalo je ljudstvo Zaharija; in čudili so se, da se tako dolgo mudí v tempeljnu.
Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
22 Ko pa izide, ni jim mogel govoriti? in spoznajo, da je videl prikazen v tempeljnu: in on jim je pomigaval, in ostal je mutast.
Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
23 In zgodí se, ko se izpolnijo dnevi službe njegove, odide na dom svoj.
Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
24 A po teh dnéh je Elizabeta žena njegova spočela, in skrivala se je pet mesecev, govoreč:
Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
25 Tako mi je storil Gospod v dnéh, ko se je ozrl na me, da odvzeme oponos moj med ljudmí.
“Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
26 A šesti mesec pošlje Bog angelja Gabrijela v mesto Galilejsko, kteremu je ime Nazaret,
Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
27 K devici zaročenej možu, kteremu je bilo ime Jožef, iz hiše Davidove; in devici je bilo ime Marija.
kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
28 In angelj vnide k njej, in reče: Zdrava, z milostjo obdarovana! Gospod je s teboj; blagoslovljena si ti med ženami.
Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
29 Ona pa, ko ga ugleda, prestraši se od besede njegove, in premišljevala je, kakošen bi bil ta pozdrav.
Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
30 Pa jej angelj reče; Ne boj se, Marija! našla si namreč milost pri Bogu.
Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
31 In glej, spočela boš v telesu, in rodila boš sina, in imenuj ime njegovo Jezus.
Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
32 Ta bo velik, in imenoval se bo sin najvišega; in dal mu bo Gospod Bog prestol Davida očeta njegovega,
Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 In kraljeval bo v hiši Jakobovej vekomaj, in kraljestvu njegovemu ne bo konca. (aiōn g165)
Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn g165)
34 Marija pa reče angelju: Kako bo to, ko moža ne poznam?
Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
35 In odgovarjajoč angelj, reče jej; Sveti Duh bo prišel na te, in moč najvišega te bo obsenčila; za to se bo sveto, ktero se bo rodilo iz tebe, imenovalo sin Božji.
Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
36 In glej, Elizabeta teta tvoja, tudi ona je spočela sina v starosti svojej; in ta mesec jej je šesti, njej, ki jo imenujejo nerodovitno:
Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
37 Ker ne bo nobene besede pri Bogu, ktera se ne bi mogla izpolniti.
Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
38 Marija pa reče: Glej, dekla sem Gospodova; zgôdi mi se po besedi tvojej. In angelj odide od nje.
Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
39 Vstavši pa Marija v té dni, odide jadrno na gorenjo stran v mesto Judovo.
Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
40 In vnide v hišo Zaharijevo, in pozdravi Elizabeto.
Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
41 In zgodí se, ko sliši Elizabeta pozdrav Marijin, zaigra dete v telesu njenem; in Elizabeta se napolni Duha svetega,
Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
42 In zavpije z močnim glasom, in reče: Blagoslovljena si ti med ženami, in blagoslovljen je sad telesa tvojega.
Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
43 In odkod meni to, da je prišla mati Gospoda mojega k meni?
Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
44 Kajti glej, ko je prišel glas pozdrava tvojega v ušesa moja, zaigralo je dete radostno v telesu mojem.
Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
45 In blagor jej, ktera je verovala; kajti zgodilo se bo, kar jej je rekel Gospod.
Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
46 Pa reče Marija: Duša moja poveličuje Gospoda,
Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
47 In duh moj se je oveselil v Bogu, zveličarji mojem:
na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
48 Da se je ozrl na ponižanje dekle svoje. Kajti glej, odslej me bodo blagrovali vsi rodovi:
Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
49 Ker mi je storil velike rečí on, ki je mogočen, in ime njegovo sveto;
Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
50 In usmiljenje njegovo od roda do roda tistim, kteri se ga bojé.
Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
51 Pokazal je moč z roko svojo: razkropil je ošabne v mislih srca njih;
Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
52 Vrgel je mogočne s prestola, in povišal je ponižne.
Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
53 Lačne je napolnil z blagom, in bogate je odpravil prazne.
Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 Sprejel je Izraela hlapca svojega, da se spomene usmiljenja svojega.
Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
55 (Kakor je govoril očetom našim, ) Abrahamu in semenu njegovemu na vekomaj. (aiōn g165)
(kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn g165)
56 Prebila je pa Marija ž njo kake tri mesece; in vrne se na dom svoj.
Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
57 A Elizabeti se izpolni čas, da porodí, in rodí sina.
Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
58 In sosedje in sorodniki njeni zaslišijo, da je pokazal Gospod veliko usmiljenje svoje na njej; in radovali so se ž njo.
Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
59 In zgodí se osmi dan, da pridejo deteta obrezovat; in klicali so ga po imenu očeta njegovega, Zaharija.
Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
60 Ali odgovarjajoč mati njegova, reče: Ne, nego imenoval se bo Janez.
Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
61 In rekó jej: Nikogar ni v rodovini tvojej, da bi mu bilo tako ime.
Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
62 In pomigavali so očetu njegovemu, kako hoče, da bi ga imenovali.
Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
63 In izprosivši tablico, napiše, govoreč: Janez mu je ime. In vsi se začudijo.
Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
64 In odprla so se usta njegova pri tej priči in jezik njegov, in govoril je, hvaleč Boga.
Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
65 In strah obide vse njih sosede; in po vsej gorenjej Judeji se razglasé vse te reči.
Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
66 In vsi, kteri jih slišijo, položé jih v srce svoje, govoreč: Kaj neki bo iz tega otroka? In roka Gospodova je bila ž njim.
Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 In Zaharija oče njegov se napolni Duha svetega, in prerokuje, govoreč:
Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
68 Blagoslovljen Gospod Bog Izraelov, da je obiskal in odrešil ljudstvo svoje;
“Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
69 In nam povzdignil rog zveličanja v hiši Davida hlapca svojega,
Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
70 (Kakor je govoril z ustmi svetih prerokov svojih, ki so bili od nekedaj: ) (aiōn g165)
kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn g165)
71 Da nas bo rešil sovražnikov naših in iz rok vseh, kteri nas mrzé:
Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 Da storí usmiljenje očetom našim, in se spomene svete zaveze svoje,
Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
73 Prisege, ktero je prisegel Abrahamu očetu našemu, da nam bo dal,
kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
74 Da mu, rešeni iz rok sovražnikov svojih, brez straha služimo,
Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
75 V svetosti in pravičnosti pred njim vse svoje žive dní.
katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
76 In ti, otrok, imenoval se boš prerok najvišega; kajti šel boš pred obličjem Gospodovim, da mu pripraviš pot;
Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
77 In daš razum zveličanja ljudstvu njegovemu za odpuščanje njih grehov,
kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
78 Po prisrčnem usmiljenji Boga našega, po kterem nas je obiskal vzhod z vižave:
Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
79 Da obsije tiste, kteri sedé v temi in smrtnej senci; da naravná noge naše na pot mirú.
kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
80 A dete je rastlo in se krepčalo v duhu; in bilo je v puščavah do dné, ko se pokaže Izraelu.
Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.

< Luka 1 >