< Kološanom 3 >

1 Če ste bili torej vred zbujeni s Kristusom, iščite, kar je gori, kjer sedí Kristus na desnici Božji.
Basi, ikiwa mmefufuka pamoja na Kristo, panieni mambo ya juu, kule Kristo aliko, ameketi upande wa kulia wa Mungu.
2 V mislih imejte, kar je gori, ne kar je na zemlji;
Muwe na hamu ya mambo ya huko juu, na siyo mambo ya hapa duniani.
3 Kajti umrli ste, in življenje vaše je skrito s Kristusom v Bogu;
Maana ninyi mmekufa na uzima wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
4 Kader se prikaže Kristus, življenje naše, tedaj se prikažete tudi vi v slavi z njim.
Uzima wenu halisi ni Kristo, na wakati atakapotokea ndipo nanyi pia mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
5 Morite torej ude svoje zemeljske, kurbarijo, nečistost, strast, hudo poželenje in lakomnost, katera je malikovanje;
Basi, komesheni kabisa kila kitu kilicho ndani yenu ambacho chahusika na mambo ya kidunia: uasherati, uchafu, shauku, tamaa mbaya na uchu (ambao ni sawa na kuabudu sanamu).
6 Po čemer prihaja jeza Božja nad nepokorščine sinove,
Kwa sababu ya mambo hayo hasira ya Mungu huwajia wote wanaomwasi.
7 Med katerimi ste tudi vi živeli nekdaj, ko ste bivali med njimi;
Wakati mmoja ninyi pia mliishi kufuatana na mambo hayo, mlipotawaliwa nayo.
8 Sedaj pa odložite tudi vi vse, jezo, srd, hudobnost, obrekovanje, nesramno besedovanje iz svojih ust.
Lakini sasa mnapaswa kuachana na mambo haya yote: hasira, tamaa, uovu; kufuru au maneno yasiyofaa yasitoke kamwe vinywani mwenu.
9 Ne lagajte med seboj, slecite starega človeka z dejanji njegovimi,
Msiambiane uongo, kwani ninyi mmekwisha vua ule utu wa kale pamoja na matendo yake yote,
10 In oblecite novega, ponovljenega v spoznanje po podobi njega, ki ga je vstvaril;
mkavaa utu mpya. Huu unaendelea kurekebishwa na Mungu, Muumba wake, kadiri ya mfano wake, ili mpate kumjua Mungu kwa ukamilifu.
11 Kjer ni Grka in Juda, obreze in neobreze, tujca, Scita, hlapca, svobodnjaka; nego vse in v vseh Kristus.
Katika hali hii, hakuna tena tofauti kati ya Mgiriki na Myahudi, aliyetahiriwa na asiyetahiriwa, msomi na asiye msomi, mtumwa na mtu aliye huru. Kristo ni kila kitu, na yumo katika yote.
12 Oblecite torej, ker ste izvoljeni in ljubljeni sveti Božji, milosrčnost, blagovoljnost, ponižnost, krotkost, potrpežljivost;
Ninyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
13 Da se prenašate med seboj, in si odpuščate, če ima kdo tožbo do koga, kakor je tudi Kristus odpustil vam, tako tudi vi;
Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe ninyi.
14 Poleg vsega tega pa ljubezen, katera je popolnosti vez.
Zaidi ya hayo yote, zingatieni upendo kwani upendo huunganisha kila kitu katika umoja ulio kamili.
15 In mir Božji naj vlada v srcih vaših, v katerega ste bili tudi poklicani v enem telesu; in hvaležni bodite!
Nayo amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu; maana kwa ajili hiyo ninyi mmeitwa katika mwili huo mmoja. Tena muwe na shukrani!
16 Beseda Kristusova prebivaj v vas obilo, v vsej modrosti; učite in opominjajte se med seboj s psalmi in hvalospevi in pesmami duhovnimi, v milosti pójte v srci svojem Gospodu.
Ujumbe wa Kristo ukae ndani yenu pamoja na utajiri wake wote. Fundishaneni na kushauriana kwa hekima yote. Imbeni zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Mungu mioyoni mwenu kwa shukrani.
17 In vse, kar počenjate v besedi in dejanji, vse v imenu Gospoda Jezusa, zahvaljujoč se Bogu in očetu po njem.
Na, kila mfanyacho kwa neno au tendo, fanyeni vyote kwa jina la Bwana Yesu na kumshukuru Mungu Baba kwa njia yake.
18 Žene, bodite pokorne svojim možem, kakor se spobodi v Gospodu.
Enyi akina mama, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana.
19 Možje, ljubite žene svoje in ne hudujte se nad njimi.
Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao.
20 Otroci, bodite poslušni roditeljem v vsem, kajti to je po volji Gospodu.
Enyi watoto, watiini wazazi wenu daima maana hiyo humpendeza Bwana.
21 Očetje, ne dražite otrók svojih, da ne bodo malosrčni.
Nanyi wazazi, msiwachukize watoto wenu, la sivyo watakata tamaa.
22 Hlapci, bodite poslušni v vsem gospodom po mesu, ne po okoslužnosti kakor ljudem ugajajoč, nego v preprostosti srca, boječ se Boga.
Enyi watumwa, watiini wakuu wenu wa kidunia katika mambo yote, na si tu wakati wanapowatazama kwa kuwa mnataka kujipendekeza kwao; ila fanyeni hivyo kwa moyo wote, kwa sababu ya kumcha Bwana.
23 In vse kar storite, delajte iz duše, kakor Gospodu, in ne ljudém;
Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wote, kwa sababu ya Bwana na si kwa ajili ya mtu.
24 Vedóč, da od Kristusa dobóte zato povračilo dedščine; kajti Gospodu Kristusu hlapčujete;
Kumbukeni kwamba atawapeni tuzo lile alilowawekea watu wake. Mtumikieni Kristo Bwana!
25 Krivični pa bode prejel, kar je krivičnega storil; in ni ga licegledja.
Atendaye mabaya atalipwa kufuatana na ubaya wake; Mungu hana ubaguzi.

< Kološanom 3 >