< Rimljanom 9 >

1 Govorim resnico v Kristusu, ne lažem, prav tako mi moja vest pričuje v Svetem Duhu,
Nasema ukweli mtupu; nimeungana na Kristo nami sisemi uongo. Dhamiri yangu ikiongozwa na Roho Mtakatifu inanithibitishia jambo hili pia.
2 da imam v svojem srcu veliko potrtost in nenehno bridkost.
Nataka kusema hivi: nina huzuni kubwa na maumivu yasiyopimika moyoni mwangu
3 Kajti lahko bi si želel, da bi bil jaz sam preklet pred Kristusom za svoje brate, moje sorodnike glede na meso;
kwa ajili ya watu wangu, walio damu moja nami! Kama ingekuwa kwa faida yao, ningekuwa radhi kulaaniwa na kutengwa na Kristo.
4 ki so Izraelci, ki jim pripada posvojitev in slava in zaveze in dajanje postave in bogoslužje in obljube;
Hao ndio watu wa Israeli ambao Mungu aliwateua wawe watoto wake, akawashirikisha utukufu wake; aliagana nao, akawapa Sheria yake, imani ya kweli na ahadi zake.
5 katerih so očetje in iz katerih je, glede na meso, prišel Kristus, ki je čez vse, Bog, blagoslovljen na veke. Amen. (aiōn g165)
Wao ni wajukuu wa mababu, naye Kristo, kadiri ya ubinadamu wake, ametoka katika ukoo wao. Mungu atawalaye juu ya yote, na atukuzwe milele! Amina. (aiōn g165)
6 Ne, kakor da Božja beseda ne učinkuje. Kajti niso vsi Izraelci, ki so iz Izraela;
Sisemi kwamba ahadi ya Mungu imebatilika; maana si watu wote wa Israeli ni wateule wa Mungu.
7 niti zato, ker so Abrahamovi potomci, niso vsi otroci, temveč: ›Po Izaku se bo imenovalo tvoje seme.‹
Wala, si wazawa wote wa Abrahamu ni watoto wake wa kweli. Ila, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Wazao wake watatokana na Isaka.”
8 To se pravi: »Tisti, ki so meseni otroci, tisti niso Božji otroci, temveč so za potomstvo šteti otroci obljube.«
Nido kusema, wale waliozaliwa kimaumbile ndio watoto wa Mungu, bali wale waliozaliwa kutokana na ahadi ya Mungu ndio watakaoitwa watoto wake.
9 Kajti to je beseda obljube: ›Ob tem času bom prišel in Sara bo imela sina.‹
Maana ahadi yenyewe ni hii: “Nitakujia wakati maalum, naye Sara atapata mtoto.”
10 Pa ne samo to; temveč, ko je tudi Rebeka spočela po enem, celó po našem očetu Izaku
Tena si hayo tu ila pia Rebeka naye alipata mapacha kwa baba mmoja, yaani Isaka, babu yetu.
11 (kajti otroka se še nista rodila niti nista naredila ničesar dobrega ali zlega, da lahko ostane Božji namen glede na izvolitev, ne iz del, temveč iz njega, ki kliče),
Lakini, ili Mungu aonekane kwamba anao uhuru wa kuchagua, hata kabla wale ndugu hawajazaliwa na kabla hawajaweza kupambanua jema na baya,
12 ji je bilo rečeno: ›Starejši bo služil mlajšemu.‹
Rebeka aliambiwa kwamba yule mtoto wa kwanza atamtumikia yule wa nyuma. Hivyo uchaguzi wa Mungu unategemea jinsi anavyoita mwenyewe, na si matendo ya binadamu.
13 Kakor je pisano: ›Jakoba sem ljubil, toda Ezava sem sovražil.‹
Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia.”
14 Kaj bomo torej rekli? Ali je pri Bogu nepravičnost? Bog ne daj.
Basi, tuseme nini? Je, Mungu amekosa haki? Hata kidogo!
15 Kajti Mojzesu je rekel: ›Usmilil se bom, kogar se hočem usmiliti in sočutje bom imel, do kogar hočem imeti sočutje.‹
Maana alimwambia Mose: “Nitamhurumia mtu yeyote ninayetaka kumhurumia; nitamwonea huruma mtu yeyote ninayetaka.”
16 Torej potem to ni od tistega, ki hoče niti od tistega, ki teče, temveč od Boga, ki izkazuje usmiljenje.
Kwa hiyo, yote hutegemea huruma ya Mungu, na si bidii au mapenzi ya mtu.
17 Kajti pismo pravi faraonu: ›Celo za ta isti namen sem te dvignil, da lahko na tebi pokažem svojo moč in da se bo moje ime lahko razglasilo po vsej celotni zemlji.‹
Maana Maandiko Matakatifu yasema hivi kwa Farao: “Nilikufanya mfalme ili kwa njia yako, uwezo wangu ujulikane, na jina langu litangazwe popote duniani.”
18 Torej se usmili, kogar se hoče usmiliti in kogar hoče, tega zakrkne.
Ni wazi, basi, kwamba Mungu humhurumia yeyote anayetaka kumhurumia, na akipenda kumfanya mtu awe mkaidi, hufanya hivyo.
19 Torej mi boš rekel: »Zakaj še najde krivdo? Kajti kdo se je uprl njegovi volji?«
Labda utaniuliza: “Ikiwa mambo yako hivyo, Mungu anawezaje kumlaumu mtu? Nani awezaye kuyapinga mapenzi yake?”
20 Ne, vendar, oh človek, kdo si ti, ki nasprotuješ Bogu? Ali bo oblikovana stvar rekla tistemu, ki jo je ustvaril: »Zakaj si me naredil takšno?«
Lakini, ewe binadamu, u nani hata uthubutu kumhoji Mungu? Je, chungu chaweza kumwuliza mfinyanzi wake: “Kwa nini umenitengeneza namna hii?”
21 Mar nima lončar moči nad ilom, da iz iste grude naredi eno posodo v čast, drugo pa v nečast?
Mfinyanzi anaweza kuutumia udongo apendavyo na kufinyanga vyungu viwili kwa udongo uleule; kimoja kwa matumizi ya heshima, na kingine kwa matumizi ya kawaida.
22 Kaj pa, če je Bog, voljan pokazati svoj bes in pokazati svojo moč, z veliko potrpežljivosti prenašal posode besa, primerne za uničenje,
Hivyo ndivyo ilivyo kwa Mungu. Alitaka kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha uwezo wake, Basi, alikuwa na saburi sana, akiwavumilia wale ambao walikuwa lengo la ghadhabu yake, ambao walistahili kuangamizwa.
23 in da bi lahko dal spoznati bogastva svoje slave na posodah usmiljenja, ki jih je vnaprej pripravil za slavo,
Alitaka pia kudhihirisha wingi wa utukufu wake ambao alitumiminia sisi tulio lengo la huruma yake; sisi ambao alikwisha kututayarisha kuupokea utukufu wake.
24 celó nas, ki nas je poklical, ne samo izmed Judov, temveč tudi izmed poganov?
Maana sisi ndio hao aliowaita, si tu kutoka miongoni mwa Wayahudi bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.
25 Kakor tudi pravi v Ozeju: ›Ljudi, ki niso bili moji, bom imenoval moji ljudje; in njo, ki ni bila ljubljena, ljubljeno.‹
Maana ndivyo asemavyo katika kitabu cha Hosea: “Wale waliokuwa Si watu wangu nitawaita: Watu wangu! Naye Sikupendi ataitwa: Mpenzi wangu!
26 In zgodilo se bo, da na kraju, kjer jim je bilo rečeno: ›Vi niste moji ljudje, ‹ tam bodo imenovani otroci živega Boga.
Na pale walipoambiwa: Ninyi si wangu hapo wataitwa: Watoto wa Mungu hai.”
27 Tudi Izaija kliče glede Izraela: ›Četudi bo število Izraelovih otrok kakor morskega peska, bo rešen ostanek; ‹
Naye nabii Isaya, kuhusu Israeli anapaaza sauti: “Hata kama watoto wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaookolewa;
28 kajti dokončal bo delo in ga nenadoma prekinil v pravičnosti; ker bo Gospod na zemlji hitro opravil svoje delo.
maana, Bwana ataitekeleza upesi hukumu yake kamili juu ya ulimwengu wote.”
29 In kakor je prej rekel Izaija: ›Razen če nam Gospod nad vojskami ne bi pustil semena, bi bili kakor Sódoma in bi posnemali Gomóro.‹
Ni kama Isaya alivyosema hapo awali: “Kama Bwana Mwenye Nguvu asingalituachia baadhi ya watoto wa Israeli, tungalikwisha kuwa kama Sodoma, tungalikwisha kuwa ma Gomora.”
30 Kaj bomo potem rekli? Da so se pogani, ki si niso prizadevali za pravičnost, dokopali do pravičnosti, celó pravičnosti, ki je iz vere.
Basi, tuseme nini? Ni hivi: watu wa mataifa ambao hawakutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu, wamekubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani,
31 Toda Izrael, ki si je prizadeval za postavo pravičnosti, se ni dokopal do postave pravičnosti.
hali watu wa Israeli waliokuwa wakitafuta Sheria iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu, hawakuipata.
32 Zakaj? Ker tega niso iskali po veri, temveč kakor bi bilo to po delih postave. Kajti spotaknili so se ob tisti kamen spotike,
Kwa nini? Kwa sababu walitegemea matendo yao badala ya kutegemea imani. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa
33 kakor je pisano: ›Glej, na Sionu položim kamen spotike in skalo pohujšanja; in kdorkoli veruje vanj, ne bo osramočen.‹
kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: “Tazama! Naweka huko Sioni jiwe likwazalo, mwamba utakaowafanya watu waanguke. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa!”

< Rimljanom 9 >