< Luka 9 >

1 Potem je sklical skupaj svoje dvanajstere učence in jim dal moč in oblast nad vsemi hudiči in za ozdravljanje bolezni.
Yesu kisha akawaita wale kumi na wawili pamoja, akawapa mamlaka na uwezo wa kutoa pepo wachafu wote na kuponya magonjwa yote,
2 In poslal jih je, da oznanjajo Božje kraljestvo in da ozdravljajo bolne.
kisha akawatuma waende wakahubiri Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.
3 Rekel jim je: »Za svoje potovanje ne vzemite ničesar, niti palic, prav tako ne malhe, niti kruha, niti denarja, niti ne imejte vsak po dva plašča.
Akawaagiza akisema, “Msichukue chochote safarini: sio fimbo, wala mkoba, wala mkate, wala fedha, hata msichukue kanzu ya ziada.
4 In v katerokoli hišo vstopite, tam ostanite in od tam odidite.
Katika nyumba yoyote mwingiayo, kaeni humo hadi mtakapoondoka katika mji huo.
5 Kdorkoli vas ne bo sprejel, kadar greste iz tega mesta, si iz svojih stopal otresite prav [ta] prah, v pričevanje proti njim.«
Kama watu wasipowakaribisha, mnapoondoka katika mji wao, kungʼuteni mavumbi kutoka kwenye miguu yenu ili kuwa ushuhuda dhidi yao.”
6 In odpravili so se in šli skozi mesta in oznanjali evangelij in povsod ozdravljali.
Hivyo wale wanafunzi wakaondoka wakaenda kutoka kijiji hadi kijiji, wakihubiri habari njema na kuponya wagonjwa kila mahali.
7 Torej Herod, vladar četrtinskega dela province, je slišal o vsem, kar je bilo storjeno po njem; in bil je zmeden, zato ker so nekateri rekli, da je bil Janez obujen od mrtvih,
Basi Mfalme Herode, mtawala wa Galilaya, alisikia habari za yote yaliyotendeka. Naye akafadhaika, kwa kuwa baadhi ya watu walikuwa wakisema Yohana Mbatizaji amefufuliwa kutoka kwa wafu.
8 in od nekaterih, da se je pojavil Elija in od drugih, da je vstal eden izmed starih prerokov.
Wengine wakasema Eliya amewatokea, na wengine wakasema kwamba mmoja wa manabii wa kale amefufuka.
9 Herod pa je rekel: »Janeza sem jaz obglavil, toda kdo je ta, o katerem slišim takšne stvari?« In želel si je, da bi ga videl.
Herode akasema, “Yohana nilimkata kichwa. Lakini ni nani huyu ambaye ninasikia mambo kama haya kumhusu?” Akatamani sana kumwona.
10 In apostoli, ko so se vrnili, so mu povedali vse, kar so storili. In vzel jih je in odšel stran, na samo, v zapuščen kraj, ki je pripadal mestu z imenom Betsajda.
Mitume wake waliporudi, wakamweleza Yesu yote waliyofanya. Akawachukua, akaenda nao faraghani mpaka mji uitwao Bethsaida.
11 Ko je množica to izvedela, mu je sledila in sprejel jih je ter jim govoril o Božjem kraljestvu in ozdravil te, ki so imeli potrebo po ozdravljenju.
Lakini umati wa watu ukafahamu alikokwenda, ukamfuata. Akawakaribisha na kunena nao kuhusu Ufalme wa Mungu na kuwaponya wale wote waliokuwa wanahitaji uponyaji.
12 In ko je dan začel minevati, potem so prišli dvanajsteri ter mu rekli: »Pošlji množico proč, da lahko gredo v mesta in naokoli po deželi ter prenočijo in si preskrbijo živeža, kajti tukaj smo na samotnem kraju.«
Ilipokaribia jioni, wale mitume kumi na wawili wakaenda kwa Yesu na kumwambia, “Waage makutano ili waende vijijini jirani na mashambani, ili wapate chakula na mahali pa kulala, kwa maana hapa tuko nyikani.”
13 Toda rekel jim je: »Vi jim dajte jesti.« Oni pa so rekli: »Nimamo več kot pet hlebov in dve ribi, razen, če bi šli in za vse te ljudi kupili hrano.«
Yesu akawajibu, “Ninyi wapeni chakula.” Nao wakajibu, “Hatuna zaidi ya mikate mitano na samaki wawili. Labda twende tukanunue chakula cha kuwatosha watu hawa wote.”
14 Kajti bilo jih je okoli pet tisoč mož. In svojim učencem je rekel: »Primorajte jih, da se usedejo v skupine po petdeset.«
Walikuwako wanaume wapatao 5,000. Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Waketisheni katika makundi ya watu hamsini hamsini.”
15 In storili so tako in vse so primorali sesti.
Wanafunzi wakafanya hivyo, wakawaketisha wote.
16 Tedaj je vzel pet hlebov in dve ribi in jih, zroč k nebu, blagoslovil in razlomil in dal učencem, da jih postavijo pred množico.
Yesu akaichukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni, akavibariki na kuvimega. Kisha akawapa wanafunzi ili wawagawie watu.
17 In jedli so in vsi so bili nasičeni. In od odlomkov, ki so jim ostali, je bilo nabranih dvanajst košar.
Wote wakala, wakashiba. Nao wanafunzi wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza vikapu kumi na viwili.
18 In pripetilo se je, ko je bil sam in molil, [da] so bili z njim njegovi učenci. In vprašal jih je, rekoč: »Kdo pravi množica, da sem jaz?«
Wakati mmoja, Yesu alipokuwa akiomba faraghani, nao wanafunzi wake wakiwa pamoja naye, akawauliza, “Watu husema mimi ni nani?”
19 Rekli so in odgovorili: »›Janez Krstnik, ‹ toda nekateri pravijo: ›Elija‹ in drugi pravijo, da je vstal eden izmed starih prerokov.«
Wakamjibu, “Baadhi husema wewe ni Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya, na bado wengine husema kwamba ni mmoja wa manabii wa kale amefufuka kutoka kwa wafu.”
20 Rekel jim je: »Toda kdo vi pravite, da sem jaz?« Peter mu reče in odgovori: »Kristus od Boga.«
Kisha akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” Petro akajibu, “Wewe ndiwe Kristo wa Mungu.”
21 In strogo jim je naročil in jim ukazal, da te besede ne povedo nobenemu človeku,
Yesu akawakataza wasimwambie mtu yeyote jambo hilo.
22 rekoč: »Sin človekov mora pretrpeti mnoge stvari in biti zavrnjen od starešin in visokih duhovnikov in pisarjev in umorjen bo in tretji dan bo obujen.«
Yesu akasema, “Imempasa Mwana wa Adamu kupata mateso mengi na kukataliwa na wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na itampasa auawe, lakini siku ya tatu kufufuliwa kutoka mauti.”
23 Njim vsem pa je rekel: »Če hoče katerikoli človek priti za menoj, naj se odpove samemu sebi in vsak dan vzame svoj križ ter mi sledi.
Kisha akawaambia wote, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake kila siku, anifuate.
24 Kajti kdorkoli hoče rešiti svoje življenje, ga bo izgubil, toda kdorkoli hoče izgubiti svoje življenje zaradi mene, ta isti ga bo rešil.
Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayaokoa.
25 Kajti kaj človeku koristi, če si pridobi ves svet, pa izgubi samega sebe ali je zavržen?
Je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akapoteza au kuangamiza nafsi yake?
26 Kajti kdorkoli se bo sramoval mene in mojih besed, njega se bo sramoval Sin človekov, ko bo prišel v svoji lastni slavi in v [slavi] svojega Očeta in svetih angelov.
Mtu yeyote akinionea aibu mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu naye atamwonea aibu atakapokuja katika utukufu wake na katika utukufu wa Baba, pamoja na malaika watakatifu.
27 Toda povem vam po resnici, tam bo nekaj tukaj navzočih, ki ne bodo okusili smrti, dokler ne bodo videli Božjega kraljestva.«
Amin, nawaambia, wako baadhi ya watu waliosimama hapa ambao hawataonja mauti kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu.”
28 In pripetilo se je okoli osmega dne po teh govorih, da je vzel Petra in Janeza in Jakoba ter odšel gor na goro, da moli.
Yapata siku nane baada ya Yesu kusema hayo, aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana, akaenda nao mlimani kuomba.
29 In medtem ko je molil, je bil videz njegovega obličja predrugačen in njegova oblačila so bila bela in sijoča.
Alipokuwa akiomba, sura ya uso wake ikabadilika, nayo mavazi yake yakametameta kama mwanga wa umeme wa radi.
30 In glej, z njim sta govorila dva moža, ki sta bila Mojzes in Elija.
Ghafula wakawaona watu wawili, ndio Mose na Eliya, wakizungumza naye.
31 Prikazala sta se v slavi in govorila o njegovem odhodu, ki naj bi ga dovršil v Jeruzalemu.
Walionekana katika utukufu wakizungumza na Yesu kuhusu kifo chake ambacho kingetokea huko Yerusalemu.
32 Toda Peter in ta dva, ki sta bila z njim, so bili obteženi s spanjem. Ko so se zbudili, so videli njegovo slavo in dva moža, ki sta stala z njim.
Petro na wenzake walikuwa wamelala usingizi mzito. Walipoamka, wakaona utukufu wa Yesu na wale watu wawili waliokuwa wamesimama pamoja naye.
33 In pripetilo se je, ko sta odšla od njega, da je Peter rekel Jezusu: »Učitelj, dobro je za nas, da smo tukaj. Naredimo tri šotore: enega zate in enega za Mojzesa in enega za Elija, « pa ni vedel, kaj je govoril.
Mose na Eliya walipokuwa wanaondoka, Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vizuri tukae hapa! Tutajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.” Lakini Petro alikuwa hajui asemacho.
34 Medtem ko je tako govoril, je prišel oblak in jih zasenčil in ko so vstopili v oblak, so se prestrašili.
Alipokuwa bado anazungumza, pakatokea wingu, likawafunika, nao wakaogopa walipoingia mle kwenye wingu.
35 In iz oblaka je prišel glas, rekoč: »Ta je moj ljubljeni Sin, njega poslušajte.«
Sauti ikatoka kwenye lile wingu ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa, niliyemchagua. Msikieni yeye.”
36 In ko je glas minil, se je Jezus znašel sam. Oni pa so [to] obdržali zase in v tistih dneh nobenemu človeku niso povedali o teh stvareh, ki so jih videli.
Baada ya sauti hiyo kusema, walimkuta Yesu akiwa peke yake. Wale wanafunzi wakalihifadhi jambo hili, wala kwa wakati huo hawakumwambia mtu yeyote yale waliyokuwa wameyaona.
37 In pripetilo se je, da ga je naslednji dan, ko so prišli dol s hriba, srečalo mnogo ljudi.
Kesho yake waliposhuka kutoka mlimani, alikutana na umati mkubwa wa watu.
38 In glej, mož iz skupine je zavpil, rekoč: »Učitelj, rotim te, poglej na mojega sina, kajti on je moj edini otrok.
Mtu mmoja katika ule umati wa watu akapaza sauti, akasema, “Mwalimu, naomba umwangalie mwanangu, kwani ndiye mtoto wangu wa pekee.
39 In glej, duh ga napada in nenadoma vpije in trga ga, da se ponovno peni in ko ga močno udari, odide od njega.
Mara kwa mara pepo mchafu humpagaa na kumfanya apige kelele, kisha humwangusha na kumtia kifafa hata akatokwa na povu kinywani. Huyo pepo mchafu anamtesa sana, na hamwachi ila mara chache.
40 In rotil sem tvoje učence, da ga izženejo iz njega, pa niso mogli.«
Niliwaomba wanafunzi wako wamtoe huyo pepo mchafu, lakini hawakuweza.”
41 Jezus pa odgovori in reče: »O neverni in sprevrženi rod, kako dolgo bom še z vami in vas prenašal? Privedi svojega sina sèm.«
Yesu akawajibu, “Enyi kizazi kisichoamini na kilichopotoka! Nitakaa nanyi na kuwavumilia mpaka lini? Mlete mwanao hapa.”
42 In ko je šele prihajal, ga je hudič vrgel dol ter ga trgal. In Jezus je oštel nečistega duha in ozdravil otroka ter ga ponovno izročil njegovemu očetu.
Hata yule mtoto alipokuwa akija, yule pepo mchafu akamwangusha, akamtia kifafa. Lakini Yesu akamkemea yule pepo mchafu amtoke, akamponya yule mtoto, na akamrudisha kwa baba yake.
43 In vsi so bili osupli nad mogočno Božjo močjo. Toda medtem ko so se vsi čudili ob vseh stvareh, ki jih je Jezus storil, je svojim učencem rekel:
Watu wote wakastaajabia uweza mkuu wa Mungu. Wakati bado watu walikuwa wanastaajabia hayo yote aliyokuwa akiyafanya Yesu, yeye akawaambia wanafunzi wake:
44 »Naj te besede prodrejo v vaša ušesa, kajti Sin človekov bo izročen v človeške roke.«
“Sikilizeni kwa makini haya nitakayowaambia sasa: Mwana wa Adamu atasalitiwa na kutiwa mikononi mwa watu.”
45 Toda tega govora niso razumeli in ta je bil skrit pred njimi, da ga niso zaznali in bali so se ga vprašati o tem govoru.
Lakini wao hawakuelewa alimaanisha nini. Maana ya maneno hayo ilifichika kwao, hivyo hawakuyaelewa, nao wakaogopa kumuuliza maana yake.
46 Potem je med njimi nastalo razmišljanje, kdo izmed njih naj bi bil največji.
Kukazuka mabishano miongoni mwa wanafunzi kuhusu ni nani miongoni mwao atakayekuwa mkuu kuliko wote.
47 In Jezus, zaznavajoč misel njihovega srca, je vzel otroka ter ga postavil poleg sebe
Lakini Yesu akayatambua mawazo yao, naye akamchukua mtoto mdogo, akamsimamisha kando yake.
48 ter jim rekel: »Kdorkoli bo tega otroka sprejel v mojem imenu, sprejema mene in kdorkoli bo sprejel mene, sprejema tistega, ki me je poslal, kajti kdor je najmanjši med vami vsemi, ta isti bo velik.«
Kisha akawaambia, “Yeyote amkaribishaye mtoto huyu mdogo kwa Jina langu, anikaribisha mimi, na yeyote atakayenikaribisha mimi, atakuwa amemkaribisha yeye aliyenituma. Kwa maana yeye aliye mdogo miongoni mwenu, ndiye aliye mkuu kuliko wote.”
49 In Janez je odgovoril ter rekel: »Učitelj, nekoga smo videli v tvojem imenu izganjati hudiče in smo mu prepovedali, ker ne hodi skupaj z nami.«
Yohana akasema, “Bwana, tumemwona mtu akitoa pepo wachafu kwa jina lako, nasi tukamzuia, kwa sababu yeye si mmoja wetu.”
50 Toda Jezus mu je rekel: »Ne prepovejte mu, kajti kdor ni proti nam, je za nas.«
Yesu akasema, “Msimzuie, kwa sababu yeyote ambaye si kinyume nanyi, yu upande wenu.”
51 In pripetilo se je, ko je prišel čas, da naj bi bil sprejet gor, se je on neomajno odločil, da gre v Jeruzalem
Wakati ulipokaribia wa yeye kuchukuliwa mbinguni, alikaza uso wake kwenda Yerusalemu.
52 in pred svojim obrazom je poslal poslance in ti so šli ter vstopili v vas Samarijanov, da pripravijo zanj.
Akatuma watu wamtangulie, nao wakaenda katika kijiji kimoja cha Samaria kumwandalia kila kitu;
53 Oni pa ga niso sprejeli, ker je bil njegov obraz, kakor da hoče iti v Jeruzalem.
lakini watu wa kijiji kile hawakumkaribisha kwa sababu alikuwa anakwenda zake Yerusalemu.
54 In ko sta njegova učenca, Jakob in Janez, to videla, sta rekla: »Gospod, hočeš, da ukaževa ognju, da pride dol z neba in jih pogoltne, kakor je storil Elija?«
Wanafunzi wake, yaani Yakobo na Yohana, walipoona hayo, wakasema: “Bwana, unataka tuagize moto kutoka mbinguni ili uwaangamize?”
55 Toda on se je obrnil in ju oštel ter rekel: »Vidva ne vesta, iz kakšne vrste duha sta.
Yesu akageuka na kuwakemea,
56 Kajti Sin človekov ni prišel, da pokonča človeška življenja, temveč, da jih reši.« In odšli so v drugo vas.
nao wakaenda kijiji kingine.
57 In pripetilo se je, ko so šli po poti, da mu je nek človek rekel: »Gospod, sledil ti bom, kamorkoli greš.«
Walipokuwa njiani wakienda, mtu mmoja akamwambia Yesu, “Nitakufuata kokote uendako.”
58 In Jezus mu je rekel: »Lisice imajo luknje in ptice neba imajo gnezda, toda Sin človekov nima kam nasloniti svoje glave.«
Yesu akamjibu, “Mbweha wana mapango, nao ndege wa angani wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa kulaza kichwa chake.”
59 In drugemu je rekel: »Sledi mi.« Vendar je ta rekel: »Gospod, dovoli mi najprej, da grem in pokopljem svojega očeta.«
Yesu akamwambia mtu mwingine, “Nifuate.” Mtu huyo akamjibu, “Bwana, niruhusu kwanza nikamzike baba yangu.”
60 Jezus mu je rekel: »Naj mrtvi pokopljejo svoje mrtve, ti pa pojdi in oznanjaj Božje kraljestvo.«
Yesu akamwambia, “Waache wafu wawazike wafu wao, bali wewe nenda ukautangaze Ufalme wa Mungu.”
61 Prav tako je rekel drugi: »Gospod, sledil ti bom, toda naj grem najprej in se poslovim od teh, ki so doma v moji hiši.«
Mtu mwingine akamwambia, “Bwana, nitakufuata lakini naomba kwanza nikawaage jamaa yangu.”
62 In Jezus mu je rekel: »Nihče, ki svojo roko položi na plug in gleda nazaj, ni primeren za Božje kraljestvo.«
Yesu akamwambia, “Mtu yeyote atiaye mkono wake kulima, kisha akatazama nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu.”

< Luka 9 >