< Luka 5 >

1 In pripetilo se je, medtem ko je množica pritiskala nanj, da sliši Božjo besedo, [da] je stal ob Genezareškem jezeru
Basi ilitokea wakati watu walipomkusanyikia na kumzunguka Yesu na kusikiliza neno la Mungu, ambapo alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti.
2 in zagledal dve ladji, pripravljeni pri jezeru, toda ribiči so odšli iz njiju ter izpirali svoje mreže.
Aliona mashua mbili zimetia nanga pembeni mwa ziwa. Wavuvi walikuwa wametoka na walikuwa wakiosha nyavu zao.
3 In vstopil je v eno izmed ladij, ki je bila Simonova in ga prosil, da bi odrinil malce proč od kopnega. In usedel se je ter iz ladje učil množico.
Yesu akaingia katika mojawapo ya zile mashua, ambayo ilikuwa ya Simoni na kumwomba aipeleke majini mbali kidogo na nchi kavu. Kisha akakaa na kufundisha kutokea kwenye mashua.
4 Torej, ko je prenehal govoriti, je rekel Simonu: »Kreni na globoko in spusti dol svoje mreže za vleko.«
kuongea, akamwambia Simoni, “Ipeleke mashua yako mpaka kwenye kilindi cha maji nakushusha nyavu zako ili kuvua samaki.”
5 Simon pa mu odgovori in reče: »Učitelj, celó noč smo garali, pa nismo nič ujeli. Vendar bom na tvojo besedo to mrežo spustil dol.«
Simon akajibu na kusema, Bwana, tumefanya kazi usiku wote, na hatukukamata chochote, lakini kwa neno lako, nitazishusha nyavu.
6 In ko so to storili, so zajeli veliko množino rib in njihova mreža se je pretrgala.
Walipofanya hivyo walikusanya kiasi kikubwa cha samaki na nyavu zao zikaanza kukatika.
7 In dali so znamenje svojim družabnikom, ki so bili na drugi ladji, da naj pridejo ter jim pomagajo. In prišli so ter napolnili obe ladji, tako da sta se začeli potapljati.
Hivyo wakawaashiria washirika wao kwenye mashua nyingine ili waja na kuwasaidia. Walikuja wakazijaza mashua zote, kiasi kwamba zikaanza kuzama.
8 Ko je Simon Peter to videl, je pri Jezusovih kolenih padel dol, rekoč: »Odidi od mene, oh Gospod, kajti grešen človek sem.«
Lakini Simoni Petro, alipoona hivyo, alianguka magotini pa Yesu akisema,”Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi Bwana.”
9 Kajti nad ulovom rib, ki so jih zajeli, je bil osupel on in vsi ti, ki so bili z njim;
Kwa sababu alishangazwa, na wote waliokuwa pamoja naye, kwa uvuvi wa samaki waliokuwa wameufanya.
10 in tako sta bila tudi Jakob in Janez, Zebedejeva sinova, ki sta bila Simonova družabnika. In Jezus je Simonu rekel: »Ne boj se, odslej boš lovil ljudi.«
Hili liliwajumuisha Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo, ambao walikuwa washirika wa Simoni. Na Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, kwa sababu kuanzia sasa na kuendelea utavua watu.”
11 In ko so svoji ladji pripeljali do kopnega, so vse zapustili in mu sledili.
Walipokwishazileta mashua zao nchi kavu, waliacha kila kitu na kumfuata yeye.
12 In pripetilo se je, ko je bil v nekem mestu, [da] zagleda človeka polnega gobavosti. Ko je [le-ta] zagledal Jezusa, je padel na svoj obraz ter ga rotil, rekoč: »Gospod, če hočeš, me lahko očistiš.«
Ilitokea kwamba alipokuwa katika mji mmojawapo, mtu aliyekuwa amejaa ukoma alikuwa huko. Wakati alipomuona Yesu, alianguka akiinamisha uso kwake mpaka chini na kumuomba, akisema, “Bwana, ikiwa unataka, waweza kunitakasa.”
13 In iztegnil je svojo roko ter se ga dotaknil, rekoč: »Hočem, bodi čist.« In gobavost je takoj odšla od njega.
Kisha Yesu alinyoosha mkono wake na kumgusa, akisema, “Nataka. Takasika.” Na saa ileile ukoma ukamwacha.
14 In naročil mu je, da ne pove nobenemu človeku: »Temveč pojdi in se pokaži duhovniku ter daruj za svoje očiščenje glede na Mojzesovo zapoved, njim v pričevanje.«
“Alimwagiza asimwambie mtu yeyote, lakini alimwambia, “Nenda zako, na ukajionyeshe kwa makuhani na utoe sadaka ya utakaso wako, sawasawa na kile Musa alichokiamuru, kwa ushuhuda kwao.”
15 Toda beseda o njem je toliko bolj na veliko šla naokoli in velike množice so prišle skupaj, da poslušajo in da bi bile po njem ozdravljene svojih slabotnosti.
Lakini habari kumuhusu yeye zikaenea mbali zaidi, na umati mkubwa wa watu ukaja pamoja kumsikiliza akifundisha na kuponywa magonjwa yao.
16 On pa se je umaknil v divjino in molil.
Lakini mara kwa mara alijitenga faraghani na kuomba.
17 In pripetilo se je na določeni dan, medtem ko je učil, da so bili tam, sedeči poleg, farizeji in učeni možje postave, ki so prišli iz vsakega mesta Galileje, Judeje in Jeruzalema. In Gospodova moč je bila prisotna, da jih ozdravi.
Ilitokea siku moja kati ya hizo siku alikuwa akifundisha, na walikuwapo Mafarisayo na waalimu wa sheria wamekaa hapo ambao walikuja wakitokea vijiji vingi tofauti katika mkoa wa Galilaya na Yudea, na pia kutokea katika mji wa Yerusalemu. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kuponya.
18 In glej, možje so prinesli na postelji človeka, ki je bil prevzet s paralizo in iskali so načine, da ga prinesejo noter in da ga položijo predenj.
watu kadhaa walikuja, wamembeba kwenye mkeka mtu aliyepooza, na wakatafuta njia ya kumwingiza ndani ili kumlaza chini mbele ya Yesu.
19 Ko pa zaradi množice niso mogli najti, po kateri poti bi ga lahko prinesli noter, so odšli na hišno streho in ga z njegovim ležiščem vred spustili navzdol skozi strešno kritino v sredo pred Jezusa.
Hawakupata njia ya kumwingiza ndani kwa sababu ya umati, hivyo walipanda juu ya paa la nyumba na kumshusha yule mtu chini kupitia kwenye vigae, juu mkeka wake katikati ya watu, mbele kabisa ya Yesu.
20 In ko je videl njihovo vero, mu je rekel: »Človek, tvoji grehi so ti odpuščeni.«
Akiangalia imani yao, Yesu alisema, “Rafiki, dhambi zako umesamehewa.”
21 In pisarji in farizeji so začeli premišljevati, rekoč: »Kdo je ta, ki govori bogokletja? Kdo lahko odpušča grehe razen samo Bog?«
Waandishi na Mafarisayo waliaanza kuhoji hilo, wakisema, “Huyu ni nani anayeongea makufuru? Ni nani anaweza kusamehe dhambi ila Mungu pekee yake?”
22 Toda ko je Jezus zaznal njihove misli, jim je odgovoril in rekel: »Kaj razmišljate v svojih srcih?
Lakini Yesu, akitambua nini walichokuwa wakifikiri, aliwajibu na kuwaambia, “Kwa nini mnaulizana hili mioyoni mwenu?
23 Ali je lažje reči: ›Tvoji grehi naj ti bodo odpuščeni‹ ali reči: ›Dvigni se in hôdi?‹
Kipi ni rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama utembee?'
24 Toda da boste lahko vedeli, da ima Sin človekov na zemlji oblast odpuščati grehe, « (je rekel bolnemu zaradi paralize) »jaz ti pravim: ›Vstani in vzemi svoje ležišče in pojdi v svojo hišo.‹«
Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani ya kusamehe dhambi, Nakwambia wewe, 'Amka, chukua mkeka wako na uende nyumbani kwako.'”
25 In ta je pred njimi takoj vstal ter pobral to, na čemer je ležal in odšel k svoji lastni hiši, proslavljajoč Boga.
Wakati huo huo akaamka mbele yao na akachukua mkeka wake aliokuwa ameulalia. Kisha akariudi nyumbani kwake akimtukuza Mungu.
26 In vsi so bili osupli in slavili Boga in izpolnjeni so bili s strahom, rekoč: »Danes smo videli čudne stvari.«
Kila mmoja alishangazwa na wakamtukuza Mungu. Walijawa na hofu, wakisema, “Tumeona mambo yasiyo ya kawaida leo.”
27 Po teh stvareh pa je odšel dalje in zagledal davkarja, imenovanega Levi, ki je sedel pri kraju plačevanja davkov in mu rekel: »Sledi mi.«
Baada ya mambo haya kutokea, Yesu alitoka huko na akamwona mtoza ushuru aliyeitwa Lawi amekaa eneo la kukusanyia kodi. Akamwambia, “Nifuate.”
28 In ta je pustil vse, vstal ter mu sledil.
Hivyo Lawi akanyanyuka na kumfuata, akiacha kila kitu nyuma.
29 In Levi mu je v svoji lastni hiši pripravil veliko praznovanje; in bila je velika skupina davkarjev in drugih, ki so se z njimi usedli.
Kisha Lawi akaandaa nyumbani kwake karamu kubwa kwa ajili ya Yesu. Walikuwapo watozaushuru wengi kule na watu wengi walioketi mezani wakila pamoja nao.
30 Toda njihovi pisarji in farizeji so godrnjali zoper njegove učence, rekoč: »Zakaj jeste in pijete z davkarji in grešniki?«
Lakini Mafarisayo na waandishi wao walikuwa wakiwanung'unikia wanafunzi, wakisema, “Kwa nini mnakula na kunywa na watoza ushuru pamoja na watu wengine wenye dhambi?”
31 In Jezus jim odgovori ter reče: »Tisti, ki so zdravi, ne potrebujejo zdravnika, temveč tisti, ki so bolni.
Yesu akawajibu, “Watu walio katika afya njema hawahitaji tabibu, ni wale tu wanaoumwa ndiyo watakao mhitaji mmoja.
32 Nisem prišel klicat pravičnih, temveč grešnike h kesanju.«
Sikuja kuwaita watu wenye haki haki wapate kutubu, bali kuwaita wenye dhambi wapate kutubu.”
33 In rekli so mu: »Zakaj se Janezovi učenci pogosto postijo in opravljajo molitve in enako učenci farizejev, tvoji pa jedo in pijejo?«
Wakamwambia, “Wanafunzi wa Yohana mara nyingi hufunga na kuomba, na wanafunzi wa Mafarisayo nao hufanya vivyo hivyo. Lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”
34 Rekel jim je: »Ali lahko primorate otroke svatovske sobe, da se postijo, medtem ko je z njimi ženin?
Yesu akawaambia, “Inawezekana mtu yeyote akawafanya waliohudhuria harusi ya Bwana Arusi kufunga wakati Bwana Arusi bado yu pamoja nao?
35 Toda prišli bodo dnevi, ko bo ženin odvzet od njih in tedaj, v tistih dneh, se bodo postili.«
Lakini siku zitakuja wakati Bwana Arusi atakapoondolewa kwao, ndipo katika siku hizo watafunga.”
36 In povedal jim je tudi prispodobo: »Nihče ne polaga koščka iz nove obleke na staro; če drugače, potem nov dela raztrganino in tudi košček, ki je bil odvzet iz nove, se ne ujema s staro.
Kisha Yesu aliongea pia kwao kwa mfano. “Hakuna anayechana kipande cha nguo kutoka kwenye vazi jipya na kukitumia kurekebisha vazi la zamani. Kama akifanya hivyo, ataichana nguo mpya, na kipande cha nguo kutoka vazi jipya kisengefaa kutumika na nguo ya vazi la zamani.
37 In novega vina nihče ne vliva v stare mehove, sicer bo novo vino mehove razgnalo in bo izlito in mehovi bodo propadli.
pia, hakuna mtu ambaye huweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai mpya ingepasua kile chombo, na divai ingemwagika, na viriba vingeharibika.
38 Toda novo vino mora biti vlito v nove mehove in oboje je ohranjeno.
Lakini divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
39 Prav tako nihče, ki je pil staro vino, noče nemudoma novega, kajti pravi: ›Staro je boljše.‹«
Na hakuna mtu baada ya kunywa divai ya zamani, hutataka mpya, kwa sababu husema, 'Ya zamani ni bora.”'

< Luka 5 >