< Luka 19 >

1 In Jezus je vstopil [v Jeriho] in šel skozi Jeriho.
Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2 In glej, tam je bil mož, imenovan Zahej, ki je bil šef med davkarji in je bil bogat.
Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3 In prizadeval si je, da bi videl, kdo je bil Jezus, pa ni mogel zaradi množice, ker je bil majhne postave.
Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4 In stekel je naprej ter splezal na egiptovsko smokvo, da bi ga videl, kajti moral bi iti mimo po tej poti.
Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5 Ko je Jezus prišel na ta kraj, je pogledal gor, ga zagledal in mu rekel: »Zahej, podvizaj se in pridi dol, kajti danes moram ostati v tvoji hiši.«
Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
6 In ta je pohitel in prišel dol ter ga radostno sprejel.
Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7 In ko so to videli, so vsi godrnjali, rekoč: »Ta je odšel, da bi bil gost pri človeku, ki je grešnik.«
Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
8 Zahej pa je vstal in rekel Gospodu: »Glej, Gospod, polovico svojih dobrin dam revnim in če sem po krivem obtožen, da sem karkoli vzel od kateregakoli človeka, mu štirikratno povrnem.«
Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
9 Jezus pa mu je rekel: »Ta dan je prišla k tej hiši rešitev duše, glede na to, da je tudi on Abrahamov sin.
Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10 Kajti Sin človekov je prišel, da poišče in da reši to, kar je bilo izgubljeno.«
Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
11 In medtem ko so slišali te stvari, je dodal in povedal prispodobo, kajti bil je blizu Jeruzalema in ker so mislili, da naj bi se Božje kraljestvo prikazalo takoj.
Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12 Rekel je torej: »Neki visoki plemič je odšel v daljno deželo, da prejme zase kraljestvo in da se vrne.
Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13 In poklical je svojih deset služabnikov ter jim razdelil deset funtov in jim rekel: ›Zaposlite se s trgovanjem, dokler ne pridem.‹
Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14 Toda njegovi državljani so ga sovražili in za njim poslali sporočilo, rekoč: ›Nočemo, da bi ta človek zavladal nad nami.‹
Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15 Pripetilo pa se je, ko se je vrnil, da je prejel kraljestvo. Potem je ukazal, naj te služabnike, ki jim je dal denar, pokličejo k njemu, da lahko izve, koliko je vsak človek pridobil s trgovanjem.
“Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16 Potem je prišel prvi, rekoč: ›Gospodar, tvoj funt je pridobil deset funtov.‹
Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17 Rekel mu je: ›V redu, ti dobri služabnik, ker si bil zvest v zelo majhnem, imej oblast nad desetimi mesti.‹
Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18 In prišel je drugi, rekoč: ›Gospod, tvoj funt je pridobil pet funtov.‹
Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19 In tudi njemu je rekel podobno: ›Tudi ti bodi nad petimi mesti.‹
Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20 In prišel je še en, rekoč: ›Gospod, glej, tukaj je tvoj funt, ki sem ga hranil v prtiču,
“Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21 kajti bal sem se te, ker si strog človek; jemlješ to, česar nisi položil in žanješ to, česar nisi posejal.‹
kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22 On pa mu reče: ›Po tvojih lastnih ustih te bom sodil, ti zlobni služabnik. Vedel si, da sem bil strog človek, ki jemljem to, česar nisem položil in žanjem to, česar nisem posejal.
Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23 Zakaj torej mojega denarja nisi dal v banko, da bi lahko ob svojem prihodu svojo lastnino zahteval z obrestmi?‹
Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24 In rekel je tem, ki so stali poleg: ›Vzemite od njega funt in ga dajte tistemu, ki ima deset funtov.‹
Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25 (Oni pa so mu rekli: ›Gospod, ta ima deset funtov.‹)
Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26 Kajti povem vam: ›Da se bo vsakemu, ki ima, dalo; od tistega, ki nima, pa se bo odvzelo celó to, kar ima.‹
Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27 Toda tiste moje sovražnike, ki niso hoteli, da bi jim jaz vladal, privedite sèm in jih pokončajte pred menoj.‹«
Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
28 In ko je tako govoril, je šel pred njimi ter se vzpenjal v Jeruzalem.
Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29 Pripetilo pa se je, ko je prišel blizu Bétfage in Betanije, pri gori, ki se imenuje Oljska gora, [da] je poslal dva izmed svojih učencev,
Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30 rekoč: »Pojdita v vas nasproti vama, v kateri bosta ob svojem vstopu našla privezano žrebe, na katerem človek še nikoli ni sedel. Odvežita ga in ga privedita sèm.
akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31 Če pa vaju katerikoli človek vpraša: ›Zakaj ga odvezujeta?‹ mu recita takole: ›Ker ga potrebuje Gospod.‹«
Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
32 In onadva, ki sta bila poslana, sta šla svojo pot in našla tako, kakor jima je povedal.
Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33 In ko sta odvezovala žrebe, so jima lastniki le-tega rekli: »Zakaj odvezujeta žrebe?«
Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
34 Onadva pa sta rekla: »Gospod ga potrebuje.«
Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
35 In privedla sta ga k Jezusu in svoje obleke vrgla na žrebe ter nanj posadila Jezusa.
Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36 In ko je šel, so na pot razgrinjali svoja oblačila.
Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37 Ko je prišel blizu, torej celó k pobočju Oljske gore, se je celotna množica učencev začela veseliti in z močnim glasom hvaliti Boga za vsa mogočna dela, ki so jih videli,
Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38 rekoč: »Blagoslovljen naj bo Kralj, ki prihaja v imenu Gospodovem. V nebesih mir in slava na višavah.«
wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
39 Nekaj farizejev izmed množice pa mu je reklo: »Učitelj, oštej svoje učence.«
Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
40 In odgovoril jim je in jim rekel: »Povem vam, da če bi ti molčali, bodo takoj kamni zavpili.«
Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
41 Ko pa je prišel bliže, je zagledal mesto ter se razjokal nad njim,
Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42 rekoč: »Če bi ti spoznalo, celó ti, vsaj na ta tvoj dan, stvari, ki pripadajo tvojemu miru! Toda sedaj so skrite pred tvojimi očmi.
akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43 Kajti nadte bodo prišli dnevi, ko bodo tvoji sovražniki okoli tebe nasuli okope in te obkolili in te stiskali na vsaki strani
Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44 in zravnali te bodo z zemljo in tvoje otroke v tebi; in v tebi ne bodo pustili enega kamna na drugem, ker nisi spoznalo časa svojega obiskanja.«
Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
45 In odšel je v tempelj ter začel izganjati te, ki so v njem prodajali in te, ki so kupovali,
Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46 rekoč jim: »Pisano je: ›Moja hiša je hiša molitve, ‹ toda vi ste jo naredili za brlog razbojnikov.«
akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
47 In vsak dan je učil v templju. Toda visoki duhovniki in pisarji in vodje ljudstva so si prizadevali, da ga pokončajo,
Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48 pa niso mogli najti, kaj bi lahko storili, kajti vsi ljudje so ga zelo pozorno poslušali.
lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.

< Luka 19 >