< Sodniki 7 >

1 Potem je Jerubáal, ki je Gideón in vse ljudstvo, ki je bilo z njim, vstalo zgodaj in se utaborilo poleg vodnjaka Haród, tako da je bila vojska Midjáncev na njihovi severni strani, v dolini pri Moréjevem hribu.
Ndipo Yerub-Baali (yaani Gideoni) na lile jeshi lililokuwa pamoja naye, wakaondoka asubuhi na mapema na kupiga kambi kando ya chemchemi ya Harodi. Kambi ya Wamidiani ilikuwa kaskazini yao katika bonde karibu na kilima cha More.
2 Gospod je rekel Gideónu: »Ljudstva, ki je s teboj, je zame preveč, da bi Midjánce izročil v njihove roke, da se ne bi Izrael poveličeval zoper mene, rekoč: ›Moja lastna roka me je rešila.‹«
Bwana akamwambia Gideoni, “Jeshi lililo pamoja nawe ni kubwa sana kwa mimi kuwatia Wamidiani mikononi mwao. Ili kwamba Israeli asije akajisifu juu yangu akisema, ‘Mkono wangu ndio ulioniokoa,
3 Zdaj torej pojdi, razglasi v ušesa ljudstva, rekoč: ›Kdorkoli je boječ in se boji, naj se vrne in zgodaj odide z gore Gileád.‹« In tam se jih je izmed ljudstva vrnilo dvaindvajset tisoč, ostalo pa jih je deset tisoč.
kwa hiyo sasa tangaza jeshi lote likiwa linasikia, kwamba: Yeyote anayeogopa na kutetemeka, yeye na arudi nyumbani, aondoke katika Mlima Gileadi.’” Hivyo watu 22,000 walirudi, wakabaki 10,000.
4 Gospod je rekel Gideónu: »Ljudstva je še preveč. Privedi jih dol k vodi in tam ti jih bom preizkusil.« Zgodilo se bo, da o komer ti rečem: ›Ta bo šel s teboj, ‹ bo ta isti šel s teboj; in o komer ti rečem: ›Ta ne bo šel s teboj, ‹ ta isti ne bo šel.«
Lakini Bwana akamwambia Gideoni, “Idadi ya jeshi bado ni kubwa. Wapeleke chini katika maji nami nitawajaribu huko kwa ajili yako. Kama nikikuambia, ‘Huyu atakwenda pamoja nawe,’ yeye atakwenda; lakini kama nikisema, ‘Huyu hatakwenda pamoja nawe,’ yeye hatakwenda.”
5 Tako je ljudstvo privedel dol k vodi in Gospod je rekel Gideónu: »Kdorkoli s svojim jezikom sreba vodo, kakor sreba pes, tega boš postavil poleg sebe, podobno vsakega, ki poklekne dol na svoja kolena, da bi pil.«
Hivyo Gideoni akalileta lile jeshi chini kwenye maji naye Bwana akamwambia Gideoni, “Watenge upande mmoja wale wote wanywao maji kwa ulimi, kama vile mbwa anywavyo, wale wote wapigao magoti ili kunywa wakipeleka mikono yao vinywani mwao, waweke upande mwingine.”
6 Število tistih, ki so srebali s pristavljanjem svoje roke k svojim ustom, je bilo tristo mož, toda vsi drugi izmed ljudstva so se upognili na svoja kolena, da pijejo vodo.
Idadi ya wale waliokunywa kwa kuramba ramba walikuwa 300, lakini wengine wote katika jeshi walipiga magoti ili kunywa.
7 Gospod je rekel Gideónu: »S tristo možmi, ki so srebali, vas bom rešil in Midjánce izročil v tvojo roko. Vse preostalo ljudstvo pa naj gre vsak mož k svojemu kraju.«
Bwana akamwambia Gideoni, “Kwa hao watu 300 walioramba maji nitawaokoa ninyi, nami nitawatia Wamidiani mkononi mwako. Waache hao watu wengine wote warudi kila mmoja nyumbani mwake.”
8 Tako je ljudstvo v svojo roko vzelo živež in svoje šofarje, ves preostanek Izraela pa je vsakega moža poslal k svojemu šotoru in obdržal tistih tristo mož. Midjánska vojska pa je bila pod njim v dolini.
Hivyo Gideoni akawaacha wale Waisraeli wengine kila mmoja aende kwenye hema yake. Akabakia na wale 300, ambao walichukua vyakula na tarumbeta za wale wenzao. Basi kambi ya Wamidiani ilikuwa chini yake bondeni.
9 Iste noči se je pripetilo, da mu je Gospod rekel: »Vstani, spusti se k vojski, kajti izročil sem jo v tvojo roko.
Usiku ule ule Bwana akamwambia Gideoni, “Ondoka, ushuke kambini, kwa kuwa nimeitia mkononi mwako.
10 Toda če se bojiš iti dol, pojdi dol k vojski s svojim služabnikom Purájem.
Lakini kama unaogopa kushambulia, shuka kambini pamoja na mtumishi wako Pura,
11 Slišal boš kaj govorijo. Potem se bodo tvoje roke okrepile, da greš dol k vojski.« Potem je s svojim služabnikom Purájem odšel dol k zunanjim izmed oboroženih mož, ki so bili v vojski.
nawe sikiliza wanayosema. Hatimaye, utatiwa moyo kushambulia kambi.” Basi yeye na Pura mtumishi wake wakashuka na kufikia walinzi wa mbele wenye silaha waliokuwa mle kambini.
12 Midjánci in Amalečani in vsi otroci vzhoda pa so ležali povprek po dolini, zaradi množice podobni kobilicam in njihovih kamel je bilo zaradi množice brez števila, kakor peska ob morski obali.
Wamidiani, Waamaleki na mataifa mengine yote ya mashariki walikaa bondeni, nao walikuwa mfano wa nzige kwa wingi wao. Ngamia zao hazikuhesabika, wingi wao ulikuwa kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.
13 Ko je Gideón prišel, glej, je bil tam mož, ki je svojemu tovarišu povedal sanje ter rekel: »Glej, sanjal sem sanje in glej, kolač ječmenovega kruha se je privalil v midjánsko vojsko, prišel k šotoru in ga udaril, da je ta padel in ga prevrnil, da je ležal postrani.«
Gideoni alifika wakati huo huo kukiwa na mtu mmoja aliyekuwa anamweleza mwenzake ndoto yake, akisema, “Niliota ndoto: Tazama mkate wa shayiri ulioviringana ulianguka katika kambi moja ya Wamidiani, ukaipiga na ikaanguka nao ukaipindua juu chini na hema ikaporomoka chini.”
14 Njegov tovariš je odgovoril in rekel: »To ni nič drugega kakor meč Gideóna, Joáševega sina, moža iz Izraela, kajti v njegovo roko je Bog izročil Midjánce in vso vojsko.«
Rafiki yake akamjibu, “Habari hii si kitu kingine zaidi ya upanga wa Gideoni mwana wa Yoashi, Mwisraeli. Mungu amewatia Wamidiani na jeshi lote mkononi mwake.”
15 Bilo je tako, ko je Gideón slišal pripovedovanje sanj in njeno razlago, da je oboževal, se vrnil v Izraelovo vojsko in rekel: »Vstanite, kajti Gospod je v vašo roko izročil midjánsko vojsko.«
Gideoni alipoisikia hiyo ndoto na tafsiri yake, akamwabudu Mungu. Akarudi kwenye kambi ya Israeli na kusema, “Inukeni! Bwana amelitia jeshi la Wamidiani mikononi mwenu.”
16 Tristo mož je razdelil na tri skupine in v roko vsakega moža položil šofar s praznimi lončenimi vrči in svetilkami znotraj vrčev.
Akawagawa wale watu 300 katika makundi matatu, akawakabidhi tarumbeta mikononi mwao wote na mitungi isiyokuwa na maji yenye mienge ndani yake.
17 Rekel jim je: »Glejte mene in storite podobno. In glejte, ko pridem k robu tabora, se bo zgodilo, da kakor storim jaz, boste tako storili tudi vi.
Akawaambia, “Nitazameni, fanyeni kama nitakavyofanya, nitakapofika mwisho wa kambi mfanye kama nitakavyofanya.
18 Ko zatrobim s šofarjem, jaz in vsi tisti, ki so z menoj, potem tudi vi zatrobite s šofarji na vsaki strani tabora in recite: › Meč od Gospoda in od Gideóna.‹«
Wakati mimi na wale walio pamoja nami wote, tutakapopiga tarumbeta zetu, ninyi nanyi pigeni tarumbeta pande zote za kambi na mpige kelele, mseme, ‘Upanga wa Bwana na wa Gideoni.’”
19 Tako so Gideón in sto mož, ki so bili z njim, prišli k robu tabora na začetku srednje straže in imeli so ravno sveže postavljeno stražo. Zatrobili so na šofarje in razbili lončene vrče, ki so bili v njihovih rokah.
Gideoni na wale watu 100 waliokuwa pamoja naye wakafika mwisho wa kambi usiku mwanzoni mwa zamu ya kati, mara tu walipokuwa wamebadili zamu. Wakapiga zile tarumbeta zao na kuvunja ile mitungi iliyokuwa mikononi mwao.
20 Tri skupine so trobile na šofarje in razbile lončene vrče in držale svetilke v svojih levicah in šofarje v svojih desnicah, da z njimi trobijo in kričali: »Meč od Gospoda in od Gideóna.«
Yale makundi matatu yakapiga tarumbeta na kuvunja mitungi. Wakashika mienge kwa mikono yao ya kushoto na katika mikono yao ya kuume tarumbeta ili kuzipiga, wakapaza sauti zao, “Upanga wa Bwana na wa Gideoni!”
21 Stali so vsak mož na svojem mestu okoli tabora in vsa vojska je stekla, kričala in pobegnila.
Wakasimama kila mtu mahali pake kuizunguka kambi pande zote, Wamidiani wote wakakimbia, huku wakipiga kelele.
22 Tristo [jih] je trobilo na šofarje in Gospod je torej po vsej vojski naravnal meč vsakega moža zoper svojega tovariša in vojska je pobegnila do Bet Šite v Cerédi in do meje Abél Mehóle, do Tabáta.
Walipozipiga zile tarumbeta 300, Bwana akafanya watu katika kambi yote kugeuziana upanga kila mmoja na mwenziwe. Jeshi likakimbia mpaka Beth-Shita kuelekea Serera hadi mpakani mwa Abel-Mehola karibu na Tabathi.
23 Izraelovi možje so se zbrali skupaj iz Neftálija, iz Aserja, iz vsega Manáseja in zasledovali Midjánce.
Watu wa Israeli wakaitwa kutoka Naftali, Asheri na Manase, wakawafuatia Wamidiani.
24 Gideón je poslal poslance po vsej gori Efrájim, rekoč: »Pridite dol zoper Midjánce in pred njimi zasedite vode do Bet Bare in Jordana.« Potem so se vsi Efrájimovi možje zbrali skupaj in zasedli vode do Bet Bare in Jordana.
Gideoni akatuma wajumbe katika nchi yote ya vilima vya Efraimu akisema, “Teremkeni dhidi ya Wamidiani na mkazuie vivuko vya maji mbele yao hadi Beth-Bara na pia Yordani.” Hivyo watu wote wa Efraimu wakakutanika pamoja na kuzingira mto wa Yordani hadi Beth-Bara.
25 Zajeli so dva princa izmed Midjáncev, Oréba in Zeéba. Oréba so usmrtili na Orébovi skali, Zeéba pa so usmrtili na Zeébovi vinski stiskalnici in zasledovali Midjánce ter glavi Oréba in Zeéba prinesli Gideónu, na drugo stran Jordana.
Wakawakamata wakuu wawili wa Midiani, Orebu na Zeebu. Wakamuulia Orebu pale penye mwamba wa Orebu, na Zeebu wakamuulia penye shinikizo la kukamulia divai la Zeebu. Wakawafuatia Wamidiani na kuleta vichwa vya Orebu na Zeebu kwa Gideoni, huko ngʼambo ya Yordani.

< Sodniki 7 >