< Псалтирь 30 >

1 Псалом песни обновления дому Давидова. Вознесу Тя, Господи, яко подял мя еси, и не возвеселил еси врагов моих о мне.
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2 Господи Боже мой, воззвах к Тебе, и изцелил мя еси.
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3 Господи, возвел еси от ада душу мою, спасл мя еси от низходящих в ров. (Sheol h7585)
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol h7585)
4 Пойте Господеви, преподобнии Его, и исповедайте память святыни Его:
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
5 яко гнев в ярости Его, и живот в воли Его: вечер водворится плачь, и заутра радость.
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
6 Аз же рех во обилии моем: не подвижуся во век.
Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7 Господи, волею Твоею подаждь доброте моей силу: отвратил же еси лице Твое, и бых смущен.
Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
8 К Тебе, Господи, воззову, и к Богу моему помолюся.
Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
9 Кая польза в крови моей, внегда сходити ми во истление? Еда исповестся Тебе персть? Или возвестит истину Твою?
“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
10 Слыша Господь и помилова мя: Господь бысть помощник мой.
Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
11 Обратил еси плачь мой в радость мне, растерзал еси вретище мое и препоясал мя еси веселием,
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
12 яко да воспоет Тебе слава моя, и не умилюся. Господи Боже мой, во век исповемся Тебе.
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.

< Псалтирь 30 >