< Бытие 9 >

1 И благослови Бог Ноа и сыны его и рече им: раститеся и множитеся, и наполните землю и обладайте ею:
Ndipo Mungu akambariki Noa na wanawe, akiwaambia, “Zaeni mkaongezeke kwa idadi na mkaijaze tena dunia.
2 и страх и трепет ваш будет на всех зверех земных (и на всех скотех земных, ) на всех птицах небесных и на всех движущихся по земли и на всех рыбах морских: в руце вашы вдах (я).
Wanyama wote wa duniani, ndege wote wa angani, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi, na samaki wote wa baharini wamekabidhiwa mikononi mwenu, nao watawaogopa na kuwahofu.
3 И всякое движущееся, еже есть живо, вам будет в снедь: яко зелие травное дах вам все.
Kila kitu chenye uhai kiendacho kitakuwa chakula chenu. Kama vile nilivyowapa mimea mbalimbali, sasa nawapa kila kitu.
4 Точию мяса в крови души да не снесте.
“Lakini kamwe msile nyama ambayo bado ina damu ya uhai wake, kwa maana damu ni uhai.
5 Крови бо вашей, душ ваших, от руки всякаго зверя изыщу (ея): и от руки человека брата изыщу ея.
Hakika damu ya uhai wenu nitaidai. Nitaidai kutoka kwa kila mnyama. Kutoka kwa kila mwanadamu pia nitaidai kwa ajili ya uhai wa mtu mwenzake.
6 Проливаяй кровь человечу, в ея место его пролиется: яко во образ Божий сотворих человека.
“Yeyote amwagaye damu ya mwanadamu, damu yake itamwagwa na mwanadamu, kwa kuwa katika mfano wa Mungu, Mungu alimuumba mwanadamu.
7 Вы же раститеся и множитеся, и наполните землю, и множитеся на ней.
Kuhusu ninyi, zaeni mwongezeke kwa wingi, mzidi katika dunia na kuijaza.”
8 И рече Бог Ноеви и сыном его с ним, глаголя:
Ndipo Mungu akamwambia Noa na wanawe pamoja naye:
9 се, Аз поставляю завет Мой вам и семени вашему по вас,
“Sasa mimi ninaweka Agano langu nanyi, pamoja na uzao wenu baada yenu,
10 и всякой души живущей с вами от птиц и от скот и всем зверем земным, елика с вами (суть) от всех изшедших из ковчега:
pia na kila kiumbe hai kilichokuwa pamoja nanyi: Ndege, wanyama wa kufugwa na wanyama wote wa porini, wale wote waliotoka katika safina pamoja nanyi, kila kiumbe hai duniani.
11 и поставлю завет Мой с вами: и не умрет всяка плоть ктому от воды потопныя, и ктому не будет потоп водный, еже истлити всю землю.
Ninaweka Agano nanyi: Kamwe uhai hautafutwa tena kwa gharika, kamwe haitakuwepo tena gharika ya kuangamiza dunia.”
12 И рече Господь Бог Ноеви: сие знамение завета, еже Аз даю между Мною и вами, и между всякою душею живою, яже есть с вами, в роды вечныя:
Mungu akasema, “Hii ni ishara ya Agano ninalofanya kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, Agano kwa vizazi vyote vijavyo:
13 дугу Мою полагаю во облаце, и будет в знамение завета (вечнаго) между Мною и землею.
Nimeweka upinde wangu wa mvua mawinguni, nao utakuwa ishara ya Agano nifanyalo kati yangu na dunia.
14 И будет егда наведу облаки на землю, явится дуга Моя во облаце:
Wakati wowote ninapotanda mawingu juu ya dunia na upinde wa mvua ukijitokeza mawinguni,
15 и помяну завет Мой, иже есть между Мною и вами, и между всякою душею живущею во всякой плоти, и не будет ктому вода в потоп, яко потребити всяку плоть.
nitakumbuka Agano langu kati yangu na ninyi na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina. Kamwe maji hayatakuwa tena gharika ya kuangamiza uhai wote.
16 И будет дуга Моя во облаце: и узрю ю, еже помянути завет вечный между Мною и землею, и между всякою душею живущею во всякой плоти, яже есть на земли.
Wakati wowote upinde wa mvua unapotokea mawinguni, nitauona na kukumbuka Agano la milele kati ya Mungu na viumbe vyote vilivyo hai vya kila aina duniani.”
17 И рече Бог Ноеви: сие знамение завета, егоже положих между Мною и между всякою плотию, яже есть на земли.
Hivyo Mungu akamwambia Noa, “Hii ndiyo ishara ya Agano ambalo nimelifanya kati yangu na viumbe vyote vilivyo hai duniani.”
18 Быша же сынове Ноевы изшедшии из ковчега, Сим, Хам, Иафеф: Хам же бяше отец Ханаань.
Wana wa Noa waliotoka ndani ya safina ni: Shemu, Hamu na Yafethi. (Hamu ndiye alikuwa baba wa Kanaani.)
19 Трие сии суть сынове Ноевы: от сих разсеяшася по всей земли.
Hawa ndio waliokuwa wana watatu wa Noa, kutokana nao watu walienea katika dunia.
20 И начат Ное человек делатель (быти) земли, и насади виноград:
Noa akawa mkulima, akawa mtu wa kwanza kupanda mizabibu.
21 и испи от вина, и упися, и обнажися в дому своем.
Alipokunywa huo mvinyo wake akalewa na akalala uchi kwenye hema lake.
22 И виде Хам отец Ханаань наготу отца своего, и изшед вон поведа обема братома своима.
Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake na kuwaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23 И вземше сим и Иафеф ризу, возложиша (ю) на обе раме свои, и идоша вспять зряще, и покрыша наготу отца своего: и лице их вспять зря, и наготы отца своего не видеша.
Lakini Shemu na Yafethi wakachukua nguo wakaitanda mabegani mwao wote wawili, kisha wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zilielekea upande mwingine ili wasiuone uchi wa baba yao.
24 Истрезвися же Ное от вина, и разуме елика сотвори ему сын его юнейший,
Noa alipolevuka kutoka kwenye mvinyo wake na kujua lile ambalo mwanawe mdogo kuliko wote alilokuwa amemtendea,
25 и рече: проклят (буди) Ханаан отрок: раб будет братиям своим.
akasema, “Alaaniwe Kanaani! Atakuwa mtumwa wa chini sana kuliko watumwa wote kwa ndugu zake.”
26 И рече: благословен Господь Бог Симов: и будет Ханаан отрок раб ему:
Pia akasema, “Abarikiwe Bwana, Mungu wa Shemu! Kanaani na awe mtumwa wa Shemu.
27 да распространит Бог Иафефа, и да вселится в селениих Симовых, и да будет Ханаан раб ему.
Mungu na apanue mipaka ya Yafethi; Yafethi na aishi katika mahema ya Shemu, na Kanaani na awe mtumwa wake.”
28 Поживе же Ное по потопе лет триста пятьдесят.
Baada ya gharika Noa aliishi miaka 350.
29 И быша вси дние Ноевы лет девять сот пятьдесят: и умре.
Noa alikuwa na jumla ya miaka 950, ndipo akafa.

< Бытие 9 >