< Деяния святых апостолов 11 >

1 Слышаша же Апостоли и братия сущии во Иудеи, яко и языцы прияша слово Божие.
Mitume na ndugu walioamini waliokuwa huko Uyahudi wakasikia kuwa watu wa Mataifa nao wamepokea neno la Mungu.
2 И егда взыде Петр во Иерусалим, препирахуся с ним иже от обрезания,
Hivyo Petro alipopanda Yerusalemu, wale wa tohara waliokuwa wameamini wakamshutumu,
3 глаголюще, яко к мужем обрезания не имущым вшел еси и ял еси с ними.
wakisema, “Ulikwenda kwa watu wasiotahiriwa na kula pamoja nao.”
4 Начен же Петр, сказоваше им поряду, глаголя:
Ndipo Petro akaanza kuwaeleza kuhusu mambo yote yalivyotokea hatua kwa hatua akisema,
5 аз бех во граде Июппийстем моляся и видех во ужасе видение, сходящь сосуд некий, яко плащаницу велию, от четырех краев низпущаему с небесе, и прииде даже до мене:
“Nilikuwa katika mji wa Yafa nikiomba, nami nikapitiwa na usingizi wa ghafula, nikaona maono. Kulikuwa na kitu kama nguo kubwa ikishuka kutoka mbinguni, ikishushwa kwa ncha zake nne, nayo ikanikaribia.
6 в нюже воззрев смотрях, и видех четвероногая земная и звери и гады и птицы небесныя.
Nilipoangalia ndani yake kwa karibu niliona wanyama wenye miguu minne wa nchini, wanyama wa mwitu, watambaao na ndege wa angani.
7 Слышах же глас глаголющь мне: востав, Петре, заколи и яждь.
Ndipo nikasikia sauti ikiniambia, ‘Petro, ondoka uchinje na ule.’
8 Рех же: никакоже, Господи, яко всяко скверно или нечисто николиже вниде во уста моя.
“Nikajibu, ‘La hasha Bwana! Kitu chochote kilicho najisi hakijaingia kinywani mwangu.’
9 Отвеща же ми глас вторицею с небесе глаголющь: яже Бог очистил есть, ты не скверни.
“Sauti ikasema kutoka mbinguni mara ya pili, ‘Usikiite najisi kitu chochote Mungu alichokitakasa.’
10 Сие же бысть трижды: и паки взяшася вся на небо.
Jambo hili lilitokea mara tatu, ndipo kile kitu kikavutwa tena mbinguni.
11 И се, абие трие мужие сташа пред храминою, в нейже бех, послани от Кесарии ко мне.
“Wakati ule ule watu watatu, waliokuwa wametumwa kutoka Kaisaria waliwasili katika nyumba niliyokuwa nikikaa.
12 Рече же ми Дух ити с ними, ничтоже разсуждая: приидоша же со мною и шесть братия сии, и внидохом в дом мужа.
Roho Mtakatifu akaniambia niende nao bila kuwa na ubaguzi kati yao na sisi. Hawa ndugu sita pia walifuatana nami, nasi tukaingia nyumbani mwa huyo Kornelio.
13 И возвести нам, како виде Ангела (свята) в дому своем, ставша и рекша ему: посли во Июппию мужы и призови Симона, нарицаемаго Петра,
Akatuambia jinsi alivyoona malaika aliyekuwa amesimama katika nyumba yake na kusema, ‘Tuma watu waende Yafa wakamlete Simoni aitwaye Petro.
14 иже речет глаголы к тебе, в нихже спасешися ты и весь дом твой.
Yeye atakupa ujumbe ambao kwa huo wewe na wa nyumbani mwako wote mtaokoka.’
15 Внегда же начах глаголати, нападе Дух Святый на них, якоже и на ны в начале.
“Nami nilipoanza kusema, Roho Mtakatifu akashuka juu yao kama vile alivyotushukia sisi hapo mwanzo.
16 Помянух же глаголгол Господень, якоже глаголаше: Иоанн убо крестил есть водою, вы же имате креститися Духом Святым.
Nami nikakumbuka neno la Bwana alivyosema, ‘Yohana alibatiza kwa maji, lakini ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu.’
17 Аще убо равен дар даде им Бог, якоже и нам веровавшым в Господа нашего Иисуса Христа, аз же кто бех могий возбранити Бога?
Basi ikiwa Mungu aliwapa hawa watu kipawa kile kile alichotupa sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani hata nifikirie kuwa ningeweza kumpinga Mungu?”
18 Слышавше же сия умолкоша и славляху Бога, глаголюще: убо и языком Бог покаяние даде в живот.
Waliposikia haya hawakuwa na la kupinga zaidi. Nao wakamwadhimisha Mungu wakisema, “Basi, Mungu amewapa hata watu wa Mataifa toba iletayo uzima wa milele.”
19 Разсеявшиися убо от скорби, бывшия при Стефане, проидоша даже до Финикии и Кипра и Антиохии, ни единому же глаголюще слово, токмо Иудеем.
Basi wale waliotawanyika kwa ajili ya mateso yaliyotokana na kifo cha Stefano, wakasafiri hadi Foinike na Kipro na Antiokia. Nao hawakuhubiri lile Neno kwa mtu yeyote isipokuwa Wayahudi.
20 Бяху же нецыи от них мужие Кипрстии и Киринейстии, иже, вшедше во Антиохию, глаголаху к Еллином, благовествующе Господа Иисуса.
Lakini baadhi yao walikuwepo watu wa Kipro na Kirene, ambao walipokuja Antiokia walinena na Wayunani pia wakiwahubiria habari njema za Bwana Yesu.
21 И бе рука Господня с ними: многое же число веровавше обратишася ко Господу.
Mkono wa Bwana ulikuwa pamoja nao, nayo idadi kubwa ya watu wakaamini na kumgeukia Bwana.
22 Слышано же бысть слово о них во ушию церкве сущия во Иерусалиме, и послаша Варнаву преити даже до Антиохии:
Habari hizi zilipofika masikioni mwa kanisa huko Yerusalemu, wakamtuma Barnaba aende Antiokia.
23 иже пришед и видев благодать Божию, возрадовася и моляше всех изволением сердца терпети о Господе:
Alipofika na kuona madhihirisho ya neema ya Mungu, akafurahi na kuwatia moyo waendelee kuwa waaminifu kwa Bwana kwa mioyo yao yote.
24 яко бе муж благ и исполнь Духа Свята и веры. И приложися народ мног Господеви.
Barnaba alikuwa mtu mwema, aliyejaa Roho Mtakatifu, mwenye imani, nayo idadi kubwa ya watu wakaongezeka kwa Bwana.
25 Изыде же Варнава в Тарс взыскати Савла, и обрет его, приведе его во Антиохию:
Kisha Barnaba akaenda Tarso kumtafuta Sauli,
26 бысть же им лето цело собиратися в церкви и учити народ мног, нарещи же прежде во Антиохии ученики Христианы.
naye alipompata akamleta Antiokia. Hivyo kwa mwaka mzima Barnaba na Sauli wakakutana na kanisa na kufundisha idadi kubwa ya watu. Ilikuwa ni katika kanisa la Antiokia kwa mara ya kwanza wanafunzi waliitwa Wakristo.
27 В тыя же дни снидоша от Иерусалима пророцы во Антиохию:
Wakati huo manabii walishuka toka Yerusalemu hadi Antiokia.
28 востав же един от них, именем Агав, назнаменаше Духом глад велик хотящь быти по всей вселенней, иже и бысть при Клавдии кесари:
Mmoja wao, jina lake Agabo, akasimama akatabiri kwa uweza wa Roho Mtakatifu kwamba njaa kubwa itaenea ulimwengu mzima. Njaa hiyo ilitokea wakati wa utawala wa Klaudio.
29 от ученик же, по елику кто имеяше что, изволиша кийждо их на службу послати живущым во Иудеи братиям,
Mitume wakaamua kwamba kila mtu, kulingana na uwezo alio nao, atoe msaada kwa ajili ya ndugu wanaoishi Uyahudi.
30 еже и сотвориша, пославше к старцем рукою Варнавлею и Савлею.
Wakafanya hivyo, misaada yao ikapelekwa kwa wazee kwa mikono ya Barnaba na Sauli.

< Деяния святых апостолов 11 >