< Второе послание к Коринфянам 10 >

1 Сам же аз Павел молю вы кротостию и тихостию Христовою, иже в лице убо смирен в вас, не сый же у вас дерзаю в вас.
Mimi Paulo mwenyewe ambaye naonekana kuwa mpole nikiwa pamoja nanyi, lakini mkali wakati nikiwa mbali nanyi, nawasihini kwa huruma na wema wake Kristo.
2 Молю же, да не присущ дерзаю надеянием, имже помышляю смети на некия непщующыя нас яко по плоти ходящих.
Nawaombeni msinisababishe kuwa mkali wakati nitakapokuja, maana nina hakika naweza kuwa mkali kwa wote wale wanaotudhania kwamba tunaishi kidunia.
3 Во плоти бо ходяще, не по плоти воинствуем:
Kweli tunaishi duniani, lakini hatupigani vita kidunia.
4 оружия бо воинства нашего не плотская, но сильна Богом на разорение твердем: помышления низлагающе,
Maana, silaha tunazotumia katika vita vyetu si silaha za kidunia, ila ni nguvu za Mungu zenye kuharibu ngome zote. Tunaharibu hoja zote za uongo,
5 и всяко возношение взимающееся на разум Божий, и пленяюще всяк разум в послушание Христово,
na kubomoa kila kizuizi cha majivuno kilichowekwa kuipinga elimu ya Mungu; tunaziteka fikira zote na kuzifanya zimtii Kristo.
6 и в готовости имуще отмстити всяко преслушание, егда исполнится ваше послушание.
Mkisha kuwa wakamilifu katika kutii, sisi tuko tayari kuadhibu kila namna ya kutotii.
7 Иже ли пред лицем, зрите? Аще кто надеется себе Христова быти, да помышляет паки от себе, зане, якоже он Христов, такожде и мы Христовы.
Ninyi hutazama mambo kwa nje tu. Je, yupo mtu yeyote anayedhani kwamba yeye ni wa Kristo? Sawa! Basi, afikirie vilevile kwamba sisi pia ni wa Kristo kama yeye alivyo wa Kristo.
8 Аще бо и лишше что похвалюся о власти нашей, юже даде нам Господь в создание, а не на разорение ваше, не постыжуся.
Hata kama nimezidi katika kujivuna kwangu juu ya ule uwezo aliotupa—uwezo wa kuwajenga na sio wa kubomoa—hata hivyo sijutii hata kidogo.
9 Но да не явлюся, яко страшя вас посланьми.
Sipendi mfikiri kwamba nataka kuwatisha ninyi kwa barua zangu.
10 Яко послания убо, рече, тяжка и крепка, а пришествие тела немощно, и слово уничиженно:
Mtu anaweza kusema: “Barua za Paulo ni kali na zenye maneno mazito, lakini yeye mwenyewe anapokuwa pamoja nasi ni mtu dhaifu, na hata anapoongea maneno yake ni kama si kitu.”
11 сие да помышляет таковый, яко яцы же есмы словом посланий, отстояще, таковии и ту суще есмы делом.
Mtu asemaye hivyo heri akumbuke kwamba hakuna tofauti ya yale tunayoandika katika barua wakati tuko mbali, na yale tutakayofanya wakati tutakapokuwa nanyi.
12 Не смеем бо судити, или прикладовати себе иным хвалящым себе самех: но сами в себе себе измеряюще, и прилагающе себе самим себе, не разумевают.
Kwa vyovyote hatungethubutu kujiweka au kujilinganisha na wale watu wanaojisifia wenyewe. Watu wenye kujifanya wao kuwa kipimo cha kujipimia, na watu wanaojilinganisha wenyewe kwa wenyewe, ni wapumbavu.
13 Мы же не в безмерная похвалимся, но по мере правила, егоже раздели нам Бог меру, достизати даже и до вас.
Lakini sisi hatutajivuna kupita kiasi; kujivuna huko kutabaki katika kile kipimo cha kazi aliyotukabidhi Mungu, kazi ambayo tunaifanya pia kwenu.
14 Не яко бо не досяжуще до вас, паче простираем себе, даже бо и до вас достигохом благовестием Христовым:
Na kwa vile ninyi mu katika mipaka hiyo, hatukuipita tulipokuja kwenu, tukiwaleteeni Habari Njema juu ya Kristo.
15 не в безмерная хвалящеся в чуждих трудех, упование же имуще, растущей вере вашей, в вас величатися по правилу нашему изобильно,
Basi, hatujivunii kazi waliyofanya wengine zaidi ya kipimo tulichopewa; ila tunatumaini kwamba imani yenu itazidi miongoni mwenu kufuatana na kipimo alichotuwekea Mungu.
16 во еже и в дальших вас странах благовестити, не чужим правилом в готовых похвалитися.
Hapo tutaweza kuihubiri Habari Njema katika nchi nyingine, mbali nanyi; na haitakuwa shauri la kujivunia kazi waliyofanya watu wengine mahali pengine.
17 Хваляйся же, о Господе да хвалится:
Lakini kama yasemavyo Maandiko: “Mwenye kuona fahari na aone fahari juu ya alichofanya Bwana.”
18 не хваляй бо себе сей искусен, но егоже Бог восхваляет.
Anayekubaliwa si yule anayejisifu mwenyewe, bali yule anayesifiwa na Bwana.

< Второе послание к Коринфянам 10 >