< Вторая книга Паралипоменон 24 >

1 Седми лет бе Иоас, егда царствовати нача, и четыредесять лет царствова во Иерусалиме. Имя же матери его Савиа от Вирсавеи.
Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka arobaini. Mama yake aliitwa Sibia aliyekuwa ametoka Beer-Sheba.
2 Сотвори же Иоас угодное пред Господем во вся дни Иодаа священника.
Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana miaka yote ya Yehoyada kuhani.
3 И поят ему Иодай жены две, и родиша сыны и дщери.
Yehoyada akamwoza wake wawili, akazaa watoto wa kiume na wa kike.
4 И бысть по сих, и взыде на сердце Иоасу, да возновит дом Господень.
Baada ya muda, Yoashi akaamua kukarabati Hekalu la Bwana.
5 И собра священники и левиты и рече им: идите во грады Иудины, и соберите от всего Израиля сребро ко обновлению храма Господня от лета до лета, и поспешно сотворите. Левити же не потщашася.
Akawaita pamoja makuhani na Walawi akawaambia, “Nendeni katika miji ya Yuda mkakusanye fedha wanazopaswa kulipa kila mwaka kutoka kwa Israeli wote, ili kukarabati Hekalu la Mungu wenu. Fanyeni hivyo sasa.” Lakini Walawi hawakufanya upesi.
6 И призва царь Иоас Иодаа началника и рече ему: почто не надсматрял еси левитов, еже принести от Иуды и от Иерусалима, еже уставлено есть от Моисеа человека Божия, егда собра Израиля в скинию свидения?
Kwa hiyo mfalme akamwita Yehoyada kuhani mkuu na kumwambia, “Kwa nini hukuwaambia Walawi walete kutoka Yuda na Yerusalemu kodi iliyowekwa na Mose mtumishi wa Bwana pamoja na kusanyiko la Israeli kwa ajili ya Hema ya Ushuhuda?”
7 Гофолиа бо бе нечестива, и сынове ея разориша дом Божий, яко святая дому Господня сотвориша Ваалиму.
Kwa kuwa wana wa yule mwanamke mwovu Athalia, walikuwa wamevunja na kuingia katika Hekalu la Mungu, nao wakawa wamevitumia hata vile vitu vilivyowekwa wakfu kwa Bwana kwa mabaali.
8 И повеле царь, да сотворят ковчежец и поставят при вратех Господних извне,
Kwa amri ya mfalme, likatengenezwa kasha, nalo likawekwa nje kwenye lango la Hekalu la Bwana.
9 и да проповедят во Иудеи и во Иерусалиме, приносити Господу, якоже устави Моисей раб Божий над Израилем в пустыни.
Tangazo likatolewa katika Yuda na Yerusalemu kwamba inapasa wamletee Bwana kodi ile ambayo Mose, mtumishi wa Bwana alikuwa amewaagiza Israeli huko jangwani.
10 И даша вси началницы и вси людие, и вношаху и влагаху в ковчежец, дондеже наполнися.
Maafisa wote na watu wote wakaleta michango yao kwa furaha, wakaweka kwenye kasha mpaka likajaa.
11 И бысть егда приношаху ковчежец к настоятелем царевым руками левитскими, и егда увидеша, яко умножися сребро, и прихождаше писарь царев и настоятель великаго жерца, и выбираху из ковчежца, и (паки) поставляху на место его: тако творяху от дне до дне, и собраша сребра много.
Ikawa kila wakati kasha lilipoletwa ndani na Walawi kwa maafisa wa mfalme na kuona kwamba kuna kiasi kikubwa cha fedha, mwandishi wa mfalme na afisa wa kuhani mkuu walikuwa wanakuja na kumimina, kisha kulirudisha mahali pake. Walifanya hivi mara kwa mara, nao wakakusanya fedha nyingi sana.
12 И вдаде е царь и Иодай жрец творящым дела на дело дому Господня: и наимаху каменосечцы и древодели, да устрояют дом Господень, и ковачы железу и меди, да укрепят дом Господень.
Mfalme na Yehoyada wakawapa wale watu waliofanya kazi iliyotakiwa katika Hekalu la Bwana. Wakawaajiri waashi na maseremala ili kutengeneza Hekalu la Bwana, pia wafanyakazi za chuma na shaba ili kukarabati Hekalu la Bwana.
13 И творяху творящии дела, и взыде долгота дел руками их, и возставиша дом Господень в состояние (прежнее) его, и укрепиша.
Watu walioshughulika na kazi walikuwa wenye bidii, nayo kazi ya kukarabati ikaendelea vizuri mikononi mwao. Wakalitengeneza upya Hekalu la Bwana likarudi katika hali yake ya awali na kuliimarisha.
14 Егда же совершиша, принесоша ко царю и ко Иодаю останок сребра, из негоже сотвориша сосуды в дом Господень, сосуды в служение всесожжений, и кадилницы златыя и сребряныя, и приношаху всесожжения в дому Господни непрестанно, во вся дни Иодаевы.
Walipokamilisha kazi hiyo ya kukarabati, wakaleta fedha zilizobaki wakampa mfalme na Yehoyada, nao kwa hizo wakatengeneza vyombo kwa ajili ya Hekalu la Bwana: Vyombo kwa ajili ya huduma na kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia mabakuli na vitu vingine vya dhahabu na fedha. Wakati wote Yehoyada alipokuwa hai, sadaka za kuteketezwa zilitolewa wakati wote katika Hekalu la Bwana.
15 И состареся Иодай исполнен дний, и умре сый ста тридесяти лет внегда скончатися ему:
Basi Yehoyada alikuwa mzee aliyeshiba siku wakati alipofariki. Alikufa akiwa na umri wa miaka 130.
16 и погребоша его во граде Давидове со царми, понеже сотвори благое со Израилем и с Богом и с домом Его.
Wakamzika pamoja na wafalme katika Mji wa Daudi, kwa sababu ya mema aliyokuwa ametenda katika Israeli kwa ajili ya Mungu na Hekalu lake.
17 И бысть по скончании Иодаеве, внидоша началницы Иудины и поклонишася царю: тогда послуша их царь.
Baada ya kifo cha Yehoyada, wakuu wa Yuda walikuja kumpa mfalme heshima, naye akawasikiliza.
18 И оставиша церковь Господа Бога отец своих и служаху Астарте и истуканным: и бысть гнев (Господень) на Иуду и Иерусалим в день той.
Wakaacha Hekalu la Bwana, Mungu wa baba zao, wakaabudu nguzo za maashera na sanamu. Kwa sababu ya hatia yao, hasira ya Mungu ikawajia Yuda na Yerusalemu.
19 И посла к ним пророки, да обратятся ко Господу, и не послушаша: и засвидетелствова им, и не покоришася.
Ingawa Bwana aliwatuma manabii wawarudishe watu kwake na ingawa waliwaonya, hawakuwasikiliza.
20 И Дух Божий облече Азарию священника сына Иодаева, и ста пред людьми и рече им: сия глаголет Господь: почто преступаете повеления Господня? Не поспешится вам, яко остависте Господа, и оставит вас.
Ndipo Roho wa Bwana akaja juu ya Zekaria mwana wa Yehoyada kuhani. Akasimama mbele ya watu akasema, “Hili ndilo asemalo Mungu, ‘Kwa nini mnakataa kuzitii amri za Bwana? Hamtafanikiwa kwa kuwa mmemwacha Bwana, yeye naye amewaacha ninyi.’”
21 И нападоша на него и побиша и камением по повелению Иоаса царя, во дворе дому Господня.
Lakini wakafanya shauri baya juu yake na kwa amri ya mfalme wakampiga kwa mawe mpaka akafa katika ukumbi wa Hekalu la Bwana.
22 И не воспомяну Иоас царь милосердия, еже сотвори Иодай отец его с ним, но уби сына его: иже, егда умираше, рече: да видит и судит Господь.
Mfalme Yoashi hakukumbuka wema aliotendewa na Yehoyada baba yake Zekaria ila alimuua mwanawe, ambaye alisema wakati akiwa amelala akingojea kufa, “Bwana na alione hili na alipize kisasi.”
23 И бысть по скончании лета, воста на него сила Сирская, и прииде на Иуду и на Иерусалим, и убиша вся началники в людех в церкви, и весь плен их послаша ко царю в Дамаск:
Mwishoni mwa ule mwaka, jeshi la Waaramu likaja dhidi ya Yoashi, likavamia Yuda na Yerusalemu na kuwaua viongozi wote wa watu. Wakapeleka nyara zao zote kwa mfalme wao huko Dameski.
24 зане в малых мужех прииде сила Сирская, и Бог предаде в руце их силу многу зело, зане оставиша Господа Бога отец своих: и на Иоаса сотвори суд.
Ingawa jeshi la Waaramu lilikuwa limekuja na watu wachache tu, Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa kuliko lao. Kwa sababu Yuda walikuwa wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao, hukumu ilitekelezwa juu ya Yoashi.
25 И по отшествии их от него, оставлену ему сущу в болезнех великих, и нападоша на него раби его за кровь священника сына Иодаева, и убиша его на постели его, и умре: и погребоша его во граде Давидове, но не погребоша его во гробех царских.
Waaramu walipoondoka, walimwacha Yoashi akiwa mgonjwa sana. Maafisa wake wakafanya hila dhidi yake kwa sababu alikuwa amemuua mwana wa Kuhani Yehoyada, nao wakamuulia kitandani mwake. Hivyo akafa na wakamzika katika Mji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.
26 Нападшии же на него, Завед сын Семаафов Амманитянин и Иозавед сын Самарифов Моавитянин,
Wale waliofanya hila mbaya dhidi yake walikuwa Zabadi, mwana wa Shimeathi mwanamke Mwamoni, Yehozabadi, mwana wa Shimrithi mwanamke Mmoabu.
27 и сынове его вси, и приступиша к нему пять. И прочая словес его, се, написана в летописце царстем. И воцарися Амасиа сын его вместо его.
Kwa habari za wanawe, unabii mwingi kumhusu na kumbukumbu za kutengenezwa upya kwa Hekalu la Mungu, zimeandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme. Amazia mwanawe akawa mfalme baada yake.

< Вторая книга Паралипоменон 24 >