< Первое послание Петра 4 >

1 Христу убо пострадавшу за ны плотию, и вы в ту же мысль вооружитеся: зане пострадавый плотию, преста от греха,
Maadamu Kristo aliteseka kimwili, nanyi pia mnapaswa kujiimarisha kwa nia hiyo yake; maana mtu akisha teseka kimwili hahusiki tena na dhambi.
2 во еже не ктому человеческим похотем, но воли Божией прочее во плоти жити время.
Tangu sasa, basi, maisha yaliowabakia kuishi hapa duniani yanapaswa kuongozwa na matakwa ya Mungu, si na tamaa za kibinadamu.
3 Довлеет бо вам мимошедшее время жития, волю языческую творившым, хождшым в нечистотах, в похотех, в мужеложстве, в скотоложстве, в помыслех, в пиянстве, в козлогласованиих, в лихоимании и богомерзких идолослужениих:
Wakati uliopita mlikuwa na muda mrefu wa kufanya mambo wanayofanya watu wasiomjua Mungu. Mliishi maisha ya anasa, ubinafsi, ulevi, ugomvi, kunywa mno na ya ibada haramu za sanamu.
4 о немже дивятся, не сходящымся вам в тоже блуда разлияние, хуляще:
Sasa, watu hao wasiomjua Mungu wanashangaa wanapoona kwamba hamwandamani nao tena katika hali ya kuishi vibaya, na hivyo wanawatukaneni.
5 иже воздадят слово готову Сущему судити живым и мертвым.
Lakini watapaswa kutoa hoja juu ya jambo hilo mbele yake Mungu aliye tayari kuwahukumu wazima na wafu!
6 На се бо и мертвым благовестися, да суд убо приимут по человеку плотию, поживут же по Бозе духом.
Kwa sababu hiyo, hao waliokufa ambao walikuwa wamehukumiwa katika maisha yao ya kimwili kama anavyohukumiwa kila mmoja, walihubiriwa Habari Njema kusudi katika maisha yao ya kiroho waishi kama aishivyo Mungu.
7 Всем же кончина приближися. Уцеломудритеся убо и трезвитеся в молитвах.
Mwisho wa vitu vyote umekaribia. Kwa hiyo mnapaswa kuwa na utaratibu na nidhamu, ili mweze kusali.
8 Прежде же всех друг ко другу любовь прилежну имейте, зане любовь покрывает множество грехов.
Zaidi ya yote pendaneni kwa moyo wote, maana upendo hufunika dhambi nyingi.
9 Страннолюбцы друг ко другу, без роптании.
Muwe na ukarimu ninyi kwa ninyi bila kunung'unika.
10 Кийждо якоже прият дарование, между себе сим служаще, яко добрии строителие различныя благодати Божия.
Kila mmoja anapaswa kutumia kipaji alichojaliwa na Mungu kwa faida ya wengine, kama vile uwakili mwema wa zawadi mbalimbali za Mungu.
11 Аще кто глаголет, яко словеса Божия: аще кто служит, яко от крепости, юже подает Бог: да о всем славится Бог Иисус Христом, Емуже есть слава и держава во веки веков. Аминь. (aiōn g165)
Anayesema kitu, maneno yake na yawe kama maneno ya Mungu; anayetumika anapaswa kutumikia kwa nguvu anayojaliwa na Mungu, ili katika mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu na nguvu ni vyake milele na milele! Amina. (aiōn g165)
12 Возлюбленнии, не дивитеся еже в вас раждежению ко искушению вам бываему, яко чужду вам случающуся:
Wapenzi wangu, msishangae kuhusu majaribio makali mnayopata kana kwamba mnapatwa na kitu kisicho cha kawaida.
13 но понеже приобщаетеся Христовым страстем, радуйтеся, яко да и в явление славы Его возрадуетеся веселящеся.
Ila furahini kwamba mnashiriki mateso ya Kristo ili mweze kuwa na furaha tele wakati utukufu wake utakapofunuliwa.
14 Аще укоряеми бываете о имени Христове, блажени есте яко Славы и Божий Дух на вас почивает: онеми убо хулится, а вами прославляется.
Heri yenu ikiwa mnatukanwa kwa sababu ya jina la Kristo; jambo hilo lamaanisha kwamba Roho mtukufu, yaani Roho wa Mungu, anakaa juu yetu.
15 Да не кто убо от вас постраждет яко убийца, или яко тать, или яко злодей, или яко чуждопосетитель:
Asiwepo mtu yeyote miongoni mwenu ambaye anapaswa kuteseka kwa sababu ni muuaji, mwizi, mhalifu au mwovu.
16 аще ли же яко Христианин, да не стыдится, да прославляет же Бога в части сей.
Lakini kama mtu akiteseka kwa sababu ni Mkristo, basi asione aibu, bali amtukuze Mungu, kwa sababu mtu huyo anaitwa kwa jina la Kristo.
17 Яко время начати суд от дому Божия: аще же прежде от вас, кая кончина противящымся Божию Евангелию?
Wakati wa hukumu umefika, na hukumu hiyo inaanza na watu wake Mungu mwenyewe. Ikiwa hukumu hiyo inaanzia kwetu sisi, basi mwisho wake utakuwa namna gani kwa wale wasioamini Habari Njema ya Mungu?
18 И аще праведник едва спасется, нечестивый и грешный где явится?
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Ni vigumu kwa watu waadilifu kuokolewa; itakuwaje basi kwa wasiomcha Mungu na wenye dhambi?”
19 Темже и страждущии по воли Божией, яко верну Зиждителю да предадят душы своя во благотворении.
Kwa hiyo, wale wanaoteseka kufuatana na matakwa ya Mungu, wanapaswa, kwa matendo yao mema, kujiweka chini ya Muumba wao ambaye ni wa kuaminika kabisa.

< Первое послание Петра 4 >