< 4 Мојсијева 28 >

1 Још рече Господ Мојсију говорећи:
Bwana akamwambia Mose,
2 Заповеди синовима Израиљевим, и реци им: Приносе моје, хлеб мој, жртве што ми се сажижу за угодни мирис, пазите да ми приносите на време.
“Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’
3 Реци им дакле: Ово је жртва огњена што ћете приносити Господу: два јагњета од године здрава, сваки дан на жртву паљеницу без престанка.
Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku.
4 Једно јагње принеси ујутру, а друго јагње принеси увече.
Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni,
5 И десетину ефе белог брашна за дар смешаног с четвртином ина чистог уља.
kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini ya mafuta ya zeituni.
6 То је жртва паљеница свагдашња, која би принесена на гори Синајској за мирис угодни, жртва огњена Господу.
Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
7 И налив њен да буде четврт ина на свако јагње; у светињи приноси налив доброг пића Господу.
Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu.
8 А друго јагње принеси увече; дар као ујутру и налив његов принеси за жртву огњену, за угодни мирис Господу.
Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
9 А у суботу два јагњета од године здрава, и две десетине белог брашна смешаног с уљем за дар с наливом његовим.
“‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta.
10 То је суботна жртва паљеница сваке суботе, осим свагдашње жртве паљенице и налива њеног.
Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.
11 И у почетак месеца својих приносите Господу жртву паљеницу, по два телета и једног овна и седам јагањаца од године здравих;
“‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari.
12 И три десетине белог брашна помешаног с уљем за дар на свако теле, и две десетине белог брашна помешаног с уљем за дар на овна;
Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa, uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta;
13 И по једну десетину белог брашна помешаног с уљем за дар на свако јагње; то је жртва паљеница на угодни мирис, жртва огњена Господу.
pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana.
14 А налив њихов да буде вина по ина на теле, трећина ина на овна, и четврт ина на јагње. То је жртва паљеница у почетак месеца, сваког месеца у години.
Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini, na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka.
15 И јарца једног за грех, осим свагдашње жртве паљенице, приносите Господу с наливом његовим.
Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.
16 А првог месеца четрнаести дан да је пасха Господу;
“‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana.
17 А петнаести дан тог месеца празник: седам дана једите пресне хлебове.
Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu.
18 Први дан нека је сабор свети; никакав посао ропски не радите.
Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida.
19 Него принесите Господу жртву паљеницу, два телета и једног овна и седам јагањаца од године, све да вам је здраво;
Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari.
20 А дар уз њих белог брашна помешаног с уљем три десетине уза свако теле и две десетине уз овна принесите.
Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa;
21 По једну десетину принесите уза свако јагње од оних седам јагањаца;
pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa.
22 И једног јарца за грех, ради очишћења вашег.
Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu.
23 То принесите осим јутарње жртве паљенице, која је жртва свагдашња.
Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi.
24 Тако приносите сваки дан за оних седам дана, да буде јело, жртва огњена на угодни мирис Господу, осим свагдашње жртве паљенице и њен налив приносите.
Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji.
25 И седми дан да имате свети сабор; посао ропски ниједан не радите.
Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
26 И на дан првина, кад приносите нов дар Господу после својих недеља, да имате сабор свети, ниједан посао ропски не радите;
“‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.
27 Него принесите жртву паљеницу за угодни мирис Господу, два телета, једног овна седам јагањаца од године;
Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
28 И дар уз њих: белог брашна помешаног с уљем по три десетине уз теле, две десетине уз овна,
Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini;
29 По једну десетину уза свако јагње од оних седам јагањаца;
na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba.
30 Једног јарца, ради очишћења вашег.
Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
31 Принесите то, осим свагдашње жртве паљенице и дара њеног; а све нека вам је здраво с наливом својим.
Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.

< 4 Мојсијева 28 >