< Књига Исуса Навина 21 >

1 Тада дођоше главари отачких породица левитских к Елеазару свештенику и к Исусу сину Навином и главарима породица отачких и племенима синова Израиљевих.
Kisha wakuu wa koo za Walawi walimwendea Eliazari kuhani, na kwa Yoshua mwana wa Nuni, na kwa viongozi wa familia za mababu zao miongoni mwa watu wa Israeli.
2 И рекоше им у Силому у земљи хананској говорећи: Господ је заповедио преко Мојсија да нам се дају градови где ћемо живети и подграђа њихова за стоку нашу.
Waliwaambia, “Yahweh aliwaagizeni ninyi kwa mkono wa Musa kwamba mtupatieni miji ya kuishi yenye maeneo kwa ajili ya kuchungia ya mifugo.” waliyasema haya huko Shilo katika nchi ya Kanaani.
3 И дадоше синови Израиљеви Левитима од наследства свог по заповести Господњој ове градове и подграђа њихова:
Hivyo, kwa agizo la Yahweh, watu wa Israeli waliwapa Walawi kutoka katika urithi wa wao miji ifuatayo pamoja na maeneo yao ya kuchungia.
4 Изађе жреб за породице Катове; и допаде синовима Арона свештеника између Левита жребом тринаест градова од племена Јудиног и од племена Симеуновог и од племена Венијаминовог.
Upigaji wa kura kwa ajili ya koo za Wakohathi ulileta matokeo haya: makuhani ambao ni wazawa wa Haruni ambao walitokana na Walawi, walipokea miji kumi na mitatu waliopewa kutoka kwa kabila la Yuda, kutoka kabila la Simoni, na kutoka kabila la Benyamini.
5 А осталим синовима Катовим допаде жребом десет градова од породица племена Јефремовог и од племена Дановог и од половине племена Манасијиног.
Koo zilizobaki za Wakohathi walipokea kwa kupiga kura kwa miji kumi kutoka katika kabila za Efraimu, Dani, na kutoka kwa nusu ya kabila la Manase.
6 А синовима Гирсоновим допаде жребом од породица племена Исахаровог и од племена Асировог и од племена Нефталимовог и од половине племена Манасијиног у Васану тринаест градова;
Na watu wazawa wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kwa kupigiwa kura kutoka kwa koo za kabila la Isakari, Asheri, Nafutali, na nusu ya kabila la Manase katika Bashani.
7 Синовима Мераријевим по породицама њиховим од племена Рувимовог и од племена Гадовог и од племена Завулоновог дванаест градова.
Watu waliokuwa wazawa wa Merari walipokea miji kumi na miwili kutoka katika makabila ya Rubeni, Gadi na Zabuloni.
8 Даше дакле синови Израиљеви Левитима те градове и подграђа њихова жребом, као што беше заповедио Господ преко Мојсија.
Basi, watu wa Israeli waliwapa Walawi miji hii pamoja na maeneo yao ya kuchungia, kwa kupiga kura, kama vile Yahweh alivyokuwa ameagiza kwa mkono wa Musa.
9 И даше од племена синова Јудиних и од племена синова Симеунових ове градове који се казују по именима:
Kutoka kwa makabila la Yuda na Simoni, waliwapa nchi katika miji ifuatayo iliyoorodheshwa kwa majina.
10 И допаде синовима Ароновим од породица Катових између синова Левијевих, за које паде први жреб,
Miji hii walipewa wazawa wa Haruni, ambao walikuwa miongoni mwa koo za Wakohathi, ambao walitoka katika kabila la Lawi. Kwa kuwa upigaji wa kura ya kwanza uliwaangukiwa wao.
11 Њима допаде: Киријат-Арва, а Арва је отац Енаков, а тај је град Хеврон у гори Јудиној, с подграђем својим унаоколо.
Waisraeli waliwapatia Kiriathi Arba ( Arba alikuwa ni baba wa Anaki), eneo hilo liliitwa pia Hebroni, katika nchi ya milima ya Yuda, pamoja na maeneo ya kulishia mifugo yaliyouzunguka mji.
12 А поље око тог града и села његова даше Халеву сину Јефонијином у наследство.
Lakini mashamba ya mji na vijiji vyake vilikuwa tayari ameshapewa Kalebu mwana Yefune, kama mali yake.
13 Даше дакле синовима Арона свештеника град за уточиште крвнику Хеврон с подграђем и Ливну с подграђем.
Na kwa wana wa Haruni kuhani, waliwapa Hebroni pamoja na eneo lake la kulishia mifugo ambao ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia na Libna pamoja na maeneo ya kulishia mifugo.
14 И Јатир с подграђем и Естемоју с подграђем,
Na Yatiri pamoaja na maeno yake ya kuchungia, na Eshitemoa pamoja na maeneo yake ya malisho.
15 И Олон с подграђем и Давир с подграђем,
Lakini pia waliwapa Holoni pamoja na maeneo yake ya malisho, Debiri pamoja na maeneo yake ya malisho,
16 И Ајин с подграђем, и Јуту с подграђем, и Вет-Семес с подграђем: девет градова од та два племена.
Aini pampoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Shemeshi pamoja na maeneo yake ya malisho. Ilikuwa ni miji kumi na tisa ambayo walipewa kutoka katika makabila haya mawilil.
17 А од племена Венијаминовог Гаваон с подграђем, и Гавају с подграђем,
Kutoka katika kabilala Benyamini walipewa Gibea pamoja na maeneo yake ya malisho, na Geba pamoja na maeneo yake ya malisho,
18 Анатот с подграђем, и Алмон с подграђем: четири града.
na Anathothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na amoni pamoja na vitongoji vyake vinne.
19 Свега градова синова Арона свештеника тринаест градова с подграђима.
Miji waliyopewa makuhani, wana wa Haruni, ilikuwa ni miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumlisha na maeneo yake ya malisho.
20 А породицама синова Катових, Левитима, што их још беше од синова Катових, допадоше на њихов жреб градови од племена Јефремовог;
Na kwa ajili ya sehemu ya familia ya Kohathi iliyosalia, wale Walawi walio wa familia ya Kohathi, walipewa miji kutoka katika kabila la Efraimu kwa kupiga kura.
21 Допаде им град за уточиште крвнику Сихем с подграђем у гори Јефремовој, и Гезер с подграђем,
Walipewa Shekemu pamoja na maeneo yake ya malisho katika nchi ya milima ya Efraimu - mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu bila kukusudia, na Gezeri pamoja na maeneo yake ya malisho,
22 И Кивсајим с подграђем, и Вет-Орон с подграђем: четири града;
na Kibzaimu pamoja na maeneo yake ya malisho, na Bethi Horoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa miji minne kwa ujumla wake.
23 А од племена Дановог: Елтекон с подграђем, Гиветон с подграђем,
Kutoka katika kabila la Dani, ukoo wa Kohathi ulipewa Elteke pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gibethoni pamoja na maeneo yake ya malisho, na
24 Ајалон с подграђем, Гат-Римон с подграђем: четири града.
Aijaloni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Gathrimoni pamoja na maeneo yake ya malisho, ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake.
25 А од половине племена Манасијиног: Танах с подграђем и Гат-Римон с подграђем: два града.
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, ukoo wa Kohathi walipewa miji miwili - Taanaki pamoja na maeneo yake ya malisho na Gathirimoni pamoja na maeneo yake ya malisho.
26 Свега десет градова с подграђима дадоше породицама синова Катових осталима.
Kulikuwa na miji kumi kwa ujumla wake kwa ajili ya koo zilizosalia za Wakohathi, pamoja na maeneo yao ya malisho.
27 А синовима Гирсоновим између породица левитских дадоше од половине племена Манасијиног град за уточиште крвнику Голан у Васану с подграђем, и Вестер с подграђем: два града;
Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, jamaa za Gershoni, ambazo hizi zilikuwa ni koo zingine za Walawi, zilipewa Golani katika Bashani pamoja na maeneo yao ya malisho, ni mji wa makimbilio kwa ajili ya mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia, sambamba na Beeshitera pamoja na maeneo yake ya malisho - ilikuwa miji miwili kwa ujumla.
28 А од племена Исахаровог: Кисон с подграђем, Даврот с подграђем.
Koo za Gershoni zilipewa pia miji minne kutoka kwa kabila la Isakari - Kishoni sambamba na maeneo yake ya malisho, Daberathi pamoja na maeneo yake ya malisho,
29 Јармут с подграђем, Ен-Ганим с подграђем: четири града;
Yarmuthi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Engnimu pamoja na maeneo yake ya malisho.
30 А од племена Асировог: Мисал с подграђем, Авдон с подграђем,
Kutoka katika kabila la Asheri, walipewa miji minne kwa ujumla - Mishali pamoja na maeneo yake ya malisho, Abdoni pamoja na maeneo yake ya malisho,
31 Хелкат с подграђем, и Реов с подграђем: четири града;
Helikathi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Rehobu pamoja na maeneo yake ya malisho.
32 А од племена Нефталимовог град за уточиште крвнику Кедес у Галилеји с подграђем, и Амот-Дор с подграђем, и Картан с подграђем: три града.
Kutoka kwa kabila la Nafutali, nasaba za Gershoni walipewa miji mitatu kwa ujumla - Kedeshi katika Galilaya pamoja na maeneo yake ya malisho, ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu yeyote aliyeua mtu bila kukusudia; na Hamothidori pamoja na maeneo yake ya malisho, na Kartani pamoja na maeneo yake ya malisho.
33 Свега градова синова Гирсонових по породицама њиховим тринаест градова с подграђима.
Kulikuwa na miji kumi na mitatu kwa ujumla, kujumuisha na maeneo yake ya malisho, kwa ajili ya koo za Gershoni.
34 А породицама синова Мераријевих, осталим Левитима, даше од племена Завулоновог Јокнеам с подграђем, Карту с подграђем,
Na kwa Walawi waliosalia, koo za Merari waliokuwa wamepewa kutoka katika kabila la Zabuloni: Yokneamu pamoa na maeneo yake ya marisho, Karta pamoja na maeneo yake ya malisho,
35 Димну с подграђем, Налол с подграђем: четири града;
Dimna pamoja na maeneo yake ya malisho, na Nahalali pamoja na maeneo yake ya malisho- ilikuwa ni miji minne kwa ujumla.
36 А од племена Рувимовог: Восор с подграђем, и Јазу с подграђем,
Kwa mbari za Merari walipewa miji minne kutoka katika kabila la Rubeni: Bezeri pamoja na maeneo yake ya malisho, Yahazi pamoja na maene yake ya malisho,
37 Кедимот с подграђем, и Мифат с подграђем: четири града;
na Kedemothi pamoja na maeneo yake ya malisho, na Mefaathi pamoja na maeneo yake ya malisho.
38 А од племена Гадовог: град за уточиште крвнику Рамот у Галаду с подграђем, и Маханајим с подграђем.
Kutoka katika kabila la Gadi walipewa miji ya Ramothi katika Gileadi pamoja na sehemu zake za malisho - huu ulikuwa ni mji wa makimbilio kwa mtu aliyeua mtu mwenzake bila kukusudia - na Mahanaimu pamoja na sehemu zake za malisho.
39 Есевон с подграђем, Јазир с подграђем; свега четири града.
Koo za Merari zilipewa pia Heshiboni pamoja na maeneo yake ya malisho, na Yazeri pamoja na malisho yake.
40 Све ове градове даше синовима Мераријевим по породицама њиховим, што још беху између породица левитских; и дође на жреб њихов дванаест градова.
Hii ilikuwa ni miji minne kwa ujumla wake. Hii yote ilikuwa ni miji ya koo kadhaa za Merari, ambao walitoka katika kabila la Lawi, miji kumi na miwili walipewa wao kwa kupiga kura.
41 Свега градова левитских у наследству синова Израиљевих беше четрдесет осам градова с подграђима.
Miji waliyopewa Walawi kutoka katikati ya nchi iliyomilikiwa na watu wa Israeli ilikuwa miji arobaini na nane, kujumuisha na sehemu za malisho yao.
42 А сви градови имају своја подграђа унаоколо; тако је у сваком граду.
Miji hii kila mmoja ulikuwa na maeneo yake ya malisho kwa kuuzunguka mji. Miji hii yote ilikuwa hivyo.
43 Тако даде Господ Израиљу сву земљу, за коју се закле оцима њиховим да ће им је дати, и наследише је и населише се у њој.
Basi Yahweh aliwapa Israeli nchi yote ambayo aliwaapia baba zao kuwa atawapa. Waisraeli waliimiliki nchi na wakakaa humo.
44 И умири их Господ од свуда унаоколо, као што се заклео оцима њиховим; и нико се не одржа пред њима од свих непријатеља њихових; све непријатеље њихове предаде им Господ у руке.
Kisha Yahweh akawapa pumziko kwa kila upande, kama tu alivyowaahidia baba zao. Hakuna hata adui mmoja atakayeweza kuwashinda. Yawhew aliwatia maadui wao wote mikononi mwao.
45 Ништа не изоста од свег добра што беше обећао Господ дому Израиљевом; све се зби.
Hakuna hata kitu kimoja miongoni kwa ahadi nzuri ambazo Yahweh alizisema kwa nyumba ya Israeli ambazo hazikutimia. Ahadi zote zilitimia.

< Књига Исуса Навина 21 >